WAZIRI WA KAZI PROF.KAPUYA AZINDUA MWAKA WA VIJANA!!

Mgeni Rasmi Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana Prof. Athman Jma Kapuya akiongea na vijana wakati wa kongamano la vijana lililoandaliwa na Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa YUNA na kufanyika ukumbi wa APEADU kwenye ofisi za Umoja huo mtaa wa Mafinga Kinondoni Jijini Dar es salaam katika kuadhimisha siku ya vijana Duniani.
Katika kongamano hilo vijana wamejadili mambo mbalimbali yanayowahusu kama vile Elimu, Afya, Ajira, Michezo, Haki zao na mambo mengine mengi wanayokumbana nayo katika maisha ya kawaida kama vijana huku wakiazimia kuomba Serikali iwaruhusu kuunda Baraza la Vijana la Taifa litakalosimamia mambo yao yote ili kuwatetea na kuwasimamia katika mipango mbalimbali ya Kisera inayowahusu vijana.
Katika Hotuba yake Waziri Kapuya amewaasa vijana kuunda Baraza litakalokuwa ni la kitaifa zaidi kuliko kuwa Baraza la kiubabaishaji linaloweza kuleta athari kubwa kwa taifa Waziri pia alizindua mwaka wa Vijana unaoanza leo tarehe 12 Agosti 2010 mpaka Agosti 11 , 2011 na utakuwa ukiadhimisha kila mwaka Duniani kote.
Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana Prof. Athman Juma Kapuya akiingia kwenye ukumbi wa mkutano wa kati wa kongamano la vijana lilioandaliwa na Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa YUNA na kufanyika ukumbi wa APEADU kwenye ofisi za umoja huo Mtaa wa Mafinga Kinondoni jijini Dar es salaam nyuma ya Waziri ni Mwakilishi wa UNIDO Nchini Emmanuel Kalenzi.
Vijana kutoka shule na Asasi mbalimbali za vijana waliohudhurika katika kongamano la vijana lililofanyika leo kwenye ofisi za Umoja wa Mataifa katika kuadhimisha siku ya vijana Duniani.

Mikoko ya Vodacom kukuza uchumi kwa washindi!!


Baadhi ya washindi wa magari ya Hyundai i10 yanayotolewa na Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania kupitia promosheni yake ya ‘Shinda Mkoko’ wamesema zawadi hiyo itawasaidia kukuza uchumi wao kwani itarahisisha usafiri katika shughuli zao.


Akizungumza kwa njia ya mahojiano kutokea Dodoma baada ya kuibuka mmoja wa washindi wa promosheni hiyo, Tolino Pechaga ambaye ni fundi umeme wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) alisema anatumaini gari hilo litakamilisha ndoto yake ya kimaisha katika kujiletea maendeleo.


Akifafanua alisema, ingawa alikuwa akitumia magari ya wafanyakazi kutoka Maili mbili anakoishi hadi Udom, ujio wa Hyundai i10 utamaliza muda wa kukimbizana na basi hilo na kumpa nafasi ya kufanya kazi zake binafsi baada ya muda wa kazi kwa mwajiri wake.


“Unajua mimi ni mwajiriwa wa chuo, lakini nafanya pia kazi zangu binafsi. Usafiri ulikuwa kikwazo namba moja kufikia malengo yangu, lakini sasa kila kitu kitaenda sawa kwani tayari nitakuwa na usafiri wangu binafsi utakaorahisisha maendeleo yangu,” alisema Pechaga.


Kwa upande wake Benard Asenga wa Keko Magurumbasi jijini ambaye ni mfanyabiashara wa duka la bidhaa ndogondogo na vyakula alisema alikuwa akitumia muda mwingi na baiskeli kufuata bidhaa sokoni Kariakoo, lakini gari hilo litamuwezesha kuboresha utoaji huduma kwa wateja wake.



Aidha Asenga alifafanua kwamba mara baada ya kukabidhiwa Hundai i10 aliyojishindia atabadilisha mtindo wa biashara anaoufanya na anafikiria kuwa mjasiriamali wa kati (SME’s) na kumiliki duka la bidhaa za jumla na rejareja.


“Sasa sitatumia tena baiskeli kufuata bidhaa mjini, nafikiria kukuza biashara yangu kutoka hatua moja kwenda nyingine jambo litakaloniwezesha kukuza hali yangu kiuchumi,” alisema mfanyabiashara huyo.


Naye Simon Kihuru ambaye ni dereva wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songea alisema zawadi hiyo iliyotolewa na Vodacom Tanzania itampunguzia gharama za usafiri kwa ajili kuwapeleka na kuwarudisha watoto wake shule kwani wataweza kutumia gari hiyo kwa matumizi ya binafsi.



“Kama nilivyosoma kwenye magazeti mbalimbali kwamba gari hiyo haitumii gharama kubwa kuihudumia, kwa kuwa mimi ni dereva itaniwezesha kutunza fedha zangu baada ya kukwepa huduma za daladala ambazo sio salama sana hususani kwa watoto,” alisema Kihuru.



Akizungumza hivi karibuni kwenye hafla ya uzinduzi wa promosheni ya ‘Shinda Mkoko’ iliyopanga kuwazawadia wateja wake gari moja aina ya Hyundai i10 kila siku Mkurugenzi wa Masoko wa Vodacom Tanzania Ephraim Mafuru alisema shindano hilo litawahusisha wateja wote wa kampuni hiyo nchini na kwamba ndani ya siku 100 kila siku mtu atakuwa anajipatia gari moja.

EUROPEAN THRILLER – BAYERN VS REAL - LIVE ON SUPERSPORT!!


Two of the traditional giants of European football clash in a mouth-watering pre-season friendly as Bayern Munich host Real Madrid at the Allianz Arena on Friday, live on your World of Champions.



Bayern were double winners in Germany last season and got their new campaign off to the perfect start with a comfortable 2-0 success over Schalke in the DFB Supercup at the weekend. They are the team to beat in Germany this year, but coach Louis van Gaal will have some personal reasons to want a win in this one too.




He has previously had two spells in charge of Real’s archrivals Barcelona, and nothing would please him more than to sow the seeds of doubt in the Madrid team’s pre-season plans. Real coach Jose Mourinho has been working hard at putting his personal stamp on the Spanish side he joined in June from European champions Inter Milan.




Mourinho plotted the downfall of Bayern in the UEFA Champions League title-decider in May, and now has a quick return fixture against the side. Pre-season friendlies count for little in the greater scheme of things, but nobody wants to lose a high-profile fixture such as this one.




Pride is everything in European football and there will be no shortage of it out there at the Allianz Arena when these giants go toe-to-toe in Munich. DStv viewers can tune in for live coverage of the match on Friday August 13 (2155) on SS3, SS3A, SS3N and Maximo.

MTANZANIA APATA NAFASI KUSOMEA SHAHADA YA UZAMILI CHINA!!

Balozi Mdogo katika Ubalozi wa China nchini Tanzania FU JIJUN (kulia) jana akimkabidhi fomu ya nafasi ya masomo nchi za nje( skolaship ) Mfanyakazi kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo Sozy Ngate ( kushoto) katika Ubalozi wa China jijini Dar es Salaam. (katikati ) ni Mkurugenzi wa Utamaduni kutoka Wizara ya Habari ,Utamaduni na Michezo Prof. Hermas Mwansoko. Ngate atakuwa nchini China kwa muda wa mwaka mmoja kusoma Shahada ya Uzamili katika Utawala.
(Picha zote na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO) .
Balozi Mdogo wa China nchini Tanzania (charge d Affaires in the Chines Embassy in Tanzania) FU JIJUN (kulia) akiongea na Mkurugenzi wa Utamaduni kutoka Wizara ya Habari ,Utamaduni na Michezo Prof. Hermas Mwansoko jana katika Ubalozi wa China jijini Dar es Salaam wakati wa hafla fupi ya kumkabidhi fomu ya nafasi ya masomo ya Shahada ya Uzamili katika UTAWALA , Mfanyakazi wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo Makao Makuu Sozy Ngate(hayupo pichani).

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii yakabidhi vifaa Tiba Dodoma!!

Katibu Mkuu wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii bi. Blandina nyoni amekabidhi vifaa mbalimbali vya tiba katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, makabidhiano hayo yamefanyika juzi mkoani humo na hii ni moja ya mashine ya usingizi iliyokabidhiwa kwa hospitali hiyo
Katibu mkuu Bi Blandina Nyoni akikabidhi moja ya vifaa tiba vinavyotumika kwa ajili ya operesheni ya akina mama wajawazito kwa katibu Tawala wa mkoa wa Dodoma bi. Madenge

Moja ya kitanda kinachotumika kulazia mgonjwa anayehitaji uangalizi wa hali ya juu katika chumba cha watu mahututi(ICU)

BLOOD DIAMONDS - A TRAGEDY OF HISTORIC PROPORTION!!


African and international headlines have been dominated with the trial of former Liberian President, Charles Taylor and his alleged gift of blood diamonds to supermodel Naomi Campbell.



In the 1990s, the African countries of Sierra Leone, Liberia, Angola and the Democratic Republic of Congo disintegrated into civil war. Civilians were raped, murdered and attacked during the decade-long war. Collectively over 4 million civilians died.



What connected each conflict was the currency used to fund them – diamonds. HISTORY™ will provide a detailed look into the harsh reality behind the production of the world’s most valuable gems. Blood Diamonds depicts the brutality of a regime – supposedly backed by Charles Taylor – where millions of people lost their lives due to the conflicts over blood diamonds.




As citizens in four African warzones suffered, diamonds from those countries flowed freely into the world’s diamond market. Diamonds are the world’s most precious gems, but in West and Central Africa, their cost has been greater than anyone could have ever imagined.



Tune in to watch BLOOD DIAMONDS on the History Channel (DStv channel 254) on Saturday August 14 at 21.30.

MWENYEKITI WA (YUNA) HAPA NCHINI AWAPA CHANGAMOTO VIJANA!!

Mwenyekiti wa Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa hapa (YUNA) chini Benny Kikove akizungumza na wajumbe waliohudhurika kwenye kongamano la vijana linaloendelea kwenye ofisi za UN katika ukumbi wa APEADU Mtaa wa Mafinga Kinondoni jijini Dar es salaam, kongamano hilo linajadili mambo mbalimbali yanayowahusu vijana pamoja na changamoto wanazokumbana nazo katika ujana wao katikamkuadhimisha siku ya vijana duniani.
Wanafunzi wa shule mbalimbali wakiwa katika kongamano hilo wamesema wana matarajio mengi mara baada ya kongamano hilo kwani litawafanya kupeana uzoefu mbalimbali katika kukabili chanagamoto wanazokutana nazo katika maisha ya sasa.

Mmoja wa Wajumbe wa mkutano huo na Afisa wa UN hapa nchini Bi Hoyce Temu kushoto akiandika mambo mbalimbali yanaojadiliwa na vijana katika kongamano hilo.


Wajumbe mbalimbali wakimsikiliza mwenyekiti wa Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa hapa nchini YUNA Bw. Benny Kikove wakati alipokuwa akiongea na wajumbe wa konamano hilo asubuhi hii.

HRW: Zaidi ya watoto 700 watekwa na LRA


Karibu watu 700 wakiwemo watoto wametekwa kwa nguvu kutoka nyumbani kwao kwenye maeneo ya vijijini katika Jamhuri ya Afrika ya kati na kaskazini mwa Jamhuri ya demokrasi ya Congo.


Asili ya kundi la Lord's Resistance Army,linaloongozwa na Joseph kony,ni Kaskazini mwa Uganda.Leo hii wapiganaji wake wako hadi Congo kaskazini,Sudan Kusini na mashariki mwa Jamhuri ya Afrika ya Kati.


Shirika la kutetea haki za binaadamu la Human Rights Watch linasema kuna ushahidi kwamba kundi hilo limekuwa likiteka watu nyara kufwatia amri ya Joseph Kony.


Habari kwa hisani ya www.bbcswahili.com

TAIFA STARS NA HARAMBEE STARS NGUVU SAWA!!

Kiungo mshambuliaji wa Timu ya Harambee Stars ya Kenya, Macdonald Mariga (kushoto) akidhibitiwa na wachezaji wa Taifa Stars, Jerry Tegete (katikati) na Nurdin Bakari, wakati wa mchezo wa Kimataifa wa kirafiki uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam leo jioni. Timu hizo zimetoka sare ya bao 1-1.
Picha kwa hisani ya www.sufianimafoto.blog

Precision Air yaleta ndege mpya!!


Na Mwandishi Wetu


SHIRIKA la Ndege la Precision linalotoa huduma bora Tanzania, limetangaza kuleta ndege yake mpya ya sita aina ya ATR42-500 itakayowasili Agosti 26 mwaka huu kutoka Toulouse, Ufaransa, ikiwa ni sehemu ya kutekeleza programu ya kutoa huduma za kisasa zaidi. Mkurugenzi Mkuu na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Precision Air, Alfonse Kioko, aliwaambia waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuwa, ndege hiyo mpya itakayopachikwa jina la Bukoba, itafuatiwa na nyingine ya saba itakayoingia Septemba 15 mwaka huu.



Mwaka 2006, Precision na ATR ya Ufaransa walisaini mkataba wa dola za Marekani milioni 129 ili kutoa ndege saba mpya. Ndege ya kwanza kati ya hizo iliwasili Machi 2008. Tangu wakati huo, Precision imepokea ndege tano aina ya ATR 72-500 na kufanya iwe na ndege tano mpya mpaka sasa. Pia ina ndege nyingine tatu za zamani. Kioko alisema baada ya ndege hiyo yenye namba 5H-PWF kuwasili, wataizindua Dar es Salaam Agosti 27.




Alisema ina vifaa vya kisasa vya burudani kwa ajili ya wasafiri kuangalia sinema na kusikiliza muziki wakiwa safarini. Ndege hiyo ina uwezo wa kubeba abiria 70. Mkurugenzi huyo pia alitangaza kwamba tangu kuanza mwaka mpya wa fedha, idadi ya abiria wapya imeongezeka kwa asilimia 12 kulinganisha na mwaka jana. Pia mizigo ya biashara imeongezeka licha ya kudorora kwa uchumi duniani.




Akizungumza katika mkutano huo, Meneja Masoko wa Precision, Emillian Rwejuna alisema kampuni hiyo inatarajia kupata ndege ya Boeing 737, kati ya Oktoba na Novemba mwaka huu. Rwejuna alisema kupatikana kwa ndege hiyo kutapanua wigo wa huduma za safari.




Ndege hiyo ya tatu aina ya Boeing 737 itaboresha safari za Johannesburg, Afrika Kusini, na pia katika miji ya Kinshasa na Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Precision Air hivi sasa inafanya safari katika miji ya Dar es Salaam, Mwanza, Tabora, Musoma, Shinyanga, Kigoma, Kilimanjaro, Zanzibar, Mtwara na Arusha. Pia ina safari za Nairobi na Mombasa, Kenya na Entebbe, Uganda.

WAGOMBEA UBUNGE WA CUF (W) ILALA WAJITAMBULISHA!!

Mgombea Ubunge kupitia Chama Cha Wannanchi CUF Hussein Siyoverwa akizungumza mbele ya wanahabari leo kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo wakati wagombvea hao kutoka Majimbo ya Ilala, Segerea na Ukonga walipojitambulisha mbele ya wanahabari, wanaofuatia katika picha ni Kimangala Ayubu Mussa na Gulam Nasoro Mkurugenzi wa Uenezi, Mahusiano ya Umma CUF Wilaya ya Ilala.
Wagombea wa ubunge katika majimbo ya Ilala, Segerea na Ukonga kupitia Chama Cha Wananchi CUF wakionyesha fomu zao mbele ya waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo leo mara baada ya kukabidhiwa na Mkurugenzi wa Wialaya ya Ilala leo, kutoka kulia ni Heko Pori Ukonga,Husein Siyoverwa Ilala na Kimangala Ayubu Musa Segerea.

MAOFISA HABARI WAKUTANA LEO JIJINI DAR.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari(MAELEZO) Clement Mshana akiongea na Maofisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Wizara,Idara zinazojitegemea na wakala wa serikali leo jijini Dar es salaam.Pamoja na mambo mengine amewatoa wito kwa Maofisa hao kushiriki kikamilifu kutoa habari zinazohusu utendaji wa serikali kwa wananchi.
Maafisa habari wakiwa katika mkutano huo.
Baadhi ya Maofisa habari ,Elimu na Mawasiliano wa Wizara,Idara zinazojitegemea na wakala wa serikali wakifuatilia masuala mbalimbali leo jijini Dar es salaam wakati Mkurugenzi wa Idar ya Habari (MELEZO)Bw. Clement Mshana alipokutana nao. Picha na Aron Msigwa.

CLOUDS TV WAUNGANA NA MTV BASE

Usiku wa kuamkia leo, ndani ya ukumbi wa Much More uliopo katika jengo la Club Billicanas, umefanyika uzinduzi rasmi wa ushirikiano kati ya Clouds TV na televisheni ya Kimarekani MTV Base. katika ushirikiano huo, Clouds TV itakuwa ikirusha baadhi ya vipindi vya MTV Base kwa saa kadhaa kila siku jioni kuanzia saa 12. Pichani ni Mkurugenzi wa Clouds Entertainment Jose Kusaga (kulia) akitoa shukrani zake kwa MTV Base kupitia mwakilishi wao Mr. Paul

TWIGA STARS RECEIVED BY WASHINGTON GOVERNOR CHRISTINE GREGOIRE!

The Twiga Stars pose with Washington's governor, Christine Gregoire.
Photos and Story By Nisha Ligon http://www.twigastars.com/.
Today the Twiga Stars, Tanzania's national women's football team, visited the Washington State Capitol, where they were received by Governor Christine Gregoire. The Twiga Stars, who were brought to Washington State for a training tour by Rahma Al-Kharoosi, president of RBP Oil and Industrial Technologies, got the chance to learn about state legislative procedure, sing a Tanzanian song for their hosts, and to speak to the Governor herself. She wished them the best of luck and told the Tanzania ladies that she has a special interest in women's football as both of her daughters are footballers. Ms. Al-Kharoosi thanked the Governor for taking the time to speak to them, and added that it was inspiring for the girls to meet such an accomplished woman who has shown "yes we can."
A special tradition at the Washington Legislative Building is to make a wish while rubbing the nose of a George Washington bust. The Twiga players each took a rub and wished to make it to the Women's World Cup (to be held in Germany in summer 2011).
The Twiga Stars have been training in Washington since August 2, and are preparing for the African Women's Championship to be held in South Africa this October. The top two teams from the African Championship will proceed to the Women's World Cup in Germany. The Twiga Stars have shown they're ready for the competition by posting a number of impressive performances here in Washington, including a 4-0 victory over Dos FC last night. Asha "Mwalala" Rashid scored 2 goals, while Mwanahamis Omary and Fatuma "Kitunini" Mustapha each scored one. Ms. Al-Kharoosi said she's very happy with the teams performance and is confident that they are gaining the experience they need to succeed in the continental championship this

The players pose with George Washington Statue!
Twiga Stars matron Rahma Al-Kharoosi rubs George Washington's Statue and wishes for her girls to make it to the World Cup.

Ms. Al-Kharoosi, who has arranged and paid all expenses for this trip.
Photo op outside of the State Capitol

Ukweli Kuhusu Haruna Moshi ‘ Boban’ : Alikosa Namba Gavle IF


Na Maggid Mjengwa,Gavle, Sweden



HII ni sehemu tu ya makala inayohusu sakata la Haruna Moshi kukatisha mkataba na klabu ya Gavle IF. Kuna mengi yamesemwa na kuandikwa kuhusu Haruna Moshi kukatisha ghafla mkataba wake na klabu ya Gavle IF ya hapa Sweden. Hata hivyo, wapenzi wa soka wa Tanzania hawakuweza kupata ukweli hasa juu ya sakata la Haruna Moshi ‘ Boban’.



Nikiwa katika mji wa Gavle, mahali ambapo Haruna Moshi aliishi na kucheza kandanda ya kulipwa nimeweza kukusanya taarifa zenye kuonyesha nini kilitokea.




Kwa mujibu wa taarifa hizo, Haruna Moshi alikuwa na uwezo wa kuichezea klabu hiyo. Kilichojitokeza ni kwa Haruna Moshi kuwa majeruhi kwa muda mrefu huku nafasi ya kiungo wa kati anayoichezea ikigombaniwa na wachezaji zaidi ya watatu.Katika muda wote aliokuwa na Gefvle IF, Haruna Moshi amecheza mechi tano tu za Ligi Kuu ya Sweden.




Katika mechi hizo, ni mbili tu amecheza tangu mwanzo na nyingine tatu aliingia akitokea kwenye benchi la wachezaji wa akiba.Kwa mujibu wa maelezo ya Mkuu wa Idara ya Michezo ya klabu ya Gefle IF, Per Olson yeye anaamini, kuwa Haruna ana bahati mbaya.




Kuwa hata walipokwenda kwenye kambi ya mazoezi nje ya nchi, Haruna hakuwepo kutokana na familia yake kutarajia kupata mtoto. Hivyo, alikosa mechi tatu muhimu za kujipima nguvu na ambazo zingemweka Haruna Moshi kwenye nafasi nzuri ya kushindania namba.




Na mchezaji aliyesababisha Haruna Moshi abaki kwenye benchi ni Yussif Chibsah kutoka Ghana. Chibsah anachezea nafasi ya kiungo wa kati kama alivyo Haruna Moshi. Kurejea kwake katika klabu hiyo akitokea Ghana ndiko kulikofuta kabisa matumaini ya Haruna Moshi.




Ni nani huyu Yussif Chibsah? Na je, ilikuwa ni sahihi kwa Haruna Moshi kukatisha mkataba wake? Angeweza kubaki Sweden na kucheza katika klabu nyingine? Itaendelea… Habari hii ni kwa hisani ya


http://www.kwanzajamii.com/?p=2705 kwa habari zaidi bofya hapo.

M-Net's Big Brother ALL STARS: Images from day 21 (Sunday August 8, 2010)

It’s day 21 on M-Net’s Big Brother All Stars --- and Lerato is evicted from the Big Brother All Stars into the Barn, to join Hannington and Sammi. Last night’s show also featured Malawian rising star Young Kay. Stay tuned to M-Net’s BIG BROTHER ALL STARS with 24/7 coverage on DStv channel 198 plus daily edited shows on M-Net and AfricaMagic. For more information on the series, log on to www.mnetafrica.com/bigbrother.

BIG BROTHER ALL STARS MUNYA OR TATIANA – AFRICA MUST DECIDE!


Zimbabwe’s Munya and Angola’s Tatiana are up for eviction this week after Monday night’s (9 August) nominations on M-Net’s Big Brother All Stars. Munya finds himself up for eviction for the second week in a row after Sheila saved herself and put him up for eviction in her place.




Head of House Sheila found herself up for eviction after receiving the bulk of nominations from her housemates, based on the fact that she could save herself. · Code nominated Yacob, because as he says "I can't trust him and I can't place him yet". His second nomination went to Sheila. ·



Jennifer nominated Uti and Meryl because she feels they have formed an alliance, which concerns her.



· Kaone nominated Sheila and Meryl – the former because she could save herself. · Meryl nominated Kaone because he "gets on my last nerve” and also because she feels he is judgmental. She also nominated Tatiana because she considers her to be strong competition but pointed out that "it has nothing to do with Lerato, I just don't want her around for too long".





· Munya kept his nominations going along the same lines he has stuck to every week – “strictly business”. He nominated Uti and Yacob, explaining "I'm starting from the top of Africa and moving down”. ·



Paloma nominated Sheila because she could save herself and Uti because she felt his jokes had gone overboard and he is hurting people “and this is getting out of hand”.




· Mwisho nominated Tatiana because he thought everyone would be thinking along the same lines after both her Head of House decisions had seen the people she replaced herself, with evicted from the house. He also named Kaone because "the game has shifted” - he feels he needs to pick a side and take a gamble and Kaone is not on the side he has picked.

Rais Kikwete azindua Ujenzi wa Miundombinu ya Mfumo wa Mabasi yaendayo Haraka Dar es Salaam!!

Rais Jakaya Mrisho Kikwete ,Mwakilishi mkazi wa Benki ya Dunia John Mc Intyre(watatu kulia),Waziri wa Miundombinu Dr.Shukuru Kawambwa(kushoto) na Waziri wa TAMISEMI Mhe.Selina Kombani(kulia) wakifunua kitambaa kuashiria kuzindua rasmi ujenzi wa Miundombinu ya mfumo wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam wakati wa sherehe za uzinduzi zilkizofanyika Ferry kivukoni jijini Dar es Salaam leo mchana.
(Picha na Freddy Maro)
Mtendaji Mkuu wa Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka jjijini Dar es Salaam(Dar Rapid Transit Agency ) Bwana Cosmas Takule akieleza jinsi mradi huo utakavyofanya kazi pindi utakapo kamilika hivi karibuni jijini Dar es Salaam huku Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaamm williuma Lukuvi wakisikiliza kwa makini.

Mtendaji Mkuu wa Mradi wa mabasi yaendayo Haraka jijini Dar es Salaam Bwana Cosmas Takule akionyesha mchoro wa ramani ya utekelezaji wa mradi huo jiji Dar es salaam huku Rais Jakaya Mrisho Kikwete,Waziri wa Miundombinu Dr.Shukuru Kawambwa, Waziri wa TAMISEMI Bi.Selina Kombani na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya dunia Bwana John Mc Intyre wakisikilza kwa makini wakati wa sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa miundombinu ya mradi huo zilizofanyika Ferry Kivukoni, jijini Dar es Salaam leo mchana.



HASHEEM THABEET KUENDESHA CLINIC YA U17 BASKETBALL DAR ES SALAAM!

Mchezaji wa Mpira wa kikapu nchini Marekani NBA anayechezea timu ya Memphis Grizzlies akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa idara ya habari Maelezo leo jijini Dar es salaam wakati alipotangaza kuanza kwa programu ya Basketball Clinic itakayoanza tarehe 12 Agosti kwenye viwanja vya Don Bosco.
Watoto zaidi ya 400 wanatarajiwa kukutana kwenye clinic hiyo ambapo TBF kupitia kwa Makamu Mwenyekiti wake Phares Magesa amesema wanatakiwa kujiandikisha katika shule zote zenye vilabu vya Basketball nchini kote.
Lakini pia Hasheem Thabeet ameeleza kwamba katika nchi za Afrika ameshafanya Basketball Clinic kama hizo katika nchi za Nigeria, Senegal, Ivory Coast pamoja na Tanzania kwa sasa, kwa nchi za Asia amefanya programu kama hiyo na mchezaji mwenzake Yao Ming kwa nchi za HongKong, Quatar. Taipei, kulia katika picha ni Makamu Mwenyekiti wa TBF Phares Magesa.

SIKU NILIPOKUTANA NA MKURUGENZI WA MASHITAKA ELIEZER FELESH!!

Siku nilipokutana na Mkurugenzi wa Mashitaka wa Serikali nchini (DPP) Eliezer Felesh katika mkutano wa wanasheria wa Africa na Asia uliokuwa ukifanyika kwenye Hoteli ya Kilimanjaro Kempinski hivi karibuni hapa nchini na kujadili mambo mbalimbali ya kisheria,tuliongea na kubadilishana mawazo mbalimbali na Mh Felesh na nilifurahi kukutana na mtu mkarimu kama huyu.
Mwandishi wa habari mwandamizi wa Mwananchi Mkinga Mkinga akizungumza na Mwanasheria mkuu wa Serikali Jaji Fredrick Werema katika mkutano huo huku wanahabari wakiwaangalia na kusikiliza kwa makini.

RAIS KIKWETE ALIPOTEMBELEA NANENANE MKOANI DODOMA HIVI KARIBUNI!!

Mkurugenzi wa Maendeleo ya Mazao (KIUMO) Bwana Geoffrey Kirenga akimwelezea Rais Jakaya Kikwete namna ya utekelezaji wa Mpango wa Ruzuku ya Pembejeo za Kilimo kwa kutumia utaratibu wa vocha nchini wakati wa Maonyesho ya Nanenane Mkoani Dodoma hivi karibuni.
(Picha zote na Anna Itenda wa Maelezo)
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Bi Nyabaganga Taraba (kushoto) akimwelezea Rais Jakaya Mrisho Kikwete jinsi ya utaratibu wa kuendeleza miradi ya Umwagiliaji alipotembelea kwenye Maonyesho ya Nanenane Mkoani Dodoma .

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Bi Nyabaganga Taraba (kushoto) akimwelezea Rais Jakaya Mrisho Kikwete jinsi ya utaratibu wa kuendeleza miradi ya Umwagiliaji alipotembelea kwenye Maonyesho ya Nanenane Mkoani Dodoma .

Rais Jakaya Kikwete mpenzi wa watoto akiwa kwenye picha ya pamoja na mtoto Betha Chiwanga na mama yake Neema Chiwanga walipokutana na Rais njiani wakati wa maonyesho ya nanenane Mkoani Dodoma hivi karibuni.



Mkurugenzi Mkuu wa Jukwaa la Wakulima na Wafugaji (Farmers Centre Ltd )akimwonyesha madawa mbalimbali yanayotumika kwa ajili ya Wakulima na wafugaji kwenye maonyesho ya Nanenane yaliyofanyika Mkoani Dodoma hivi karibuni .

Msajili John Tendwa aliasa Baraza la Vyama vya Siasa!!


Benjamin Sawe Maelezo Dar es Salaam.



Msajili wa Vyama vya Siasa John Tendwa ameliasa Baraza la Vyama vya Siasa kuhakikisha uchaguzi wa mwaka huu unakuwa wa Kidemokrasia na wa amani.
Bwana Tendwa alisema hayo jana (leo) jijini Dar es Salaam wakati akifungua mkutano wa kwanza wa Baraza la vyama vya siasa ambapo alilitaka Baraza lililoundwa kisheria kuishauri serikali na jamii hasa katika kipindi cha uchaguzi.




Aidha alisema Baraza hilo si la kujitolea bali limeundwa kwa mujibu wa sheria na linawajibika kwa serikali na ni mshairi mkuu wa serikali katika shughuli za kisiasa. Alisema ni wajibu kwa baraza hilo kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa amani na utulivu na alilitaka baraza hilo kutoa tamko kulaani vitendo vinavyovunja amani na sheria ikiwa ni pamoja na kukemea vyama vya siasa vilivyoanza kampeni kabla ya tarehe ya kampeni.





Pia alivionya vyama vya siasa kuachana na siasa za kutumia lugha ya matusi wakati wa kampeni na ni wajibu wa Baraza hilo kutoa miongozo mbalimbali ambayo itafuatwa na vyama vya siasa.. Bwana Tendwa alilitaka Baraza hilo kuitisha mikutano ya mara kwa mara ambapo itatoa miongozo ambayo italiweka taifa katika mahala pazuri ili kufanikisha uchaguzi kwa amani na utulivu.





Alisema baadhi ya vyama vya siasa vimeanza kapeni kabla ya uchaguzi na vinajua kufanya hivyo ni kukiuka sheria za uchaguzi na moja ya athari za kuanza kampeni kabla ya uchaguzi ni kuwekeana pingamizi na kama likikubalika chama kitakuwa hakina mgombea hivyo amevitaka vyama kufuata taratibu na sheria za uchaguzi.





Akitoa shukrani kwa niaba ya Baraza hilo Mwenyekiti wa Baraza hilo Dr.Emanuel Makaidi amesema hawatamuogopa mwanasiasa au chama chochote cha siasa kitakachokiuka maadili kwani Baraza hilo limeundwa kwa mujibu wa kanuni na sheria. Dr. Makaidi alisema Baraza hilo litakuwa mshauri mzuri wa Serikali katika mambo ya kisiasa hasa katika kipindi cha uchaguzi.

Nokia yatoa toleo jipya lenye maudhui ya mfungo wa ramadhani



Benjamin Sawe Maelezo Dar es Salaam


Nokia imetangaza kuzindua mfumo mpya kwenye simu wenye maudhui ya kuridhisha kwa wakenya maalumu katika kipindi cha mwezi Mtukufu wa Ramadhan unaotarajia kuanza hivi karibuni. Toleo hilo ni jipya la maudhui ya mfungo wa Ramadhan 2010,ambapo simu zimeongezewa mambo muhimu ya mwezi mtukufu na yanapatikana kwenye Ovi, moja ya mfumo maarufu wa Nokia utakaoweza sasa kuupata kutumia simu ya nokia bure Mkuu wa kitengo cha mauzo Afrika Mashariki na kusini Bwana Kenneth Oyolla alisema, sasa watumiaji wa simu za Nokia ni wamoja na itakuwa rahisi kwao kupata maudhui na ujuzi ambao waislamu wengi wangependa kuupata ili uwaweke karibu zaidi na mwezi huu mtukufu.







Tumeshuhudia ongezeko kubwa la mahitaji kwa Wakenya na tunatarajia majibu kutoka kwa watumiaji watakapotumia mfumo huu mpya haswa kwa ndugu zetu waislam wanaoingia kwenye mwezi huu mtukufu.” Mfumo huo wa Ramadhan una wasifu pamoja na Quran tukufu, muda wa kuswali na hadithi za Mtume.








Quran tukufu imejumuisha maandiko ya Quran kutoka kwenye simulizi mbali ambapo watumiaji wataweza kuchagua katika mfumo wa MP3 na pia itatoa muongozo wa Qibla, inayotolewa kwa maeneo 1000 katika nchi 200, pia utaweza kuiingiza kwenye simu yako, kuitoa, kuisahihisha au kuongeza eneo lolote kwa kutumia GPS.







“Mfumo wa mwaka huu utawezesha simu za Nokia zikiwamo za kugusa na kuandika zote zinapatikana kwa lugha mbalimbali. Tunayofuraha kutoa mfumo huu katika kipindi hiki”, alisema Bwana Oyolla. “Hiki ni kipindi maalumu kwetu na tumejidhatiti kuhakikisha kwamba tunatoa suluhisho litakalokidhi mahitaji. Mfumo huu wa Ramadhani 2010 ni bure na unatoa ridhaa mbalimbali kutoka kwa watoaji wakimataifa na kitaifa na itapatikana kwa kupitia simu mbalimbali,” aliongeza Bwana Oyolla.






Bwana Oyolla alisema mfumo huo maalum kwa ajili ya Ramadhani 2010 umeunganishwa na simu za Nokia ambazo ni pamoja na Nokia N97 mini, Nokia E72, Nokia E52, Nokia X6, Nokia 5230,Nokia 5530,Nokia C5,Nokia 5235, Nokia 5800, Nokia E5, Nokia 6700 slide, Nokia 5233, Nokia X3, Nokia 6303i, Nokia 2710, na Nokia C3. Pia unapatikana kwa lugha ya Kiingereza, Kiarabu, Farsi, Kifaransa na Urdu.

Mzee wa "aladji aladji" kuwasha moto Bilicanas Club leo.



Baada ya kuzikonga nyoyo za wapenzi wa lile songi lililobamba sana hapa bongo la Alaji Alaji,ndani ya tamasha la Fiesta Jipanguse 2010 ndani ya viwanja vya Lidaz Club,kutoka kwa mwanamuziki wa Ivory Coast Jeff Bogolabang, leo usiku atalitikisa tena goma la alaji alaji ndani ya Bilicanas Club (Much More) kwenye uzinduzi wa Clouds Tv kujumuisha vipindi na muziki kutoka kituo cha MTV BASE.


Katika uzinduzi huo utakaokuwa na msisimko mkubwa kwa wadau wa mambo ya muziki na burudani ,utapambwa na wasanii wengine wa hapa nyumbani na pia kutoka kwa wale watani zetu wa jadi kutakuwepo na wale wakali wa kusugua sugua sahani CODERED DJ'S,ambao pia walifamya makamuzi ya kiaina ndani ya tamasha la Fiesta Jipanguse.


Aidha katika taarifa iliyotolewa na Clouds TV/MTV BASE,imeeleza kuwa kuanzia agasti 10 2010,watazamaji wa Clouds TV watapata nafasi ya kuburudishwa kwa masaa mawili ya vipindi vya muziki na mitindo ya maisha kutoka katika kituo cha televisheni cha Kimataifa,kinachorusha matangazo yake Afrika pekee cha MTV BASE.Burudani hiyo itarushwa hewani jumatatu hadi jumapili kati ya saa 12 jioni na saa 1 usiku,na vile vile kukiwa na mwendelezo wa burudani kati ya saa 4 na saa 5 usiku kwa siku za wiki.

BANTU NITE!!! FACE CLUB READING.

A BRAND NEW SEDUCTIVE & AFRO NITE LIKE NEVA BEFORE
BANTU NITE !!!!
SAT 28Th AUGUST 2010 BANK HOLIDAY W,KEND
COME & BANJUKA WITH FINEST DEEJAYS ON THE MIX
BONGODEEJAYS(TANZANIA) in collabo with TAMUSANA DJS(KENYA)
PLUS GUEST DEEJAYS
PLAYING THE BEST IN BONGO FLAVA -GENGE - ZOUK,LINGALA,NAIJA,KWAITO,R n B - HIP HOP,DANCE HALL & MANY MORE
venue -FACE CLUB
time 10PM-6AM
NO WORK ON MONDAY,SO DONT LET YOUR CURIOSITY TROUBLE YOUCOME AND JOIN US PARTY HARD TILL DAWN
For more info visit www.bongodeejays.blogspot.com

TAIFA STARS NA HARAMBEE STARS KUUMANA JUMATANO UWANJA WA HUHURU!!



Mchezo wa kirafiki wa kimataifa baina ya timu ya Taifa ya TANZANIA,TAIFA STARS na timu ya Taifa ya KENYA,HARAMBE STARS utachezwa kwenye dimba la UHURU na sio kwenye dimba la TAIFA kama ilivyokawaida ya michezo mingine ya TAIFA STARS.




Msemaji wa shirikisho la soka hapa nchini FLORIAN KAIJAGE amesema hakuna tatizo lolote lilofanya mchezo huo ukafanyike kwenye dimba la UHURU bali ni mpangilio tu wa TFF kama wasimamizi wakuu wa mchezo huo.



Mchezo huo utachezwa siku ya jumatano AUGUST 11 ambayo ni siku ya michezo ya kimataifa kama ilivyo kwenye karenda ya FIFA ambapo TAIFA STARS itaingia dimbani ikiwa na kocha mpya JAN PAULSEN toka DENMARK alieanza kuinoa timu hiyo toka wiki iliyopita.




Katika hatua nyingine wachezaji watatu wa TANZANIA wanaocheza soka la kulipwa nje ya nchi wanatarajiwa kuwasili jumanne wiki hii kwaajili ya mchezo huo.




Wachezaji hao ni NIZAR KHALFAN anacheza soka nchini CANADA,DANY MRWANDA anaecheza soka nchini VIETENAM na HENRY JOSEPHA anaecheza soka nchini NORWAY wakati mlinzi IDRISA RAJABU anaecheza soka nchini KENYA yeye alishawasili toka jumapili.
Habari kwa hisani ya www.janejohn5

VODACOM MISS TANZANIA KUPIGA KAMBI AGOSTI 16th…!!!


MKURUGENZI wa Kampuni ya Lino International Agency , ambaye pia ni Mratibu wa shindano la Vodacom Miss Tanzania Hashim Lundenga leo ametangaza majina ya warembo 31 watakaoingia kambini Agosti 16 mwaka huu.




Lundenga ilitaja majina ya washiriki na maeneo wanayowakilisha katika mabano ni hawa wafuatao Ester Dennis na Gloria (UDSM),Shadia Mohammed, Furaha David na Mary Kagali (Nyanda za Juu Kusini).




Wengine ni Bahati Chando, Salma Mwakalukwa na Consolata Lukosi (Kanda ya Kati),Flora Florence, Mary Adam na Angelina Ndege (Kanda ya Mashariki), Alice Lushiku, Irene Hezron na Amisuu Malick (Kanda ya Kinondoni), Genevive Emmanuel, Anna Daudi na Britney Urassa (Kanda ya Temeke), Glory Mwanga, Prisca Mkonyi na Jally Murei (Kanda ya Kaskazini).
Wengine ni Gloria Mosha na Christine Justine (Kanda ya Chuo Kikuu Huria), Flora Martin, RachelSindbad na PendoSam (Kanda ya Elimu ya Juu), Fatma Ibrahim, Buduri Ibrahim na Margareth Godson (Kanda ya Ziwa).




Taarifa hiyo ilisema kuwa warembo wote wanatakiwa kuripoti Agosti 16 saa tatu asubuhi katika ofisi za Kamati ya Miss Tanzania zilizopo mtaa wa Samora na Mkwepu baadaye watapelekwa katika hoteli ya Giraffe iliyopo Jangwani beach ambako ndipo itakuwa kambi yao.





Aidha washiriki wote wametakiwa kufika katika muda uliopangwa na si vinginevyo, mshiriki atakayechelewa kufika bila ya kutoa taarifa atakuwa amejitoa katika fainali hizo.
Wakiwa kambini washiriki hao watapata mafunzo mbalimbali kutoka kwa wakufunzi walioandaliwa pamoja na wataalamu wa nyanja tofautitofauti.

Fatma Ibrahim ndiye Vodacom Miss lake Zone 2010!!

Vodacom Miss lake Zone 2010 Fatma Ibrahim kutoka Mara akitabasamu baada ya kutawazwa kuwa malkia wa taji hilo, kushoto ni mshindi wa pili Buduli Ibrahim kutoka Shinyanga, Kulia ni Margreth Godson mshindi wa tatu kutoka Shinyanga. Shindano hilo lilifanyika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Natiro Annex Capripoint jijini Mwanza.