TAIFA STARS NA HARAMBEE STARS KUUMANA JUMATANO UWANJA WA HUHURU!!



Mchezo wa kirafiki wa kimataifa baina ya timu ya Taifa ya TANZANIA,TAIFA STARS na timu ya Taifa ya KENYA,HARAMBE STARS utachezwa kwenye dimba la UHURU na sio kwenye dimba la TAIFA kama ilivyokawaida ya michezo mingine ya TAIFA STARS.




Msemaji wa shirikisho la soka hapa nchini FLORIAN KAIJAGE amesema hakuna tatizo lolote lilofanya mchezo huo ukafanyike kwenye dimba la UHURU bali ni mpangilio tu wa TFF kama wasimamizi wakuu wa mchezo huo.



Mchezo huo utachezwa siku ya jumatano AUGUST 11 ambayo ni siku ya michezo ya kimataifa kama ilivyo kwenye karenda ya FIFA ambapo TAIFA STARS itaingia dimbani ikiwa na kocha mpya JAN PAULSEN toka DENMARK alieanza kuinoa timu hiyo toka wiki iliyopita.




Katika hatua nyingine wachezaji watatu wa TANZANIA wanaocheza soka la kulipwa nje ya nchi wanatarajiwa kuwasili jumanne wiki hii kwaajili ya mchezo huo.




Wachezaji hao ni NIZAR KHALFAN anacheza soka nchini CANADA,DANY MRWANDA anaecheza soka nchini VIETENAM na HENRY JOSEPHA anaecheza soka nchini NORWAY wakati mlinzi IDRISA RAJABU anaecheza soka nchini KENYA yeye alishawasili toka jumapili.
Habari kwa hisani ya www.janejohn5

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment