MISS EAST AFRICA RWANDA LEO SERENA HOTEL!!

Kamati ya Miss East Africa, ikiwa pamoja na Waziri wa Jumuiya ya AfrikaMashariki Rwanda, Madame Monique Mukaruliza (mwenye suti) pamoja nawarembo wanaowania shindano la Miss East Africa Rwanda. kulia kwa wazirini Bosi wa Udhamini, Matukio na Uhusiano wa New Habari (2006) Limited,Petter Mwendapole, wakati kushoto ni Rena Callist na Adam Kapama kutokaRena Events.
Wasichana wanaoshiriki shindano la Miss East Africa wakiwakatika picha ya pamoja

WASICHANA 12 leo wanatarajia kupanda jukwaani katika hoteli ya Serenamjini hapa kwa ajili ya kuwania taji la Miss East Africa Rwanda.Mshindi wa kwanza na wa pili katika shindano hilo watawakilisha Rwandakatika fainali za Miss East Africa zitakazofanyika Desemba 18 mwaka mjiniDar es Salaam.
Mshindi wa shindano la leo ataondoka na kitita cha faranga za Rwandamilioni moja sawa na karibu sh milioni tatu za kitanzania.Mshindi wa pili ataondoka na Faranga mia tano sawa na karibu milioni mojana nusu za Kitanzania.Tayari Kamati ya Miss East Africa makao makuu iko mjini hapa kwa ajili yakushuhudia shindano hilo ambapo Jaji mkuu usiku wa leo atakuwa RenaCallist, mkurugenzi wa Rena Events.Pia Miss East Africa, anayemaliza muda wake,
Claudia Niyonzima atakuwepokushuhudia shindano hili pamoja na Miss Burundi wa mwaka jana AliceKaneza.Wakati shindano hilo linashirikisha warembo hao 12, mchuano mkali zaidiunaonekana kuwahusisha warembo wanne ambao wanachuana kwa vitu vingi.Nafasi kubwa sana inaonekana kwenda kwa Sabrina kaganza, Leticiaumuizayire, Annet Mahoro na Cynthia Akazuba.Lakini pamoja na hao wanne msichana mwingine ambaye anaweza kufanyamaajabu usiku wa leo ni Viviane Umulisa.
Warembo hao juzi walikutana na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo wahapa, Joseph Habineza ‘Mr Joe’. Jana pia walikutana na Waziri wa AfrikaMashariki wa hapa Monique Mukaruliza.Warembo wengine ambao wanashiriki shindano hilo ni pamoja na ClariseIshimwe, Rita Uwera, Pamela Ungabire, Clarise Ushuti na SoniaUwambambazi,

Maradona recalls Cambiasso!!

Argentina coach Diego Maradona.
Argentina coach Diego Maradona has called-up midfielder Esteban Cambiasso for the first time ahead of next month's international friendly against Spain in Madrid. Cambiasso, 29, had been a regular for Argentina, winning 45 caps for his country before Maradona took charge of the national team last November.
The Inter Milan midfielder was overlooked for the final eight games of a stuttering 2010 FIFA World Cup South Africa™ qualifying campaign, during which Maradona came under increasing pressure for his high rotation of players. Argentina only secured their place at next summer's finals with a 1-0 win over Uruguay in their final game.
Cambiasso is joined in being recalled to the national team by Real Madrid's Fernando Gago and Atletico Madrid's Maxi Rodriguez, both of whom missed the crucial match in Montevideo. Maradona, who turned 49 on Friday, also sprung a surprise by including uncapped left-back Cristian Ansaldi, who plays for Russian champions Rubin Kazan.
Argentina meet Spain in their friendly at the Vicente Calderon in Madrid on 14 November.
Argentina squadGoalkeepers: Sergio Romero (AZ Alkmaar/The Netherlands), Mariano Andujar (Catania/Italy)
Defenders: Fabricio Coloccini (Newcastle United/England), Martin Demichelis (Bayern Munich/Germany), Gabriel Heinze (Marseille/France), Nicolas Pareja (Espanyol/Spain), Cristian Ansaldi (Rubin Kazan/Russia)
Midfielders: Jonas Gutierrez (Newcastle United/England), Maximiliano Rodriguez (Atletico Madrid/Spain), Javier Mascherano (Liverpool/England), Fernando Gago (Real Madrid/Spain), Esteban Cambiasso (Internazionale/Italy), Angel Di Maria (Benfica/Portugal), Pablo Aimar (Benfica/Portugal)
Forwards: Lionel Messi (Barcelona/Spain), Gonzalo Higuain (Real Madrid/Spain), Carlos Tevez (Manchester City/England), Sergio Aguero (Real Madrid/Spain), Ezequiel Lavezzi (Napoli/Italy) story by http://www.fifa.com/

Wanafunzi 592 wameacha shule wilayani Nkasi kwa kipindi cha miaka miwili!!

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akisalimiana na wanafunzi katika moja ya shule alizowahi kuziutembelea.
Na Anna Nkinda - Maelezo, Nkasi
31/10/2009 Wanafunzi 592 wameacha shule wilayani Nkasi kutokana na tatizo la utoro, mimba, kukosa mahitaji na kuugua kwa kipidi cha miaka miwili na hivyo kusababisha kupungua kwa idadi ya wanafunzi wanaomaliza elimu ya shule ya msingi na sekondari wilayani humo.
Hayo yamesemwa jana na Mkuu wa wilaya hiyo Joyce Mgana wakati akisoma taarifa ya utekelezaji wa shughuli za maendeleoa ya wilaya kwa Mke wa Rais Mama Salma Kikwete aliyepo ziara ya kikazi ya siku tatu wilayani humo.
Mgana alisema kuwa tangu mwaka 2008 hadi sasa wanafunzi wa shule ya msingi alioacha masomo ni 226 kati ya hao wasichana ni 102 na wavulana 124 na katika shule za sekondari wanafunzi 366 waliacha masomo wakiwemo wasichana 195 na wavulana 171.
"Kuanzia mwaka 2008 hadi sasa wanafunzi 17 wa shule za msingi na wanafunzi 69 kwa upande wa sekondari walipata ujauzito na kesi zao zinaendelea mahakamani, kitendo hiki kinasababisha kwa kiasi kikubwa kushusha maendeleo ya mtoto wa kike", Mgana alisema.
Ili kukabiliana na tatizo la wanafunzi wa kike kupata ujauzito wilaya hiyo iko katika mkakati wa kujenga Hosteli mpya za wasichana zisizopungua tano kwa kila mwaka hadi sasa jumla ya Hosteli saba zinatarajiwa kukamilika kujengwa katika mwaka 2009/ 10.
Mkuu wa wilaya hiyo alisema kuwa, "Kuhusiana na tatizo la utoro mashuleni wanafunzi katika wilaya hii wanakula chakula cha mchana shuleni jambo ambalo limesaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza tatizo hili".
Wilaya hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali katika sekta ya elimu ikiwa ni pamoja na ongezeko la watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu kwani hadi sasa katika shule za msingi kuna watoto yatima 4766 kati yao wasichana ni 2362 na wavulana 2404
Kwa upande wake Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) aliwataka wakazi wa wilaya hiyo kuhakikisha kuwa watoto wao wanasoma na kufuatilia maendeleo yao mashuleni.
"Ninawasihi kina baba na kina mama msipokee mahari ya watoto wenu msubiri hadi matokeo ya mtihani yametoka kama mtoto amefeli na mzazi anao uwezo wa kumsomesha katika shule ya kulipia ni bora ukampeleka mwanao shuleni kuliko kumuoza jambo ambalo litarudisha nyuma maendeleo yake ", alisema Mama Kikwete.
Aliendelea kusema kuwa Serikali ina makusudi ya kuanzisha shule za Sekondari za kata na kuongeza idadi ya shule za Msingi ili watoto wetu wasome na kupata wataalamu wengi ambao watasaidia kupunguza tatizo la wataalamu tulilonalo hivi sasa.
Wilaya hiyo ina shule za msingi 97 na shule za sekondari za Serikali 18 zilizojengwa kwa kushirikiana na wananchi, jumla ya wanafunzi katika shule za sekondari ni 6066 wasichana 2053 na wavulana 4013 na katika shule za msingi ni 49,428 kati ya hao wavulana ni 24,682 na wasichana ni 24,746.
Taasisi ya WAMA ilivichangia vikundi vya wanawake wajasiriamali vilivyopo wilayani humo Tshs. 1,500,000/= na Umoja wa Wanawake (UWT) Tshs. 500,000 fedha ambazo zitatumika kuinua mitaji ya vikundi hivyo.

Rais Kikwete azindua kliniki ya meno Ilembo!!

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kuzindua rasmi kliniki inayotembea(Mobile Health Lab) kwaajili ya kutoa huduma za upimaji ukimwi na huduma nyinginezo za kimaabara katika uwanja wa Shule ya Msingi Ilembo, Mbeya vijijini.Wengine katika picha kushoto ni Mwakilishi wa Jumuiya ya Ulaya Dr.Inge Baumgarten na kulia ni afisa kutoka taasisi ya jeshi la Marekani ya Walter Reed Army Institute Bwana Edward Sekonde(picha na Freddy Maro)..
Mganga wa meno katika kliniki ya Meno kata ya Ilembo wilaya ya Mbeya vijijini Dr.Marietha Sanga akimpa maelezo Rais Jakaya Mrisho Kikwete jinsi mitambo mipya ya kuhudumia wagonjwa wa meno inavyofanyakazi muda mfupi baada ya Rais Kikwete kuzindua kliniki hiyo jana.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na wafanyakazi wa kujitolea kutoka taasisi ya American Peace Corps Meesh Santoro(wapili kushoto) anayeishi kata ya Ilembo na Jenna Covey anayeishi Isangati Mbeya vijijini muda mfupi baada ya Rais Kikwete kuwahutubia wakazi wa kata ya Ilembo,wilaya ya Mbeya vijijini jana mchana
Sehemu ya umati wa wananchi wa Kata ya Ilembo wakimsikiliza Rais Jakaya Mrisho Kikwete alipokuwa akiwahutubia katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa michezo wa shule ya Msingi Ilembo,wilaya ya Mbeya vijijini.





Big Brother Revolution: Images from Day 53 - THURSDAY OCTOBER 29!!

Day 53 on M-Net’s Big Brother Revolution and the question that surely was on the housemates minds…is Big Brother ever coming back?
Having received a note from Big Brother on Monday saying that the housemates are on their own as they had failed to inspire Biggie, and with telephonic access to a call centre where no-one picks up the phone, the housemates were still waiting and wondering…
And on Thursday night, the housemates created their own task and presented a performance sketch…but was Biggie watching?
Tune in to Big Brother Revolution on DStv channel 198 or 199 and for more information, log on to www.mnetafrica.com/bigbrother.

JESHI LA POLISI KUENDELEA KUTOA TUZO KWA ASKARI NA WANANCHI!!

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Said Mwema akimtunuku nishani heshima Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam William kutokana na mchango wake wa kushirikiana na Jeshi la polisi kukabiliana na masuala mbalimbali wakati wa sherehe za kuwatunuku nishani maafisa polisi, askari na raia (wafanyabiashara) waliotoa michango mbalimbali kulisaidia jeshi la polisi leo jijini Dar es salaam.
(Picha, Habari na Aron Msigwa- MAELEZO).

30/10/2009, Dar es salaam.
Jeshi la Polisi limesema kuwa litaendelea kutoa tuzo kwa askari , raia na wafanyabiashara wanaotoa michango mbalimbali na kushirikiana na Jeshi hilo katika kufanikisha vita dhidi ya vitendo vya uhalifu nchini.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Said Mwema wakati wa sherehe za kuwatunuku nishani maafisa polisi na askari walioshiriki katika oparesheni za kulinda amani nchi Comoro na raia wema (wafanyabiashara) waliotoa michango mbalimbali ili kuliwezesha Jeshi la polisi kutekeleza majukumu yake ipasavyo.
Amesema mpango huo wa utoaji tuzo kwa wafanyakazi bora wa jeshi la polisi, raia na wafanyabiashara wanaoshirikiana na Jeshi la Polisi unatokana na jeshi kutambua mchango mkubwa walioutoa na wanaoendelea kuutoa katika kuboresha utendaji kazi ndani ya jeshi.
Amefafanua kuwa Jeshi la Polisi litaendelea kuwathamini askari wake kwa kuwapa motisha ili kuhakikisha kuwa ulinzi na usalama ndani ya nchi unaimarishwa.
“Hata tukiwa na magari, tuwe na ndege ni lazima tuthamini askari wetu kuliko kitu kingine ili kuhakikisha ulinzi na usalama pamoja na maisha bora kwa kila mtanzania yanapatikana” amesema.
Ameongeza kuwa viongozi wa Jeshi wataendelea kukaa pamoja ili kuvipima, kuviibua na kuviendeleza vithaminiwa vya polisi pamoja na kutoa zawadi kwa askari wanaofanya kazi nzuri ya kulinda mali na maisha ya raia ikiwa ni sehemu ya kuthamini mchango wao na kuwapa sifa stahiki.
Kuhusu Jeshi la Polisi kuendelea kushirikiana na raia wote katika Nyanja ya ulinzi shirikishi amesema kuwa Jeshi la Polisi linaandaa utaratibu ili kuhakikisha kuwa raia wote wanashiriki kikamilifu katika kujilinda wenyewe mahali wanakoishi pamoja na kuaandaa askari na maafisa wa polisi wa kudumu watakaoshirikiana na vikundi maalum vya ulinzi vitakavyoanzishwa katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es salaam.
Kwa upande askari waliotunukiwa nishani kwa kushiriki harakati za kulinda amani nchini Comoro Generali Mwema amesema ni mfano wa kuigwa kwani walifanya kazi katika nchi tofauti na waliyoiazoea pamoja na kushirikiana kikamilifu na askari kutoka katika nchini nyingine zilizoshiriki operesheni za ulinzi wa amani nchini Comoro.
Hata hivyo amesema Jeshi la Polisi liko makini kuhakikisha kuwa mafunzo ya askari yanaboreshwa ili kuwawezesha askari kufanya kazi kikamilifu watokapo mafunzoni hatua hii ikijumuisha mpango wa kuongeza mafunzo kivitendo zaidi kwa askari kwenye maeneo ya raia.
Mbali na hilo amesema Jeshi la Polisi linaendelea kufanya marekebisho kwa kuwawezesha kielimu askari wake ili kuwajengea uwezo na kulifanya kuwa la kisasa zaidi na lenye wataalam wa kutosha na hivyo kuongeza ufanisi katika majukumu ya kila siku.
Aidha ametoa wito kwa wananchi na kushirikiana na jeshi la Polisi katika kutimiza wajibu wake kwa ulinzi shirikishi na kuongeza kuwa mpango wa utoaji tuzo kwa wafanyakazi wa jeshi la polisi, raia na wafanyabiashara wanaoshirikiana na Jeshi la Polisi utaboresha mawasiliano na ushirikiano zaidi.

WAPENDA MAENDELEO KUCHANGIA (VICOBA) WILAYANI MISENYI!!

Mwenekiti wa UWT Umoja wa wanawake wa CCM Wilaya ya Misenyi Mkoani Kagera Mrs. Assumpter Mshama akizungumza katika mkutano na wanahabari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo jana wakati alipokuwa akitangaza hafla ya chakula cha jioni kuchangia mfuko wa VICOBA Wilayani Misenyi itakayofanyika kesho kwenye Hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam, wapenda maendeleo wote wanaalikwa kwa ajili ya kusaidia mfuko huo wa VICOBA katika kusaidia na kuwaondoa kwenye lindi la umasikini wanawake wa Wilaya hiyo katika hafla hiyo mgeni rasmi atakuwa ni Naibu kamishna wa TRA Janerose Mateyunga.

Rais Kikwete aweka jiwe la msingi kituo cha Watoto yatima Rungwe!!

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Lucy Hope Centre Bi.Lucy Mwandosya pamoja na Waziri wa Maji Profesa Mark Mwandosya muda mfupi baada ya kuwahutubia wananchi wa Lufilyo,Rungwe wakati wa uwekaji jiwe la Msingi katika jingo la taasisi hiyo uliofanyika jana.Taasisi ya lucy Hope inawahudumia watoto Yatima.(picha na Freddy Maro).

Rais Jakaya Mrisho Kikwete,mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Lucy Hope Centre Bi.Lucy Mwandosya na Waziri wa Maji Profesa Mark Mwandosya wakishangalia wakati wa hafla ya kuweka jiwe la Msingi katika jingo la taasisi hiyo iliyofanyika huko Lufilyo,Rungwe, mkoani Mbeya jana jioni.Taasisi ya Lucy Hope inawahudumia watoto Yatima kwa kuwalea na kuwapa elikmu katika ngazi mbalimbali

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Lucy Hope Centre Bi.Lucy Mwandosya na Mumwewe Profesa Mark Mwandosya wakimkabidhi picha iliyochorwa na Bi.Lucy mwandosya inayoonesha ngoma ya utamaduni ya Rungwe wakati wa hafla ya kuweka jiwe la msingi katika jengo la taasisi hiyo huko Lufilyo Rungwe jana jioni.

MAJENGO YAJENGWA SHULE YA SEKONDARI MPANDA!!

Na Nkinda - Maelezo, Mpanda
30/10/2009 Serikali imetoa jumla ya Tshs. 52,000,000/= kwa ajili ya ujenzi wa madarasa manne, choo matundu sita na nyumba moja ya mwalimu katika shule ya Sekondari ya wasichana ya Mpanda.
Hayo yamesemwa jana na Mkuu wa shule hiyo Mwalimu Nyabise Sabasi wakati akitoa taarifa ya shule hiyo kwa Mke wa Rais Mama Salma Kikwete aliyetembelea shuleni hapo kwa ajili ya kuongea na wanafunzi wa kike wa wilaya ya Mpanda katika mkoa wa Rukwa.
Mwalimu Sabasi alisema kuwa katika utekelezaji wa ujenzi wa miradi hiyo shule imetoa mchango wake kwa kufyatua matofali laki moja na thelathini elfu. Pia shule iliandaa harambee kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa elimu ambapo zilipatikana Tshs.4,549,000/= ila bado kuna upungufu wa Tshs. 25, 595,145/= ili ujenzi wa miradi hiyo uweze kukamilika.
Shule hiyo inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na upungufu wa mabweni manne kwani shule hiyo ilijengwa kwa ajili ya kulala wanafunzi 320 lakini hivi sasa kuna wanafunzi 640 kutokana na tatizo hilo shule inatumia baadhi ya vyumba vya madarasa kuwa mabweni.
Aliendelea kuzitaja changamoto zingine kuwa ni ongezeko la wanafunzi yatima na wanaotoka katika mazingira magumu kwani hivi sasa shule hiyo ina wanafunzi 33 ambao hupata shida mbalimbali na kukosa mahitaji muhimu, baadhi yao hulazimika kubaki shuleni kwa vipindi vyote vya likizo lakini kuna wengine wanaacha shule kwa sababu ya maisha duni na wengine hulazimika kuingia kwenye vitendo viovu wakidhani kuwa watapata mahitaji muhimu kwa maisha.
"Tunakabiliwa na upungufu wa madarasa matatu,, upungufu wa nyumba za wafanyakazi, upungufu wa vitendea kazi vinavyoendana na karne ya sayansi na keknolojia, upungufu wa vitabu vya kidato cha tano na sita, ukosefu wa uzio, upungufu wa wafanyakazi na hatuna gari dogo ambalo litatumika wakati wa dharula", alisema.
Akiongea na wanafunzi wa kike 1500 kutoka shule za sekondari 15 Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) alisema kuwa sababu za kihistoria zilikuwa zikiwanyima watoto wa kike fursa ya kupata elimu ikilinganishwa na watoto wa kiume.

FIESTA ONE LOVE YACHANJA MBUGA KWENYE MITANDAO!!

Libeneke la Fiesta One love ndani ya You Tube, chek link hiyo upate uhondo wa Fiesta kwa kubofya hapa http://www.youtube.com/watch?v=i0zUl2xvckg.

TUSIMAME NA KUUPIGA VITA UMASIKINI JAMANI!!

Katibu mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wasioona Tanzania Bw. Felician Mkude ambaye ana ulemavu wa macho, akiongea mbele ya waandishi wa habari kwenye ukumbi wa idara ya habari maelezo leo wakati akizungumzia kampeni ya "Simama na chukua hatua dhidi ya umaskini" iliyofanyika kati ya tarehe 16-18 katika nchi nzima, katika kuiunga mkono serikali kuupiga vita umaskini na kufikia malengo ya milenia ifikapo mwaka 2015, wanaofuatia katika picha ni Mussa Billegeya Mratibu wa Kampeni na Ms. Martina KabisamaMwenyekiti wa kampeni hiyo.

ALLIANCE FRANCAISE, THE FRENCH EMBASSY AND VISA2DANCE PRESENT


HIPHOP NITE / MUSIC & DANCE / TANZANIA & FRANCE with:

ZAHRBAT DANCE COMPAGNIE
(Contemporary / hip hop dance from France)
THE BEST FRIENDS
(Winners of DSM street dance competition)
TMK WANAUME HALISI
PROFESSOR JAY
MRISHO MPOTO
FID-Q
Venue: Diamond Jubilee-Main Hall.
Date: Saturday 31 October 2009.
Time: 8pm - 12pm
Entrance fees: TSH 6000

TSH 2000 (students & under 26 years)

A brilliant mix of Tanzanian & French music and dance, hip hop style. For both hip hop fans and contemporary dance lovers.
The opening act will be a presentation by selected Tanzanian dancers as the result of a two days workshop conducted by Zahrbat French dancers and choreographers.
Zahrbat performance will start by a 30mn danced lecture on the history of hiphop dance. It will be followed by “El Firak” a 30mn dance duo about separation and dealing with the issue of the wall built between Israel and the West Bank and the families torn apart by the conflict. The night will continue with live performances of
TMK WANAUME HALISI, PROFESSOR JAY, MRISHO MPOTO, FID-Q and BEST FRIENDS dance show.

Wanafunzi 220 wapata mimba kwa muda wa miezi kumi mkoani Kigoma!!

Na Anna Nkinda - Maelezzo, Kigoma
29/10/2009 Jumla ya wanafunzi 220 wa shule za Msingi na Sekondari Mkoani Kigoma wamepata ujauzito kuanzia mwezi wa kwanza hadi wa kumi mwaka huu na hivyo kushindwa kuendelea na masomo yao.
Hayo yamesemwa jana na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kanali Mstaafu Joseph Simbakalia wakati akisoma taarifa ya maendeleo ya mkoa huo kwa Mke wa Rais Mama Salma Kikwete aliyepo mkoani humo kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.
Taarifa ya Mkuu wa Mkoa huyo ilifafanua kuwa wanafunzi wa shule za Sekondari waliopata ujauzito ni 163 na wa shule za msingi ni 57.
Kwa upande wa mwaka jana wanafunzi waliopata ujauzito ni 167 ambapo wanafunzi wa shule za sekondari ni 85 na shule za Msingi ni 82.
Ili kukabiliana na tatizo hilo mkoa huo unajenga hosteli ambazo zitawasaidia wanafunzi wa kike kukaa shuleni wakati wote wa masomo na hivyo kuepukana na mazingira ambayo yatawafanya wapate mimba kirahisi.
Kwa upande wake Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) alipata muda wa kuongea na wazazi pamoja na wanafunzi wa kike wa mkoa huo na kuwataka kutojiingiza katika mapenzi kabla ya wakati bali wasubiri hadi pale watakapomaliza masomo yao.
"Hao wanaume wanawadanganya tu, wanawachezea miili yenu na hawawapi kitu chochote zaidi ya ujauzito na ugonjwa wa UKIMWI. Elimu ni mkombozi wa maisha yenu hivyo basi shirikianeni katika masomo ili muweze kufaulu vizuri na kujiunga na vyuo vikuu", alisema Mama Kikwete.
Alisema, "Mkumbuke kuwa jukumu la ulezi wa mtoto ni la jamii nzima si la mzazi peke yake kwani kuharibika kwa mtoto wako ni kuharibika kwa taifa zima hivyo basi sote kama wazazi tunajukumu la kupunguza kasi ya upatikanaji wa mimba za utotoni kwa watoto wetu na kuhakikisha kuwa watoto wanakuwa katika maadili mema ya kitanzania".
Mkoa huo unajumla ya shule za msingi 621 kati ya mahitaji 668 hivyo kuna upungufu wa shule 46 na shule za sekondari 130.

WHO WILL BE THE ONE AND ONLY M-NET FACE OF AFRICA 2009…


It’s more than a name, more than a moment.

In Africa, for a decade, one search has led the way to find iconic, unforgettable African style.

That search is M-Net’s powerful Face of Africa and this month, the legendary competition returns to television screens once more to tell a story of hope and opportunity, as the journey from Africa’s busy streets to Africa’s glamourous catwalks continues.

From Saturday October 31 at 19.00 CAT (M-Net East), and running 17 weeks, Face of Africa will cross countries, uncover fresh new faces, and chart their rise to the top, from discovery to success, from potential to fame, from possibility to reality. Along the way, audiences will discover how Tanzania’s gorgeous Lillian Alphonce Mduda was discovered at this year’s audition in Dar es Salaam and how far she’s progressed in the competition.

Speaking as M-Net readies itself to screen a new expanded series, Africa Director Biola Alabi was clear on the project’s legacy, its aims and its outcomes.

“Over time, this initiative has shown that it is about so much more than just fashion and beauty. There is a bigger picture there to see, something more than shoes, and cameras and clothing. It’s about young women with so much courage that they will leave their homes to find new experiences, so much determination that they will venture into the unknown to discover themselves, so much passion that they will chase their dreams.”

She goes on to say, “There’s something so magical about this, so special to see, that M-Net wants to share it with audiences across Africa. Because these are Africa’s own and they are taking their chance to shine. We want to laugh with them, cry with them, celebrate with them and now our audiences can do this, every step of the way.”

With a winner prize of USD 50 000 plus a modeling contract with O Model Africa, the new season of Face of Africa began earlier this year with auditions in 14 countries - Angola, Botswana, Ethiopia, Ghana, Kenya, Malawi, Mozambique, Namibia, Nigeria, South Africa, Tanzania, Uganda, Zambia and Zimbabwe. Further entry was open online to entrants from across sub-Saharan Africa who wished to participate gaining entries from as far afield as Sudan and Cameroon. The next step was the casting sessions where a special team of model scouts evaluated entries and selected contestants to continue in the series.

Emotional, dramatic and entertaining, these castings were filmed and audiences will now be able to see behind-the-scenes of the search and live the experience.

At the end of the audition phase, 24 models from16 countries were selected to participate in Model BootCamp, in Mombasa in Kenya. This idyllic tropical paradise with its breathtaking shoreline served as backdrop for another selection round amidst modeling workshops, fashion photo-shoots and television filming.

With some of the selected contestants exiting the competition at this point, the Mombasa BootCamp was action-packed, exciting and a little tense, as contestants learnt, honed their skills and competed to remain in the competition under the watchful eye of BootCamp presenter and former Face of Africa 2005 Kaone Kario.

With stops scheduled in Johannesburg as well as a second Model BootCamp in Dar es Salaam at Swahili Fashion Week, plus the shooting of a music video with Nigerian superstar D’Banj, the Face of Africa adventure will be told every Saturday evening on M-Net East, in the lead-up to the Face of Africa 2009 Finale, to be held in Lagos on Saturday February 6, 2010.

For fans of the series, remember you can also log on to www.mnetafrica.com to watch exclusive footage, find out more about the contestants, access photographs and chat to other fans about this year’s search.

Meanwhile as the search for a new Face of Africa gets underway, last year’s winner Kate Menson is living her dream job. The 24-year-old has been starring in M-Net’s advertising campaign for the new season of Face of Africa and in addition, she recently completed a stay at the Big Brother house. Other credits include appearances at Mozambique Fashion Week, New Delhi Fashion Week, Cape Town Fashion Week and New York Fashion Week, plus she’s appeared on the pages of Elle, Glamour and Cosmopolitan.Now, as Kate continues her rise to the top of the fashion world, a new face is about to be transformed from aspiring model to fully fledged modeling sensation…to find out who, simply follow the search on M-Net.

KATIBU MKUU VIWANDA NA BIASHARA AZINDUA TAMASHA LA BIASHARA!!

Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Joyce Mapunjo akisoma risala mbele ya waalikwa mbalimbali waliohudhuria katika uzinduzi wa Tamasha la Biashara la International Shopping Festival ambalo limeanza leo kwenye Viwanja vya Mwalimu J.K.Nyerere barabara ya Kirwa na litaendelea mpaka Novemba 10, tamasha hilo linashirikisha nchi 11 kutoka mashariki ya kati, Asia na Afrika Mashariki, wanaofuatia katika picha kulia ni Edwin Novath Rutageruka Director of Export Promotion (BET) na Ali Nizam General Manager Nizam Exhibitions Co.
Katibu mkuu wa Wizara ya Biashara na viwanda Joyce Mapunjo akiwa katika picha ya Pamoja na kamati ya maandalizi ya Tamasha hilo linalojulikana kama International Shopping Festival.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Bi Joyce Mapunjo akikata utepe kama ishara ya kuzindua rasmi tamasha la biashara linalofanyika kwenye viwanja vya Mwalimu J.K.Nyerere barabara ya Kirwa.
Katibu mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Joyce Mapunjo akiwa ameongozana na Balozi wa Syria Ahmamed Mansoor wakati walipotembelea mabanda mbalimbali katika tamasha la biashara lililozinduliwa leo kwenye viwanja hivyo.
Kikundi cha ngoma kikitumbuiza wakati wa uzinduzi wa Tamasha la biashara lililoanza leo kwenye viwanja vya Mwalimu J.K.Nyerere barabara ya Kirwa

CHANGIA SIMBA NA YANGA KWA KUJISAJIRI NA M-PESA

Meneja Udhamini na wa Vodacom Tanzania Emilian Rwejuna akizunngmza na wanahabari katika makao makuu ya kampuni hiyo jengo la PPF Tower wakati walipozindua rasmi kampeni ya kuzichangia timu za Simba na Yanga kwa kujisajiri na M-Pesa na kuingia kwenye bahati nasibu itakayokufanya ushinde na kujipatia Tiketi za kuingilia mpirani kwa ajili ya pambano la timu hizo litakalofanyika kwenye uwanja wa Taifa katika mfurulizo wa michezo ya ligi kuu ya Vodacom utakaochezwa jumamosi oktoba 31 jijini Dar es salaam au kujishindia fulana za timu unayoipenda, kulia ni mkuu wa kitengo cha M- Pesa Bw. Flanklin Bagalla.

Big Brother Revolution: Images from Day 51 - TUESDAY OCTOBER 27!!

Day 51 on M-Net’s Big Brother Revolution sees the housemates relaxing as they come to terms with the fact that Biggie seems to have disappeared leaving the housemates with a note saying they’re on their own for now! Biggie also left behind a bright red telephone which connects the housemates to the Big Brother call centre but the operators are never available to take the call. How will the housemates cope without Biggie? Will Biggie be back? And will there be any new ‘housemates’ joining the game when Biggie returns? Tune in to Big Brother Revolution on DStv channel 198 or 199 and for more information, log on to www.mnetafrica.com/bigbrother.

Shikito kupamba shoo ya Ferre Dar!!


MWIMBAJI nyota chipukizi wa Kongo Makinu Kombo ‘Shikito’ anatarajiwakuongozana na mkali wa bolingo kutoka nchini humo, Ferre Gola Batangire.Akizungumza mjini Dar es Salaam jana, msaidizi Kitengo cha Uhusiano,Udhamini na Matukio wa New Habari, Aziza Seif, alisema Shikito ni miongonimwa wanamuziki 17 watakaokuja nchini kwa mwaliko wa New Habari(2006)Ltd.“Katika orodha ya wanamuziki 17 ambao Ferre ametutumia majina yake, yupopia Shikito lakini mtoto mwingine aitwaye Ilunga hatakuja kwenye msafarahuu,” alisema.Aziza Aliwataja wanamuziki wengine wanaokuja na Ferre kuwa ni pamoja naFreddy Makola Linakasi, Nikodeni Kanday Ngoy, Olenga Makiese, ClizoKalonda Lopeta, Sungu Mbobolo, De Gaule Matima Makitela, Guy NgolaMawesele, Awulu Wala Tshipanga Wale, Ngwanzu Bavuidibio Gaza, DebosSunguesabena wa Kayembe, Mabiala Mobele, Mchele Mkelele Kitongo naChristian Solo Kabongo Muyambi.Wengine ni Vicky Moleka Leta, Patricia Isako Apakati, Renate KungaMuwangu, Nancy Mbemba-Lohuma.Shikito ni kijana mdogo ambae amejichukulia umaarufu mkubwa sana ndani nanje ya Kongo kwa kuwa mwimbaji mahiri mwenye umri mdogo zaidi katika angaya muziki wa dansi afrika.

Kigoma waanzisha daftari la mkulima ili kupata takwimu sahihi katika Kilimo!!

Mama Salma kikwete.

Na Anna Nkinda - Maelezo, Kigoma
Serikali mkoani Kigoma imeanzisha Daftari la Mkulima litakalowezesha kupata takwimu sahihi na kupima mafanikio katika mapinduzi ya kijani ili kuratibu utekelezaji wa mapinduzi ya kilimo na kauli mbiu ya kilimo kwanza.
Hayo yamesemwa jana na Mkuu wa Mkoa huo Kanali Mstaafu Joseph Simbakalia wakati akisoma taarifa ya Maendelezo ya Mkoa kwa Mke wa Rais Mama Salma Kikwete aliyeko ziara ya kikazi ya siku mbili katika mkoa wa Kigoma. Kanali Mstaafu Simbakali alisema kuwa Halmashauri zote tatu za mkoa huo zimeshaanzisha daftari hilo ambalo limesaidia kupata "Database" ya wakulima ambayo inatoa taarifa zote muhimu za kilimo ikiwa ni pamoja na idadi na orodha ya wakulima, hekta zilizolimwa kwa kila zao, kiasi cha pembejeo kilichotumika na mavuno yanayotarajiwa kuvunwa. "Daftari la mkulima litakuwa likiboreshwa kila msimu na kimsingi takwimu zitakaopatikana katika msimu husika zitasaidia kupanga msimu unaofuata" , alisema.
Katika kuhakikisha kuwa mkoa huo unazalisha chakula cha kutosha Halmashauri zote tatu za mkoa huo zimejiwekea malengo ya kuzalisha mazao makuu manne ya chakula ambayo ni mahindi, maharage, mpunga na muhogo.
Aliendelea kusema kuwa malengo mengine ni kupanua maeneo yanayolimwa kutoka Hekta 411,810 msimu wa 2008/2009 hadi Hekta 434,950 msimu wa 2009/2010, kuongeza tija katika kilimo na kuimarisha kilimo cha umwagiliaji. Aidha uzalishaji wa mazao hayo makuu ya chakula unatarajiwa kuongezwa kutoka tani 737,270 msimu 2008/2009 hadi tani 910,316 msimu 2009/2010 sawa na ongezeko la asilimia 23.

Rais Kikwete azindua mradi wa umeme Kilolo na kutembelea shamba la Ngo'mbe la Philips!!

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akifunua kitambaa kuzindua rasmi mradi wa umeme katika wilaya mpya ya Kilolo.Mradi huo unatekelezwa na wakala wa nishati vijijini(Rural Energy Agency) na unakadiriwa kugharimu Sh.1,665,600,000/-.(picha na Freddy Maro).

Baadhi ya wakazi wa wilaya mpya ya Kilolo wakisalimiana na Rais Jakaya Mrisho Kikwete muda mfupi baada ya kuweka jiwe la msingi katika jengo la Halmashauri ya Wilaya hiyo na kuwahutubia.

Muasisi wa Shamba la Mifugo la Philips Bi.Elizabeth Philips(84)(Aliyekaa kwenye wheel chair) akisalimiana na Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakati alipotembelea shamba hilo kujionea ng’ombe wanaofugwa kisasa leo mchana

Mmiliki wa Shamba la mifugo la Philips Bwana Richard Philips akimuonesha Rais Jakaya Mrisho Kikwete baadhi ya ngo’mbe wa maziwa wanaofugwa kwa kutumia utaalamu wa kisayansi nje kidogo ya manispaa ya Iringa leo mchana.

RAIS KARUME AREJEA KUTOKA UFARANSA!!

Rais wa Zanzibar na mwenyekiti wa baraa la Mapinduzi Amani Abeid Karume na mkewe mama Shadya Karume wakiwa wameongozana mara baada ya kuteremka kwenye ndege ya shirika la ndege la British Airways wakitokea nchini Ufaransa aklikokwenda kuhudhuria mkutano wa Unesco ambao ulizungumzia kukuwa kwa elimu Duniani.


MATUKIO KATIKA PICHA BUNGENI LEO!!

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akifurahia katika mazungumzo ya Mbunge wa Kilwa Kaskzini,
Dk. Samson Mpanda, kwenye jengo la utawala la Bunge Mjini Dodoma leo, Kulia ni Mke wa Mbunge huyo , Martina Mpanda.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Spika wa Bunge Samuel Sitta akimwapisha Mwanansheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Warema , (kulia) Bungeni Mjini Dodoma leo asubuhi (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Wawakilishi wa Baraza la Watoto wakipitia Muswada wa Sheria ya Mtoto leo asubuhi mjini Dodoma!!

Waziri wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia na Watoto, Mhe. Margaret Sitta akizungumza na baadhi ya watoto wakati watoto hao kutoka mikoa mbalimbali walipokuwa wakipitisha muswaada wa sheria ya watoto leo asubuhi kabla ya muswaada huo kupelekwa mbele ya wabunge wa bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania linaloendelea mjini Dodoma.
wawakilishi wa Baraza la Watoto la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakipitia Muswada wa Sheria ya Watoto mjini Dodoma leo katika Ukumbi wa CCT,kabla ya kuwasilishwa Bungeni.
Watoto hao wanawakilisha watoto wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka katika Mikoa mbalimbali nchini. Picha na (Asteria Muhozya wa Wizara ya Wanawake Jinsia na Watoto)


MISS TOURISIM ILALA WALAMBA MILIONI 50 ZA CHICKEN HUNT!!

Mwandaaji wa Miss Tourism Ilala 2009 Amina Boka wa pili kutoka kulia akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Savannah Lodge katika Hoteli ya City Paradise Mchana huu wakatika kampuni ya Chicken Hunt ambayo ni kampuni mama ya Savannah Lodge na Kampala Unirvesity ilipotangaza udhamini wa shilingi Milioni 50 kwa shindano hilo linalotarajiwa kufanyika Novemba 6 kwenye ukumbi wa Dar West Tabata jijini Dar es salaam.

Katika shindano hilo burudani zitaporomoshwa na bendi mbili tofauti katika kuleta ladha tofauti ambazo ni Diamond Musica na Extara Bongo wakati burudani nyingine italetwa na mtaalam wa nyimbo za Asili Mfalme Costa Siboka, katika picha wengine kulia ni Hamees Suba mkuu wa uhusiano Miss Tourism Tanzania, wa tatu ni Lucas Paul meneja mkuu Chicken Hunt na mwisho ni Pascal Boniventure Meneja wa Savannah Lodge nyuma ni warembo watakaoshirikia katika shindano hilo la pili kwa mkoa wa Dar es salaam mara baada ya lile la Temeke kumalizika.

PATA OFA KABAMBE ZA SASATEL HEBU ZICHEKI!!

Big Brother Revolution: Images from Day 49 - SUNDAY OCTOBER 25!!

Day 49 on M-Net’s Big Brother Revolution saw the departure of Comrades-in-Arms Kristal (Zimbabwe) and Quinn (South Africa) plus performances from the energetic hip hop artist XOD. In addition, series presenter IK announced that the Comrades-in-Arms part of the series is over and housemates will once more play as individuals! With the series now past the halfway mark, the remaining ten housemates are in the hunt for the USD 200 000 grand prize as the tension and drama grows.

Milan certain of Beckham deal!!

David Bekham.

AC Milan vice-president Adriano Galliani is "100% certain" David Beckham will return to the San Siro outfit in the winter transfer market.

The England midfielder has been strongly linked with a second loan spell at the Rossoneri to improve his chances of making Fabio Capello's FIFA World Cup™ squad.

Galliani told the Italian media: "Beckham's arrival is certain to happen, 100%. The agreement is done and all that is missing are the signatures."

The 34-year-old Beckham returned to the Los Angeles Galaxy in the summer after a successful six-month loan spell with Milan, where he helped the Rossoneri finish fourth in Serie A with two
story by www.fifa.com

Xavi glad to silence critics

Barcelona midfielder Xavi.
Barcelona midfielder Xavi hopes his side's 6-1 demolition of Real Zaragoza is more than enough proof that all is well at the European champions.
Barça found themselves in the spotlight heading into their home clash with Zaragoza following a disappointing couple of results in the last week. They lost their 100 per cent start to the La Liga season and a chance to break a club record when they were held goalless by Valencia last weekend, and then in midweek they crashed to a shock 2-1 home defeat to Rubin Kazan in the UEFA Champions League.
That was Barça's first defeat in Europe since last December and first loss in any competitive match since May, and led to Pep Guardiola's side coming under fire in the Spanish media. However, the Barça players last week dismissed suggestions of a possible crisis and let their football do the talking last night by thrashing Zaragoza to go three points clear at the top of La Liga.

The victory helped show that we are doing things well, has helped build confidence, and has made us league leaders.
Barcelona midfielder Xavi
"We've shown that we are fine physically and that we aren't lacking goals," said Xavi following the victory. "I already said that the game the other day (against Rubin) was just one of those things. People tend to be guided by results, but we know that if we continue playing like that then we will almost always win.
"We weren't very good against Valencia, but we were fine against Rubin apart from in front of goal. We've been good here (against Zaragoza), we've had chances and we were winning 2-0 very quickly. The victory helped show that we are doing things well, has helped build confidence, and has made us league leaders."
Midfielder Seydou Keita led Barca's goal blitz with a hat-trick, while big-money summer signing Zlatan Ibrahimovic continued his good start to life at Barcelona with a brace, and Lionel Messi added the other. Ibrahimovic has now struck seven times in La Liga, leaving him level with Valencia's David Villa at the top of the Primera Division scoring charts and one above team-mate Messi.
"I'm very happy, because I started the season a little flat, but every day I'm getting better. However, without my team-mates I wouldn't be able to play like that," Ibrahimovic said. story by www.fifa.com

Big Brother Revolution: Images from Day 49!!

Day 49 on M-Net’s Big Brother Revolution saw the departure of Comrades-in-Arms Kristal (Zimbabwe) and Quinn (South Africa) plus performances from the energetic hip hop artist XOD. In addition, series presenter IK announced that the Comrades-in-Arms part of the series is over and housemates will once more play as individuals! With the series now past the halfway mark, the remaining ten housemates are in the hunt for the USD 200 000 grand prize as the tension and drama grows.

X Plastaz represent Africa at BET Hip Hop Awards 2009


America's annual 'gathering of giants' pays tribute to Tanzanian hip hop

Rapper Gsan of the group X Plastaz from Arusha, Tanzania, is representing Africa in this year's edition of the BET Hip Hop Awards, broadcast on October 27 on BET (Black Entertainment Television) in the USA. Meanwhile, X Plastaz' dj/producer Threesixty is heard all around the world through his production for major hip hop artist Redman (Def Jam).
The annual BET Hip Hop Awards are watched by millions of hip hop fans across the United States. Especially the part of the show in which Gsan participates, titled the BET Hip Hop Awards cypher, is highly anticipated as it's a true gathering of giants in rap music. The cypher, in which the artists go back to the raw essence of hip hop, sees legendary dj/producer Premier team up with emcees such as Mos Def, Black Thought, Eminem and Joe Budden. The section in which BET pays tribute to the growing popularity of hip hop from East Africa by including Gsan has the Arusha-born rapper performing alongside veteran rapper KRS One along with newcomers Wale and Nipsey Hussle.

The inclusion of X Plastaz in this year's BET Hip Hop Awards came about when BET contacted X Plastaz, after seeing their music video 'Nini dhambi kwa mwenye dhiki' on the Youtube website. 'Nini dhambi' which has drawn over 400.000 views is one of the most popular East African music videos on the web. Gsan flew out to Brooklyn, New York where the cypher was pre-recorded in an empty factory building. His contribution was a rap in Swahili over an old school loop, cut up by dj Premier. While Swahili language hip hop was something new for the other artists, KRS One and Premier were full of love for the African input into this year's cypher.
After recording the cypher, Gsan attended the Awards ceremony which took place in Atlanta on October 10, and which will finally be broadcast next tuesday, October 27.

Says Gsan in an interview with Emcee Africa presenter Lee Kasumba: "Well, the Cypher segment was recorded in New York before the actual award ceremony. For me, it was just amazing to be there with people like Eminem, KRS One, DJ Premier playing the beats, and being able to showcase what I had. Many people were blown away with what I did and asked me why I rhymed in Swahili ‘cause they wanted to understand. I was just like ‘English is not my first language, I speak it, I love it but you will be able to mess me up if I rhyme in English’. There were emcees from all over the world in one setting, and I was happy to represent for Africa. I wasn’t starstruck, just glad to showcase what I did and could do with my American counterparts. I mean, think of it, we really have the same names, just one word changes, African American and African, do you understand what that means?"
Also this week, X Plastaz dj Threesixty (real name: Bamba Nazar) is being hailed as a breath of fresh air in hip hop as his production for Def Jam-artist Redman was distributed across the internet. The beat reminds of the energetic old school sound of the late 1970's and is a sureshot dancefloor filler. The song, titled 'Coc Back', is the first single off Redman's long awaited new album titled 'Reggie Noble 9.5' which will be released in December. The video for 'Coc Back' will be out this week.
Watch Gsan from X Plastaz in the BET Hip Hop Awards cypher on tuesday, October 27 at 8 pm (EDT) on BET. Outside of USA the cypher can be watched on Youtube from the day after the Awards show.
Official BET Hip Hop Awards website: http://www.bet.com/specials/hiphopawards09
X Plastaz website: http://www.xplastaz.com
Dj Threesixty website: http://www.bambanazar.com
Also see this clip in which dj Premier announced the participants of this year's BET Hip Hop Awards cypher (mispronouncing Gsan as 'Anson'):

SERENGETI YAKABIDHI VYANDARUA NA MASHUKA HOSPITALI YA BOMBO!!

Meneja uhusiano wa kampuni ya Serengeti Breweriers Teddy Mapunda akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Tanga mjini Bw. Ibrahim Msengi Mashuka na Vyandarua kwa ajili ya Hospitali ya wodi ya wazazi katika Hospitali ya Rufaa ya Bombo.

WATEJA WA VODACOM KUONGEA BURE KUPITIA CHEKA TIME!!

Mkuu wa kitengo cha udhamini wa Vodacom George Rwehumbiza, mkuu wa kitengo cha huduma na bidhaa Boniface Emmanuel, mkuu wa mawasiliano Vodacom Mwamvita Makamba na Ofisa bidhaa wa Vodacom Elihuruma Ngowi wakiwa wameshikilia vipeperushi katika uzinduzi wa huduma ya CHEKA TIME ambapo mteja wa Vodacom atakatwa shilingi 500 na kuweza kupiga simu dakika 60.
Ili mteja aweze kupata huduma hiyo atalazimika kujiunga kwa kupiga *147# na mteja anaweza kujisajili mara nyingi ili aweze kupata muda wa maengezi kadri atakavyo.
Huduma hii imezinduliwa jijini Dar es Salaam leo.(Picha na Rajabu Mhamila a.k.a Super D)

YANGA YAIBANJUA MORO UNITED UWANJA WA UHURU!!

Kikosi cha Timu ya Yanga.
Timu ya Yanga ya jijini Dar es salaam leo imejiweka katika mazingira mazuri kwenye msimamo wa ligi kuu ya Vodacom iliyondelea kwenye uwanja wa Uhuru wakati ilipomenyana na watoto wa mji kasoro bahari Moro United
Yanga ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata goli katika kipindi cha kwanza cha mchezo huo baada ya mchezaji wake Nurdin Bakari kuwazidi ujanja mabeki wa timu hiyo na kuubetua mpira juu mbele ya golikipa wa Moro United hivyo kuandika goli hilo lililowafanya kuongoza mpaka kipindi chote cha kwanza kilipomalizika.
Katika kipindi cha pili cha mchezo huo Moro United walionekana kuelewana vyema na kujipanga kwa mashambulizi ya mara kwa mara katika ngome ya yanga, hata hivyo washambuliaji wa timu hiyo hawakuwa makini kitu kilichowafanya washindwe hata kupata goli moja mbele ya vijana hao wa mtaa wa Jangwani kitu kilichoifanya Yanga kuibuka na ushindi wa goli 1-0 na kufikisha pointi 18
Mchezo wa leo uanawaweka yanga katika nafasi nzuri kwa morari wakati watakapopambana na watani wao wa jadi timu ya Simba ya jijini Mchezo wa ligi kuu ya Vodacom unaotarajiwa kupigwa kwenye uwanja mkuu wa Taifa oktoba 31 siku ya Jumamosi, Timu ya Simba mara baada ya kumaliza mchezo wao wa jana dhidi ya Azam Fc ilirejea tena mjini Zanzibar ambako imepiga kambi kwa ajili ya kujiandaa na mchezo huo

Rais Kikwete ampongeza mwenyekiti wa mtaa Kivukoni!!

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimpongeza Mwenyekiti wa Mtaa wa Kivukoni Bwana Jasper John Makame baada ya kupita bila kupingwa katika uchaguzi wa wa wenyeviti wa mitaa na wajumbe wa mitaa uliofanyika leo.Rais Kikwete na Mama Salma kikwete walijumuika na wakazi wengine wa kivukoni kusikiliza ushindi huo uliotangazwa katika shule ya Msingi Bunge jijini Dar es Salaam(picha na Freddy Maro)

Milioni 31 zapatikana katika Harambee ya kuchangia Ujenzi wa shule ya Agape!!

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete.

Na Anna Nkinda - Maelezo, aliyekuwa Morogoro
24/10/2009 Jumla ya shilingi milioni 31 zimepatikana katika Harambee ya kuchangia ujenzi wa shule ya Msingi ya Agape ya Kanisa la Waadiventista Wasabato iliyopo mkoani Morogoro.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete ndiye aliyekuwa mgeni rasmi kwenye Harambee hiyo iliyofanyika hivi karibuni katika viwanja vya Hoteli ya Morogoro.
Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) aliwataka wadau mbalimbali wa elimu waliohudhuria katika harambee hiyo kutoa kwa moyo kadri Mwenyezi Mungu alivyowajalia kwani Mungu aliyewapa ndiye wanayemtolea kwa njia ya ujenzi wa shule ambayo itawasaidia watoto kukua katika malezi yanampendeza Mungu.
"Napenda kuwapongeza wote waliotoa wazo la kufanya shughuli ya kuchangia ujenzi wa shule ya Agape kwani ujenzi wa shule hii ni wa muhimu sana kwakuwa utaongeza fursa ya watoto kupata elimu bora na malezi mazuri", alisema Mama Kikwete.
Akisoma taarifa ya shule hiyo Levi Yango ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya shule alisema kuwa ujenzi wa shule hiyo ambayo ni ya mchepuo wa kiingereza ulianza tangu mwaka 2003 huko Kitungwa umbali wa kilomita 12 kutoka Morogoro mjini.
Kabla ya kuanza kwa ujenzi wa shule hiyo wanafunzi wa darasa la kwanza walianza mwaka 2002 katika eneo la kanisa ambako kulikuwa na majengo ya vyumba vinne vya madarasa, vyoo matundu saba na ofisi moja ya walimuAliendelea kusema kuwa kutokana na ushauri wa Mkaguzi Mkuu wa Elimu Manispaa ya Morogoro walilazimika kutafuta eneo lingine huko Kitungwa na kuanza ujenzi ambako kanisa limeshakamilisha ujenzi wa vyumba vitano vya madarasa na vingine vitatu vipo katika hatua ya ukamilishaji.
Yango alisema, "Kwasasa shule imekuwa ikitumia majengo yasiyo rasmi yaliyopo karibu na shule kwa baadhi ya shughuli zingine kama vile ofisi ya walimu, vyumba kwa ajili ya darasa la kwanaza na la pili majengo mbayo hayakidhi mahitaji kitaaluma".
"Hali hii imechelewesha usajili wa kudumu ili kupata usajili wa kudumu , Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (Idara ya Ukaguzi) imeshauri tukamilishe ujenzi wa vyumba vitatu vilivyobaki na jengo la utawala lenye ofisi za walimu".