Mwanasoka bora Afrika wa BBC

Wachezaji watano wametajwa kugombea tuzo ya mwanasoka bora wa Afrika anayetambuliwa na BBC mwaka 2009.
Waliotajwa ni: Didier Drogba (Chelsea na Ivory Coast), Michael Essien (Chelsea na Ghana), Samuel Eto'o (Inter Milan na Cameroon), Tresor Mputu Mabi (TP Mazembe na DR Congo) na Yaya Toure (Barcelona na Ivory Coast).
Ingia hapa uweze kupiga kura kwa njia ya wavuti
Namba ya kutuma ujumbe au SMS ni +447786 200 070 ( kwa wasikilizaji wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC, hii ni tofauti na namba ya kawaida).
Unaweza kumpigia kura mchezaji wa chaguo lako mpaka tarehe 4 Januari na mshindi atatangazwa siku nne baadaye, Januari 8 huko Angola wakati wa michuano ya kombe la mataifa ya Afrika.
Tuzo hiyo ya hadhi kubwa ndiyo pekee ya aina yake kutolewa kutokana na idadi ya kura zinazopigwa na mashabiki wa soka.
Mshindi wa mwaka jana alikuwa Mohamed Aboutrika wa Al Ahly na Misri, aliyeisadia nchi yake kutetea kikombe cha kombe la mataifa ya Afrika na kuiwezesha timu yake kuchukua kombe la ligi ya vilabu bingwa Afrika.
Waliowahi kushinda tuzo ya mwanasoka bora wa Afrika2008 - Mohamed Aboutrika2007 - Emmanuel Adebayor2006 - Michael Essien2005 - Mohamed Barakat2004 - Jay-Jay Okocha2003 - Jay-Jay Okocha2002 - El Hadji Diouf2001 - Sammy Kuffour2000 - Patrick Mboma

Drogba: Catch us if you can

Didier Drogba.

Didier Drogba has said that Chelsea now have the mental edge over their rivals for the Premier League title.
The Blues restored their advantage over Manchester United to five points with an impressive 3-0 win at Arsenal, which leaves the Gunners some 11 points off the pace, albeit having played a match less. Drogba - whose brace at Emirates Stadium continued his fine form against Arsene Wenger's side - believes victories over all three of their traditional rivals this season, without conceding, shows Carlo Ancelotti's men have the making of champions.
"Arsenal played their game, but we were stronger than them," said the Ivorian international, who now has 10 goals in 11 games against the Gunners. "Every time we had the chance to score we did. We took our chances. Physically we defended well and were really strong, mentally as well.
"I don't know about Arsenal, but it is our strength to perform when it matters. Even against Manchester United, when the game was really difficult, we won. We know how to go through difficult periods when the game is hard. That is why when we get a chance we know how important it is to score."
Despite confidence in his team-mates, Drogba, 31, knows full well the battle for the championship is not yet won. However, looking down on the rest of the chasing pack rather than playing catch-up makes a big difference.
When you are top of the league, it is good - the others have to chase us. They have to produce and do more than us to win games.

MFUNGWA MWINGINE KUTUNUKIWA SHAHADA YA SHERIA KESHO!!

Kamishna wa Magereza Agustino Nanyaro.

Kamishna mkuu wa jeshi la Magereza nchini, Agustino Nanyaro amesemna kwamba kesho mfungwa mwingine Bw. Semayoga Ernest kwa mara ya pili kutoka gereza la ukonga atatunukiwa shahada ya sheria na Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (CKHT) , baada ya mfungwa wa kwanza Haruna Mgombela kutunukiwa shahada na chuo hicho mwaka 2007 .
Sherehe hizo zitafanyika kesho katika bustani za gereza la ukonga. Hizo zote ni juhudi za pamoja kati ya jeshi la magereza kupitia Wizara ya mambo ya ndani pamoja na wadau mbalimabli nchini katika kuwasaida wafungwa kubadili tabia wakiwa gerezani na kuhakikisha kuwa wanatoka wakiwa wema na wenye manufaa na walio tayari kujenga tiafa katika jamii zao.
Jeshi la Magereza kupitia Wizara ya Mambo ya ndani pamoja na chuo kikuu huria cha Tanzania vina mpango wa kujenga maktaba ndogo katika gereza la Ukonga pia kupita katika magerza yote nchini na kuwahamasisha wafungwa pamoja na askari magereza wajiunge na chuo hicho, yote hayo yakiwa ni kuwaelimisha na kuwatoa katika dimbwi la upungufu wa elimu, ikiwa ni kutekeleza kauli mbiu ya serikali inayosema 'maisha bora kwa kila mtanzania'.

Siri yafichuka Uchina

Nchini Uchina, watu takriban 60, wakiwemo waandishi wa habari kumi, wameshtakiwa kwa kuficha habari za ajali iliyotokea kwenye mgodi kwa madhumuni ya kuepuka aibu kabla ya michezo ya olimpiki ya mwaka jana.
Gazeti la China Daily linasema kwamba ajali hiyo, ambamo wachimba migodi thelathini na watatu wameuwawa, ilitokea wiki tatu kabla ya michezo ya olimpiki.
Gazeti hilo linasema maiti zilitolewa kutoka sehemu hiyo, ushahidi kuharibiwa na waandishi wa habari kupewa hongo ili kutotangaza tukio hilo.
Pia, liliongeza kwamba familia na jamaa za wachimba migodi zilishurutishwa kutokuzungumzia tukio hilo kwa vitisho na rushwa.

MAMA JAKAYA AKIWA TRNIDAD & TOBAGO

Mama Salma Kikwete akikaribishwa kwa kukumbatiwa na Mke wa Waziri wa Trinidad na Tobago, Seneta Hazel Manning wakati Mama Kikwete alipowasili kwenye Kituo cha Kidiplomasia mjini Port of Spain kuhudhuria Kongamano la Wajasiriamali lililoandaliwa nchini humo, Jumamosi, Novemba 28, 2009, na Seneta huyo kama sehemu ya shughuli za wake wa wakuu wa Serikali wanaohudhuria Mkutano wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuia ya Madola. (Picha na Juma Kengele, Ikulu)

WASHIRIKI WA KISURA WA TANZANIA WASHIRIKI KWENYE WARSHA!!


Washiriki wa Kisura wa Tanzania 2009 walishiriki katika warsha fupi mwisho wa wiki iliyopita ikiwa kama sehemu ya mafunzo yao wakiwa kambini.
Warsha hiyo iliyofanyika katika Hoteli ya Kiromo mjini Bagamoyo ilikuwa na lengo la kuwapatia visura hao elimu ya usimamizi wa fedha na ustaarabu yaani ‘etiquette.’
Akizungumzia warsha hiyo Meneja Mradi wa Kisura wa Tanzania 2009 Grace Kilembe alisema kuwa warsha hiyo ni sehemu ya mafunzo kwa wasichana hao wakiwa kambini.
“Moja ya malengo ya Kisura wa Tanzania ili aweze kujitambua, ni kuwapatia elimu ili waweze kutambua umuhimu wao katika jamii, uwezo walionao na mambo wanayoweza kutenda katika jamii na katika maisha yao kwa ujumla. Hivyo basi warsha hii ni muhimu sana kwao kwa sababu inawapa ujuzi wa usimamizi wa fedha na ustaarabu katika mazingira tofauti,” alielezea Grace.
Katika masuala ya ustaarabu wasichana hao walifunzwa jinsi kusalimiana, adabu za mezani, ustaarabu wa simu, kuwahi, matumizi na usafi binafsi. Somo hili lilitolewa na Sarah Majengo kutoka kampuni ya Innovative Creations.
Katika somo lake Sarah aliwaeleza wasichana umuhimu wa usafi kwa ujumla, jinsi ya kujitambua, na kuweza kujitokeza kisahihi kwatika mzingira tofauti.
“Kama mrembo lazima ujue jinsi ya kujimudu katika mazingira tofauti. Ni muhimu ufahamu ustaarabu wa mazingira unayokuwepo kama vile sehemu za sala, ofisi au starehe. Hii inajumuisha mavazi na jinsi ya kusalimia katika mazingira haya,” aliongeza Sarah.
Kuhusu usimamizi wa fedha Bi Chaba Mavura Meneja Mkuu wa kampuni ya Eazy Finance alitoa elimu ya usimamizi wa fedha.
“Ni Muhimu sana kujua jinsi ya kupanga matumizi yako ukiwa unatoa kipaumbele mahitaji ambayo ni ya muhimu kwa binadamu kama vile malazi, chakula na afya kabla ya kutumia pesa kwenye vitu vya anasa kama urembo na starehe. Mkiwa kwenye shindano kama hili mmoja wenu lazima ataibuka mshindi wa pesa na hivyo basi inapasa kujua jinsi ya kutumia pesa kwa uangalifu na vile vile kuwekeza ili kuongeza kipato chako,” alisema Chaba.
Washiriki wote walishiriki ipasavyo katika warsha hiyo fupi wakionekana kufurahia elimu waliyokuwa wakipata na kuuliza maswali mengi kuhusu masuala ya fedha na ustaarabu. Baada ya somo la usimamizi wa fedha visura hao walipewa zoezi dogo la kila mtu kuandika jinsi atakavyotumia shilingi 50,000 na mshindi wa shindano hilo kisura Ressoni Soto alijinyakulia kitita hicho cha elfu hamsini.
Visura wakiwa kambini hapo hupata mafunzo mbali mbali na hadi sasa wameshapata elimu ya ukimwi kupitia FHI, vile vile masuala ya kijamii na kilimo.
Shindano la kisura kwa mwaka huu linalodhaminiwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti litafikia tamati tarehe 18 Desemba ambapo mshindi atatangazwa katika hoteli ya Movenpick jijini Dar Es Salaam.
Wadhamini wengine wa shindano hilo ni Kiromo View Hotel, Family Health International (FHI), Air Tanzania, Mwananchi Communication, EM entertainment, Clouds fm, Hugo Doming na Mercy G Beauty Parlour.

Sebastian Ndege Best Student Overall -Post Graduate Diploma in Insurance & Risk Management (IFM)

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi mh. Laurence Masha, akifafanua jambo wakati wa Sherehe za Kumpongeza, Mhitimu wa Mafunzo ya Post Graduate Diploma in Insurance & Risk Menegement, Sebastin Ndege,zilizofanyika kwenye Hotel ya Pick Cock Mellenium jana.
Mkurugenzi wa Ndege Insurance, Sebastian Ndege, na Mkewe, wakiwakaribisha wageni kwenye Sherehe zao zilizofanyika Pick Cock Millenium

SERENGETI BREWERIERS YADHAMINI NYAMAGANA CUP KWA M.10!!

Bahati Singh akimkabidhi jezi Diwani Biku wa Nyamagana kwa ajili ya mashindano hayo ya Nyamagana Cup
Kampuni ya bia ya Serengeti leo imekabidhi hundi ya shilingi milioni 10 kwa waandaaji wa kombe la nyamagana la mpira wa miguu
Ndugu Bahati Singh Mkuu wa Masoko na Utekelezaji alikabidhi hundi ya Shilingi milioni kumi pamoja na vifaa vya michezo vikiweno jezi, vikombe na medali katika hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika nyumbani hotel jijini Mwanza, Makabidhiano hayo yalihudhuriwa na Meneja mauzo wa kanda ya ziwa Bwana Avinash Maggirwar na Meneja Masoko kanda ya ziwa Bwana Yohana Manoli
Akizungumza katika hafla hiyo Bwana Bahati Singh alisema’ Ni heshima tele tena SBL kudhamini mashindano haya katika jiji la Mwanza kwa kuwa tuna kiwanda chetu na malengo makubwa ya SBL ni kukuza kiwango cha mpira wa miguu Nchini na hasa katika mikoa ambayo tunaihudumia kijamii.
Mchango wetu wa leo ni kupitia zao la Premium Serengeti Lager tunaleta mahusiano mazuri na wanachi wa nyamagana na kuwaleta pamoja kwa njia ya mpira wa miguu na kuleta Amani, Urafiki, Upendo na Umoja kwa watu wa Mwanza
Pamoja tunawaweza kusema Asante kwa jamii ya watu wa Mwanza kwa kuunga mkono SBL na hii ni shukurani yetu tunasema asante tena watu wa Mwanza.

BIG BROTHER AFRICA REVOLUTION - Voting Note!

In order to ensure that all our voting audiences understand the way the vote is being counted, M-Net has clarified this in the paragraph below. M-Net understands and appreciates the audience’s right to be fully informed regarding the voting results each week and hopes that the below will assist in explaining the vote counting process clearly.
- Vote lines close at 06:00 CAT on Sundays.- Results from voting via text message, MXit, on the website and via WAP, are tabulated. - The housemate with the fewest votes in a specific country gets that country’s eviction vote. - The more country votes a housemate accumulates, the less popular that housemate is. - This is because they are the least popular housemate in the majority of countries.

WAREMBO MISS EAST AFRIRCA KUANZA KUWASILI WIKI HII!!

Nediat (21) ETHIOPIA
Warembo wanaoshiriki katika mashindano ya kimataifa ya urembo ya Miss East Africa 2009 wataanza kuwasili Nchini kuanzia wiki hii tayari kwa mashindano hayo yanayotarajiwa kufanyika tarehe 18 mwezi wa 12 katika ukumbi wa mlimani city jijini Dar es salaam.
Aidha, warembo watakaoiwakilisha Tanzania katika mashindano hayo wanatarajiwa kutangazwa kesho kutwa baada ya kamati maalumu iliyopewa jukumu la kuratibu zoezi hilo kukamilisha kazi yake.
Mashindano ya Miss East Africa mwaka huu yanatarajiwa kuwa na mvuto wa aina yake kutokana na Nchi zinazoshiriki mashindano hayo kuchagua warembo wenye viwango vya hali ya juu ili kuziwakilisha katika mashindano ya mwaka huu
Miss East Africa 2009 itashirikisha warembo kutoka katika Nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Ethiopia, Eritrea, Somalia, Djibouti, na Mauritius ambazo zote zimeshathibitisha ushiriki wao.
Mashindano hayo makubwa ya urembo kwa ukanda huu wa Africa yanaandaliwa na kumilikiwa na kampuni ya Rena Events Limited ya jijini Dar es salaam.
Miongoni mwa makampuni yanayodhamini mashindano hayo kwa mwaka huu ni pamoja na Kunduchi Beach Hotel & Resort, EATV, Kings & Queens Worldwide, CMC Automobiles Limited na AKO Catering Services Ltd.

Dalysha Nirena Doorga (21) MAURITIUS

Fatma Abdulahi (20) SOMALIA

Tabitha (20) KENYA

Queen Belle Monique (23) BURUNDI

Fatma Abdulahi (20) SOMALIA

Rebecca Getachew (23) ETHIOPIA

Asli Osman Mahamud (20) –SOMALIA

TAMASHA LA MICHEZO LA VODACOM FOUNDATION SHARE & CARE LILIFANA!

Mh Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akimvisha medali Salumu Athumani baada ya kituo chao cha Tacoda kuibuka washindi wa kwanza katika mchezo wa miguu katika tamasha la michezo la Vodacom Foundation la share & care lililofanyika jana kwenye kiwanja cha Shekhe Amri Abeid mjini arusha na kuudhuriwa na zaidi ya watoto yatima 550.
Salumu Haji na Wilson Kimaro ambao ni watoto yatima wakichuana vikali katika mbio za kilometa 100 kwa upande wa wanaume katika tamasha la michezo la Vodacom Foundation lililofanyika kwenye kiwanja cha Shekhe Amri Abeid mjini arusha na kuudhuriwa na zaidi ya watoto yatima 550.

Kurwa shamputa mmoja wa watoto waishio katika mazingira magumu akishiriki katika mchezo wa kuruka viunzi katika tamasha la michezo la Vodacom Foundation la share & care lililofanyika kwenye kiwanja cha Shekhe Amri Abeid mjini arusha na kuudhuriwa na zaidi ya watoto yatima 550.

Rajabu Hussen mmoja wa watoto waishio katika mazingira magumu akishiriki katika mchezo wa kuruka juu( Long jump) katika tamasha la michezo la Vodacom Foundation la share & care lililofanyika kwenye kiwanja cha Shekhe Amri Abeid mjini arusha na kuudhuriwa na zaidi ya watoto yatima 550.

Janeth Shirima mmoja wa watoto waishio katika mazingira magumu akiibuka kuwa mshindi katika mbio za kilometa 100 kwa upande wa wasichana katika tamasha la michezo la Vodacom Foundation la share & care lililofanyika kwenye kiwanja cha Shekhe Amri Abeid mjini arusha
Afisa habari wa Vodacom Tanzania Matina Nkurlu(kushoto)akifanya mahojiano na mmoja wa watoto waishio katika mazingira magumu Salma Mohamed(kulia) katika tamasha la la michezo la Vodacom Foundation la share & care lililofanyika kwenye kiwanja cha Shekhe Amri Abeid mjini arusha

Tiger Woods atoka hospitalini!

Tiger Woods.

Mcheza gofu namba moja duniani Tiger Woods ametoka hospitali baada ya matibabu ya ajali ya gari Florida Marekani siku ya Ijumaa.
Taarifa za awali zilieleza alijeruhiwa vibaya, lakini baadae mtandao wake ulifahamisha "alilazwa, akatibiwa na akaruhusiwa akiwa hajambo".
Gari lake inaarifiwa liligonga bomba la maji ya kuzimia moto barabarani na baadae likauparamia mti.
Woods, aliyeshinda mashindano 14 makubwa duniani, inaelezwa amepata majeraha usoni.
Mkewe Elin aliwambia polisi ilimbidi atumie fimbo ya kuchezea gufu kuvunja kioo cha nyuma cha gari baada ya kusikia kishindo cha ajali akiwa nyumbani. na

Hoeness in as Bayern president

Uli Hoeness

Uli Hoeness, club manager at Bayern Munich for 30 years, on Friday officially replaced Franz Beckenbauer as president of the board of the Bundesliga club.
"Thanks Uli for these 30 years of pure passion," club chairman Karl-Heinz Rummenigge said as Hoeness was elected to massive applause at the club's annual general meeting.
Hoeness, a former Bayern player in the 1970s, also won the 1972 European championship and 1974 FIFA World Cup™ with West Germany. He joined the club's coaching staff in 1979 after a recurring knee injury ended his playing career.
At the time Bayern Munich were heavily in debt with an annual turnover of 12 million Deutschmarks (€6 million ). The club has since flourished and under his guidance have won 16 Bundesliga titles and the Champions League in 2001.
In 2008-09 the club's annual turnover was estmated at €268.7 million with profits of €2.5 million, according to figures released on Friday. Former Bayern and German football legend Beckenbauer moves into the post of honorary president in a move which was announced a year ago. www.fifa.com

OPERESHANI KIPEPEO NI KIBOKO, IMENASA MAJANGILI 70!

Waziri wa Maliasili na Utalii Mh. Shamsa Mwanguna akiongea na waandishi wa habari katika makao makuu ya Wizara hiyo Mtaa wa Samora, ambapo amesema Jitihada za serikali katika kudhibiti ujangili wa wanyamapori nchini hususan wa Tembo kupitia operesheni kipepeo iliyoanza rasmi novemba 8, 2009 ndani na pembezoni mwa pori la akiba la Selous zimefanikiwa kwa kiasi kikubwa ambapo hadi kufikia novemba 25, 2009 jumla ya watuhumiwa 70 wamekamatwa kwa makosa mbalimbali.
Wamekamata mizoga 9 ya Tembo, 12 ya viboko ,16 ya Nyati, 2 ya kuro na mmoja wa mamba, pamoja na kuonekana kwa mizoga hiyo nyara zifuatazo zilikamatwa meno 8 na vipande 12 vya meno ya tembo vyenye uzito wa kilo 39, nyama ya Nyati na Swalapala, Ngozi moja ya Mbawala, na mkia mmoja wa nyumbu, pia kilo 20 za samaki wabichi.
Silaha zilizokamatwa ni Bunduki za kuwindia wanyama (RIFLE) 3 na ShotGun 15 , SMG 1, Magobole 2, risasi 114 kati ya risasi hizo 25 zimetengenezwa kienyeji, sumu aina ya Furudan itumikayo kuulia samaki, mamba hata viboko na kwa vile sumu hii huwekwa kwenye maji madhara yake yanampata pia binadamu anayetumia maji hayo.
Kwa maana hiyo basi Wizara itawashughulikia wahalifu ipasavyo vilevile itaendeleza doria za pamoja kati ya jeshi la polisi na idara ya wanyamapori, TANAPA,Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro(NCAA) na Taasisi nyingine za Kanda na Kimataifa katika kudhibiti Ujangili.
Operesheni imepewa jina la "Kipepeo" kutokana na kutumiwa kwa Helkopta na Ndege za kusafirisha askari katika vituo ndani ya pori ikiwa ni pamoja na kuhakikisha askari wanapatiwa mahitaji yote muhimu mahali popote walipo.

Dada Zainab Ameremeta zaidi!

Da Zainab akiwa na Matron wake wakifurahia jambo wakati wa sherehe yake ya kumuaga iliyofanyika kwenye Hoteli ya Lamada Ilala juzi Reception inatarajiwa kufanyika jumapili kwenye ukumbi wa Msasani Beach Club jijini Dar es Salaam, FULLSHANGWE inakutakia kila mafanikio katika maisha yenu mapya Hongereni Sana.
Hapa ni Kufurahi tu kwa kwenda mbele.
Da Rehema wa pili kutoka kulia akiwa na rafiki zake wakati wa Sendoff ya Bi Zainab iliyofanyika kwenye ukumbi wa Lamada Juzi.

ROTARY CLUB YACHANGISHA FEDHA ILI KUSAFIRISHA VIFAA VYA MSAADA!!

Mjomba Mrisho Mpoto wa pili kutoka kulia akiimba na wanamuziki wa bendi yake inayoitwa Mjomba Band kwenye ukumbi wa Palice Officers Mess jana jioni, wakati wa chakula cha jioni kwa ajili ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kulipia usafiri kutoka bara la Ulaya, Vifaa hivyo vya hospitali vimetolewa na wafadhili mbalimbali katika bara hilo kupitia taasisi ya Rotary Club na vitatolewa katika hospitali mbalimbali ili kusaidia kuondoa matatizo mbalimbali yanayoikabili Sekta ya Afya nchini.
Msanii Paul Nunda kutoka Kenya akiwashwangwesha mashabiki waliojitokeza kwenye unyesho la kuchangisha fedha kwa ajili ya kusafirisha vifaa vya mahospitalini vilivyopatikana kwa wafadhili mbalimbali kutoka bara la Ulaya kupitia Rotary Club, onysho hilo lilifanyika kwenye ukumbi wa police Officers Mess jijini jana.

NARGIS MOHAMED MARA BAADA YA KULA NONDOOZ MIAKA 3 IFM!!

Stella kushoto na Nargis wakiwa katika picha ya pamoja katika mahafali ya chuo cha usimamizi wa Fedha IFM baada ya kuhitimu masomo yao mahafali hayo yamefanyika leo kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam.
Nargis akiwa na rafiki yake Evelyne katika mahafali yaliyofanyika leo IFM.

Evelyne katikati akiwa na marafiki zake Siddy kushoto na Hafsa mara baada ya kuhitimu stashahada yake katika chuo cha usimamizi wa fedha IFM leo.

DI BANJI ANAIPENDA TANZANIA, ATAKAMUA KESHO TANGANYIKA PAKERS!!

Mwanamuziki Di Banji Kutoka Nigeria anayepiga muziki wa Dancall akizungumza na wandishi wa habari kwenye mkutano uliofanyika kwenye kiwanda cha Sigara TCC barabara ya Nyerere wakati alipozungumzia ziara yake nchini na onyesho analotarajiwa kulifanya kesho kwenye viwanja vya Tanganyika Pakers jijini Dar es salaam Novemba 28, katika mkutano huo mwanamuziki hyo aliongozana na wanamuziki wengine ambao atashirikiana nao katika onyesho hilo ambao ni Nameless na Nonini kutoka nchini Kenya walioko katika picha ni Isamba Kasaka (Brand Castopian) kulia na Jackie Lemboko Meneja wa Matamasha kushoto
Nameless akiongea mbele ya wanahabari wakati wa mkutano ulifanyika leo kwenye kiwanda cha sigara TCC barabara ya Nyerere.
Mwanamuziki Di Banji kutoka Nigeria wa pili kutoka kulia akiwa katika picha ya pamoja na wanamuziki wengine kutoka nchini Kenya wa kwanza kushoto ni Nameless, anayefuatia ni Nonini, katikati ni Dr. Sid kutoka Mo Hits Records ya Nigeria na mwisho kulia ni Ikechukwau Rapa aliyeongozana na Di Banji hii ilikuwa ni baada ya mkutano na waandishi wa habari uliofanyika kwenye kiwanda cha Sigara TCC barabara ya Nyerere leo.



Rajabu Kiravu azungumzia wajibu wa vyombo vya habari wakati wa uchaguzi mkuu.

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Bw. Rajab Kiravu akisisitiza jambo kuhusu nafasi na wajibu wa vyombo vya habari wakati wa uchaguzi mkuu kwa Maofisa habari na Mawasiliano wa Wizara, Taasisi, Idara zinazojitegemea na Wakala wa Serikali leo katika ukumbi wa kimataifa wa Arusha (AICC).
Picha na Aron Msigwa – MAELEZO

MAPACHA WANNE KATIKA UZINDUZI!!


MCHUNGAJI CHANCY LUHASA KUTOKA UBELGIJI KUHUBIRI INJILI ASSEMBLIES OF GOD MIKOCHENI B.

Mchugaji Getrude Rwakatale wa Assemblies Of God Mikocheni kushoto na Afisa mtumishi mwingine wa kanisa hilo wakimlaki Mchungaji Chancy Luhasa aliyekuja nchini akitokea Ubelgiji kwa ajili ya kuja kuhubiri neno la mungu katika kanida hilo, Mchungaji Luhasa alilakiwa kwenye uwanja wa ndege wa mwalimu J.K.Nyerere akiwa mwenye furaha, bila shaka ilikuwa ni bashasha ya kumshukuru mungu kwa kufika salama na kukutana na wenyeji wake.

MWANAMUZIKI DI BANJI WA NIGERIA ATUA JIJINI, KUFANYA MAMBO TANGANYIKA PAKERS JUMAMOSI!!

Mwanamuziki Di Banji katikati wa Nigeria amewasili leo mchana kwenye uwamja wa ndege wa mwalimu J.K.Nyerere kwa ndege ya shirika la ndege la Ethiopia Airline tayari kwa onyesho lake litakalofanyika kwenye viwanja vya Tanganyika Pakers jijini Dar es salaam akihirikiana na wanamuziki wengine mbalimbali wa nyumbani na Uganada na Kenya, onyesho hilo linatarajiwa kufanyika jumamosi wiki hii Novemba 28/2009.

Mwanamuziki Di Banji akichengua vimwana kutoka kampuni ya Sigara TTC vilivyokuja kumpokea uwanja wa ndege wa J.K.Nyerere leo mchana

SERENGETI BREWERIERS KUSAMBAZA VINYWAJI VIKALI KUTOKA EABL!!

Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki ambaye pia alikuwa Mgeni rasmi Mh. Deodorous Kamala akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa ubia kati ya kampuni ya Serengeti Breweriers Ltd na East African Breweriers Ltd/DIAGEO ya Kenya katika kusambaza vinyaji vikali vinavyotengenezwa na EABL/DIAGEO hapa nchini uzinduzi huo ulifanyika jana kwenye Hoteli ya Kilimanjaro Kempinski jana jioni, ambapo kampuni ya Serengeti sasa inazo haki za kusambaza vinyaji vikali kutoka kapuni hiyo ya kenya hapa nchini kama vile Smirnoff,Johnnie Walker range of whiskies, Richot Brand na Bond 7.
Novemba 20/ 2009 siku ya Ijumaa jijini Arusha nchi za Afrika Mashariki zilitia saini makubaliano ya soko la pamoja kwa nchi zote zinazounda jumuiya hiyo makubaliano yanayoitwa (East Africa Community Common Market Protocol) hivyo kwa makubaliano haya ya kampuni hizi mbili kutoka Kenya na Tanzania ni mwanzo mzuri wa utekelezaji wa makubaliano hayo ya soko la pamoja kwa jumuiya yetu, kushoto katika picha ni mwenyekiti wa Serengeti Breweriers Ltd jaji Marck Bomani.
Meneja uhusiano wa Kampuni ya bia ya Serengeti Breweriers Ltd Teddy Mapunda akizungumza mbele ya wageni waalikwa wakati wa uzinduzi huo.



Hapa Kocha mkuu wa timu ya Taifa Taifa Stars Marcio Maximo akiomsalimia Waziri wa Kazi na Maendeleo ya Vijana Prof. Juma Kapuya, waziri huyo ni shabiki mkubwa wa timu ya Simba na hapa ni kama vile Kocha huyo anamwambia Mh. Kapuya kuwa Hongera sana kwa mafanikio yenu wanasimba.
Kuanzia kushoto ni Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo Diodorous Kamala Waziri wa Afrika Mashariki ,Mkurugenzi wa EABL Patricia Ithau, Waziri wa anayeshughulikia Muungano Seif Maohamed Khatib na Mkurugenzi wa masoko na mauzo wa Serengeti Breweriers Shantanu Chitgopkar wakiwa wamekaa wakimsikiliza mwenyekiti wa Serengeti Breweriers Jaji Marck Bomani wakati alipokuwa akizungumza katika uzinduzi huo.
Chrristopher Mwita Gachuma Mkurugenzi wa Serengeti Breweriers Ltd Mwanza akizungumza jambo na Rais wa Shirikisho la mpira nchini TFF Rodger Tenga kulia huku Kocha mkuu wa timu ya taifa Taifa Stars Maecio Maximo katikati akipoozi kwa picha Serengeti inaidhamini timu ya Taifa na kuihudumua kwa vifaa vya michezo.
Waziri wa mambo ya ndani Lawrence Marsha akiteta jambo na Waziri wa Kazi na maendeleo ya Vijana Prof. Juma Kapuya kwenye uzinduzi wa Ubia kati ya Serengeti Breweriers Ltd na East African Breweriers/ Diaego juu ya usambazaji wa vinyaji vikali vinavyotengenezwa na kampuni ya EABL .
Hapa ni Sarakasi kamaunavyoona mdau.
Kikundi cha burudani cha Splendid kikitumbuiza wakati wa uzinduzi huo kwenye Hoteli ya Kilimanjaro Kempinski jana.