MCHAKATO WA KUMPATA KISURA WA TANZANIA KUANZA AGOSTI 16

Meneja Mradi wa shindano la Kisura wa Tanzania Nicole Kapesi akizungumza na wanahabari katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo leo kuelezea kuanza kwa mchakato wa kutafuta kisura huyo utakaoanzia Arusha Moshi, Karatu, Tanga na Dar es alaam kuanzia tarehe 16 mpaka 21Agosti na kufuatiwa na miji ya Musoma, Mwanza na Ngara tarehe 27 Agosti mpaka tarehe 2 Septemba kabla ya kupisha mfungo wa Ramadhan kushoto ni Emmy Melau Kisura wa Tanzania mwaka jana 2008.

Majambazi Yapora milioni 150 kwa kutumia mabomu ya kutupa!!

Hivi ndivyo hali ilivyokuwa kama unavyoona damu ikiwa imetaopakaa katika kaunta ya benki ya NMB Wilaya ya Temeke baada ya majambazi yenye mabomu kuvamia Benki hiyo na kurusha mabomu yaliyojeruhi watu 13 na mmoja kuuwawa ambapo hatimaye majambazi hayo yalipora kiasi cha shilingi Milioni 150 katika Benki hiyo, kwa mbinu hii ya Ujambazi kwakweli hali ni Tete wadau.

FM ACADEMIA WATOA VIDEO DVD YA LIVE!!

Mwanamuziki na kiongozi wa bendi ya FM Academi Nyoshi El Sadaat akiongea na wanahabari kwenye Mgahawa wa Hadee juu ya kukamilika kwa DVD yao ya Live yenye nyimbo mchanganyiko 5 inayoitwa (World Number 0 utamu wa Vanilla) Nyoshi amesema DVD hiyo ina viwango vya hali ya juu na itaanza kuuzwa madukani kuanzia sasa, ametoa mwito kwa mashabiki mbalimbali kuinunua DVD hiyo kwani hawatajutia kuinunua bali watasuuzika na roho zao kwa Zombo na Matembele iliyomo humo kushoto ni afisa uhusiano wa kampuni ya Zain Celina Njuju.

HAWA NDIYO WALIOVAA UHUSIKA KWENYE ONYESHO LA VIPAJI LA REDDS MISS ILALA JANA!!

Huyu aliyakata mauno kwa kwenda mbele katika muziki wa Taarab yaani ilikuwa si mchezo mpaka nilihisi labda ni Five Star Molden Taarab wanafanya mambo yao makubwa hii ilikuwa katika onyesho la vipaji la Redds Miss Ilala 2009 lililofanyika kwenye Hoteli ya Lamada Ilala ambapo warembo 17 walipanda jukwaani kuonyesha vipaji vyao katika nyanja mbalimbali ikiwa ni kuimba muziki, kucheza, kuigiza, ubunifu kuigiza na kadhalika
Redds Miss Ilala linatarajiwa kufanyika Agosti 7 kwenye viwanja vya ukumbi wa Karimjee jijini Dar es alaam Warembo wanaoshiriki kwenye shindano hilo ni Fatma Bongi, Everline Gamasa, Julieth Lugembe, Magreth Motau, Lilian Nyamizi Mihayo, Irene Karugaba, Neema Doreen Kasunga, Winnfrida Mmari, Husna Ahmed Doris Luis, Groly Mwandani, Pendo Lema, Anne Mkandawile, Khadija Mhecha, Sylivia Shally, Gladness Shao na Zena Mbasha pamoja na mwalimu wao Regina Joseph na matron Nelly Kamwelu aliyekuwa Miss Ilala namba mbili mwaka jana. .
Huyu aliigiza kama mbunifu wa mitindo kama unavyoona akifuma kitambaa mbele ya majaji.

Hapa ameshajifungua mtoto kama unavyomuona akimbebeleza.

Huyu kipaji chake kilikuwa kuigiza ambapo aliigiza kama mama mjamzito aliyekuwa shambani kisha akapatwa na uchungu na kujifungua mtoto hukohuko shambani.
Huyu aliimba nyimbo za kuabudu mpaka mishipa ikamtoka na aliigiza kwa hisia.

Majaji wakifuatilia kwa makini wakati wa onyesho hilo.

Wakuu wa Kamati ya Miss Tanzania wakiwa tayari katika onyesho la vipaji la Redds Miss Ilala ili kujua kinachoendelea kuanzia kushoto ni mwenyekiti wa kamati hiyo Prashant Patel, Mh. Yakub aliyekuwa Naibu meya wa Manispaa ya Ilala Mkurugenzi Miss Tanzania Hashim Lundenga,Mkuu wa Itifaki Albert Makoye na Mkuu wa Uhusiano Yason Mashaka.

Mbunifu wa mavazi Asia Idarous katikati akiwa katika pozi na warembo mablimbali waliojitokeza katika onyesho hilo lililofanyika kwenye Hoteli ya Lamada jana.

mashabiki mbalimbali waliojitokeza katika onyesho la vipaji la Redds Miss Ilala 2009 lililofanyika katika Hoteli ya Lamada Ilala.
keza ka

Becks’ boys vs Barca

David Bekhams LA Galaxy.

Fc Barcelona

David Beckham’s LA Galaxy will host European champions Barcelona in an intriguing friendly this weekend and DStv will screen all the action live on SuperSport 3 at 04:55 CAT on August 2.
As the football season draws closer, audiences will again be treated to the best in football action as the Spanish giants and 2008/09 La Liga champions take on L.A Galaxy.
“We’re thrilled to have an opportunity to play one of the best clubs in the world, FC Barcelona” said Galaxy President of Business Operations Tom Payne. “This summer is shaping up to be an exciting one for Galaxy fans with AC Milan and Barcelona coming to Los Angeles”.
The Home Depot Center is unavailable for the game as a result of the X Games therefore Galaxy returns to the Rose Bowl for the first time since 2002. The stadium is expecting up to 85000 spectators for the game this weekend.
FC Barcelona has multi-talented line-up that includes Lionel Messi, Rafa Marquez, Xavi, Carrlos Puyol, Andres Iniesta and Thierry Henry. While L.A Galaxy has David Beckham, Landon Donovan, Donovan Ricketts, Josh Sanders and Tristen Bowen.
Barca is in the midst of the best campaign in recent history and stands a chance of completing all three of their major tournaments; Spain’s La Liga, UEFA Champions League and the Copa del Rey.
Audiences can tune into SuperSport 3 at 04:55 CAT on Sunday and the match will be re-screened at 12:30 CAT later in the day. For other results and fixtures, viewers can press OK on the DStv remote control or go to http://www.supersport.com/.

Vodacom miss kanda ya ziwa wako fiti kwelikweli!!

Pichani ni warembo watakaochuana siku ya tarehe 7/8/2009 ijumaa, pale yatch club kwa mpambano mkali wa kumsaka, atakae mvua taji Nasreen Karim 2009.mchuano unaonekana kuwa mkali kwani washiriki woote wako bomba saaana!! JE KANDA YA ZIWA INAWEZA KUTOA TENA MISS TANZANIA? MATUMAINI YAPO TUNAWAOMBEA WAFANYE VUZURI HESHIMA IRUDI TENA KANDA YA ZIWA. kwa picha zaidi waingie florasalon.blogspot.com


Grizzlies sign second-round pick Young to deal!!

Hasheem Thabeet.

MEMPHIS, Tenn. (AP) -- The Memphis Grizzlies signed Sam Young to a multi-year contract in a deal announced Wednesday.
Young was the 36th pick overall in June. He led Memphis to a 5-0 record in the NBA summer league in las Vegas, averaging a team-high 13.6 points and 4.2 rebounds. The 6-foot-6 guard/forward led Pittsburgh in scoring and set a single-season record in being named All-Big East.
With the deal, the Grizzlies now have signed their three draft picks. They signed No. 2 pick overall Hasheem Thabeet and DeMarre Carroll earlier this month story by www.nba.com

TANGAZO LA WADAU WA DULLONET!!

Habari za kazi wanamtandao wenzangu. Kwanza tunapenda kuwaomba radhi kutokana na kutopatikana hewani kwa website yetu ya Dullonet hii ni kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wetu.
Naomba kwa muda muweze kutupata katika link ya
www.habarinamatangazo.net mpaka hapo tutakaporekebisha tatizo hili lililotupata.
Tunaomba radhi kwa mara nyingine lakini kwa kupitia link hiyo mambo yataendelea kama kawaida.
Dullonet Daima.

Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiwa na mkurugenzi wa Bahati Nasibu ya Taifa!!

Waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh. Mizengo Pinda akiwa na Mkurugenzi wa Bahati Nasibu ya Taifa Abbas Tarimba katika viwanja vya Bunge leo asubuhi picha kwa hisani ya http://issamichuzi.blogspot.com

MWANA HIPHOP MTANZANIA RENATUS MUGANDA KUTOKA MAREKANI KUKANDAMIZA JIJINI ARUSHA IDD PILI!!

Msanii Mtanzania wa muziki wa Hiphop anayeishi nchini Marekani Renatus Muganda aka GTK akiongea na wanahabari katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo leo asubuhi wakati alipozungumzia mkakati wake wa kukuza na kuendeleza muziki nchini ambapo ameandaa tamasha la muziki wa hiphop litakaloitwa ( Hiphop na Jamii)litakalofanyika jijini Arusha wakati wa sikukuu ya Idd Pili mwaka huu na kushirikisha baadhi ya wanamuziki wakali katika muziki huo wanaotikisa hapa nchini kama Chid Benz na wengine, Muganda amesema katika tamasha hilo anataka kuhamashisha mashule mbalimbali ili yashiriki katika tamasha hilo ambalo kiasi fulani cha pesa kitakachopatikana kitaenda kusaidia jamii
Mugada anayeishi katika jiji la Connecticut Marekani amesema amekuwa akifanya muziki wa Hiphop nchini Marekani toka mwaka 2000 na tayari ana nyimbo kama Juu kama Obama,mama,ZigZag Hussle na Thought they can be ambazo anatarajia atakamua nazo wakati wa onyesho hilo jijini Arusha.

Redds Miss Temeke 2009 Kusakwa Agosti 1 TCC Sigara!!

Mkurugenzi wa BMP Promotion Benny Kisaka akiongea mbele ya waandishi wa habari katika ukumbi wa idara ya Habari Maelezo juu ya maandalizi ya shindano la kumtafuta mlimbwende atakayewakilisha kanda ya Temeke katika shindano la Vodacom Miss Tanzania litakalofanyika baadae mwaka huu.
Vimwana watakaowania taji la Redds Miss Temeke 2009 wakiwa katika pozi mara baada ya mkutano na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa idara ya habari maelezo leo.


Kwanza kabisa ningewashukuru kwa kufika kwenu leo, na kuwa wadau wakubwa si tu katika mashindano ya urembo maeneo mengine lakini hasa mlivyokuwa karibu zaidi nasi waandaji wa Redd's Miss Temeke 2009.
Kubwa leo ni kuwatangazia warembo 12 watakaopanda jukwaani Jumamosi Agosti 1, 2009 katika ukumbi wa TCC Club kuwania taji hilo linaloshikilia na Angela Lubala ambaye kwa sasa yupo masomoni nchini Marekani. Warembo hao ni Stella Solomon, Sia Ndaskoy, Shani Anthony, Irene Christopher, Celine Chipeta, Fatuma Suzan, Sara Stepehen, Christine Thomas, Samira Kafinda, Grace Shayo, Nezia Anthony na Herieth Kibambe. Hawa wanatoka katika vitongoji vya Chang'ombe, Temeke South, Kurasini na Kigamboni.
Redds Miss Temeke imedhaminiwa na Redds Premmiun Cold, Vodacom Tanzania, Aurora Security, Gazeti la Jambo Leo, Sofia Recordings, 88.4 Clouds FM(redio ya watu) nawapongeza sana kwa kuhamia katika jengo lao hii ikiwa ni moja ya hatua kubwa ya kimaendeleo nasi wanaburudani hatuna budi kuyatazama kwa mema mafanikio haya, Mwasu Fashions, 100,5 Times FM(mguso wa jamii), Screen Masters, Valley Springs, Renzo Salon, Mariedo Boutique, Fredito Entertainment, i-View Photographer na mwanamitindo Ally Rhemtullah.
Kiingilio VIP 50,000 pamoja na chakula cha jioni na sh.10,000 kawaida. Hatutakuwa na mgeni rasmi bali tutakuwa na wageni maalum wenye nyadhifa mbalimbali nchini. Burudani; Mwanamuziki Lawrance Malima 'Marlaw' mzee wa 'Jam', shoo ya safu nzima ya Twanga Pepeta na kundi mahiri la The Chocolate. *Marlow*
Redd's Miss Temeke 2009, kwanza kabisa atapata Crwon, pia ataandaliwa kila kitu na mwanamitindo Happiness Magesse ambaye kwa sasa katika kazi zake za mitindo hujutumia jina la Millen. Happiness ambaye alikuwa Miss Temeke mwaka 2001 na pia kutwaa taji la Miss Tanzania mwaka huo na kuiwakilisha nchi.
Pia mshindi huyo atazawadiwa kitita cha Sh milioni 1 na laki tano(1.5 milioni). Mwaka jana alipewa Sh. 1.2 Mshindi wetu wa pili atazawadiwa Milioni 1 wakati mshindi wa tatu atapewa kitita cha Sh laki nane(Laki 8). Hii ni zawadi iliyo juu kupita mashindano ya vitongoji kwa mshindi wa tatu. Mshindi wa nne na watano kila mmoja atajinyakulia shilingi laki tatu(laki 3) ambapo kifuta jasho kitakuwa Sh laki moja na nusu.(150,000)

1 LADIES’ DETECTIVE AGENCY PREMIERS ON M-NET!



July 2009
This month DStv viewers across Africa can tune in for the highly anticipated series THE NO. 1 LADIES’ DETECTIVE AGENCY on M-Net.
Airing from Monday August 3 (19:30 CAT) the popular series is based on Alexander McCall Smith’s best-selling novels of the same name! Shot on location in Botswana, the series features Grammy Award winner Jill Scott as the charming Precious Ramotswe.
Following the 2008 feature film, THE NO. 1 LADIES’ DETECTIVE AGENCY is a poignant and passionate series chronicling the adventures of Precious Ramotswe, the eminently sensible and wise proprietor of the only female-owned detective agency in Botswana.
The series kicks off when Precious Ramotswe (Jill Scott) was a little girl spending her days with her beloved father (Winston Ntshona) in the Botswana, learning to use her eyes, ears, memory and patience.
Years later, after he dies, Precious inherits his 180 cows – a windfall that draws the interest of her abusive ex-husband Note (Colin Salmon), a trumpet player, and conniving lawyer Lucky (Tumisho Masha).
Asserting her independence, Precious sells the cows at auction, using the money to drive her father’s truck to Gaborone, where she buys a house and opens THE NO. 1 LADIES’ DETECTIVE AGENCY, her dream business, in a former post office.
Encouraged by new acquaintances like JLB Matekoni (Lucian Msamati), an auto mechanic she met when her truck broke down, and BK (Desmond Dube), a hairdresser working at The Last Chance Salon next door to the agency, Precious sets about establishing herself as a detective, hiring the lovable Grace (Anika Noni Rose), a high-strung yet devoted secretary.
Aided by her highly efficient yet rather peculiar secretary, Precious investigates a variety of cases helping townspeople solve ‘mysteries’ in their lives, from missing children to philandering husbands to con-artist scams.
DStv viewers can tune in for THE NO. 1 LADIES’ DETECTIVE AGENCY from Monday August 3 (19:30 CAT) on M-Net.

VIKOSI VYA ZIMAMOTO VYAPAMBANA NA KUZIMA MOTO KATIKA KIWANDA CHA BIA!!

Vikosi vya Zimamoto kutoka Knight Support na Kikozi cha Jiji vikiwa kazini wakati askari wake walipopambana kwa nguvu zote kuhakikisha wanazima moto uliokuwa ukiwaka katika kiwanda cha bia cha TBL kama unavyoona katika picha hali ilivyokuwa kiwandani hapo leo alfajiri na kufanikiwa kuuzima moto huo kabla haujaleta madhara makubwa zaidi.
Moto ukiwa unawaka kwa kasi kubwa kiwandani hapo hali iliyokuwa ikitishia kuteketeza kiwanda hicho kabla ya moto huo kuzimwa na vikosi vya zimamoto.

FM ACADEMIA KUWALISHA "ZOMBO NA MATEMBELE" REDDS MISS KINONDONI IJUMAA!!

Mwandaaji wa shindano la Redds Miss Kinondoni Boy George akiongea na waandishi wa habari leo kwenye Mgahawa wa Hadees, wakati alipozungumzia maandalizi ya shindano hilo litakalofanyika ijumaa ya wiki hii tarehe 31 julai pale Mlimani City jijini Dar es alaam kushoto ni Kiongozi wa Bendi ya Fm Academia mwanamuziki Nyoshi El Sadaat na kulia mwisho ni Miss Vodacom Tanzania 2007 Richa Adhia, anayefuata ni Mkurugenzi wa Miss Kinondoni Rahma George Fm Academia watatoa burudani katika shindano hilo.
Warembo watakaoshiriki katika shindano la Redds Miss Kinondoni wakipozi katika picha mara baada ya kumalizika kwa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo kwenye mgahawa wa Hadees jijini Dar es alaam.


SIMBA YASAJIRI YOSSO WATATU KUTOKA MJINI MAGHARIBI ZANZIBAR!!

Wajumbe wa kamati ya usajili ya simba Godfrey Nyange (Kaburu) kushoto na Mulamu Ng'ambi kulia wakiwa pamoja na wachezaji waliosajiliwa kutoka timu ya Mjini Magharibi Zanzibar ,mabingwa wa Copa Cocacola na ambao pia ni wachezaji wa timu ya taifa ya Zanzaibar.
Wachezaji wa Timu ya Simba B. wakiwa katika picha ya pamoja kwenye mkahawa wa Hadees leo wakati walipokuwa walipokuwa wakisaini fomu za usajili na kula chakula cha mchana kabla ya kuingia kambini leo.


New Habari (2006) Limited wadhamini washiriki Miss Vodacom Tanzania 2009!!

Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano, Udhamini na Matukio wa Kampuni ya New Habari (2006) Limited, Petter Mwendapole akibadilishana mkataba wa udhamini wa shindano la Miss Tanzania na mkurugenzi wa Lino Agency waandaji wa michuano hiyo, Hashimu Lundenga wakati wa hafla iliyofanyika jana makao makuu wa New Habari, Sinza Dar es Salaam.

KAMPUNI ya New Habari (2006) Limited, imejitokeza kudhamini shindano la Vodacom Miss Tanzania mwaka 2009.Akizungumza leo kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika makao makuu ya kampuni hiyo, Sinza, Dar es Salaam, Mkuu wa kitengo cha Uhusiano, Udhamini na Matukio wa New Habari, Petter Mwendapole alisema udhamini wao utagharimu kiasi cha sh milioni 80. “Hizi ni fedha ambazi zitahusisha mambo mbalimbali ikiwemo matangazo na promosheni ya shindano lenyewe, hapa tunazungumzia pia mavazi kama Tops, fulana na kofia kwa washiriki na watu mbalimbali,” alisema.

Mwendapole alisema kampuni yao imeamua kudhamini shindano hilo katika kuunga mkono juhudi za kampuni ya Lino International Agency kusaidia kumuwezesha binti wa Tanzania kujitegemea. Miss Tanzania inadhaminiwa kupitia gazeti la Bingwa ambalo hutoka kila sikuMbali ya hilo amesema lengo la kampuni hiyo ni kuhakisha utalii wa ndani unakuwa na kupitia magazeti yao watasaidia kutangaza vivutio mbalimbali.
Katika kuhakikisha shindano hilo linawafikia watu wengi, Mwendapole amesema watakuwa na kurasa maalum kwa ajili ya Miss Tanzania na pia watakuwa na matoleo maalum ya shindano hilo.

Katika mkutano huo, Mkurugenzi wa Lino Agency ambao ni waandaaji wa Miss Tanzania, Hashim Lundenga na Meneja Huduma kwa wateja wa Vodacom, Elihuruma Ngowi waliipongeza New Habari kwa udhamini wao na kueleza kuwa wana uhakika shindano la mwaka huu litakuwa na nguvu zaidi.New Habari ni wachapishaji wa magazeti ya Bingwa, Mtanzania, Dimba, The African, Rai, Weekend African na Mtanzania Jumapili..

UNATAKA KUPATA HUDUMA ZA SASATEL NENDA KWENYE DUKA LAO LILILOKO MTAA WA JAMHURI!!

Hili ndilo duka la kampuni ya simu za mkononi ya Sasatel lililoko mtaa wa Jamhuri kwa mahitaji yako ya simu za mezani zimu za mkononi na kuunganishwa na mtandao (Internet) nemda waone katika maduka yao yalioyotapakaa hapa jijini liliwemo hili la mtaa Jamhuri.
Meneja wa duka la Sasatel lililoko mtaa wa Jamhuri Lusako Owen kushoto akiwapa vipeperushi wateja waliotembelea dukani hapo ili kupata huduma, vipeperushi hivyo vina maelezo muhimu juu ya matumizi ya simu zinazouzwa na kampuni hiyo na viwango vya malipo kwa wateja wa kampuni hiyo


wanawake walio wengi wanachangia kwa kiasi kikubwa kuharibika kwa tabia za watoto!!

Watoto wa mitaani wakiomba msaada kwa mpita njia, kumekuwa na tatizo kubwa la watoto wa mitaani ambapo moja ya mambo ambayo yamekuwa yakisababisha kuongezeka kwa watoto hao ni matatizo ya kifamilia yanayosababisha watoto kusambaratika na kwenda mitaani.
Na Anna Nkinda - Maelezo
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete amesema kuwa wanawake walio wengi wanachangia kwa kiasi kikubwa kuharibika kwa tabia za watoto wao hii ni kutokana na tabia ya kutokuwakemea pale wanapokosea na kujifanya kuwa wanakwenda na awakati.
Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) aliyasema hayo jana wakati akiongea na wanawake wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) wa mkoa wa Kagera katika ukumbi wa Lina’s Pub.
"Mnachotakiwa kukifanya ni kusimamia maadili ya watoto wenu kwani watoto wengi wanajifanya kwenda na wakati kwa kuvaa mavazi ambayo yanaacha wazi sehemu za miili yao huku wazazi wao wanafurahia huko si kwenda na wakati bali ni kupotea kimaadili", alisema
Mama Kikwete alisema, "Ni wajibu wetu kutumia fursa zilizopo kujikwamua kiuchumi na hivyo kutoa mchango wetu katika jamii na taifa kwa ujumla. Vikundi vya kiuchumi kama vile SACCOS na benki za jamii yaani VICOBA ni moja ya mikakati ambayo inatekelezwa kiutaifa ili kumkomboa kwanamke".
Akisoma taarifa ya umoja huo Kaimu katibu wa Mkoa Editha Mwinula alisema kuwa umoja huo umefanikiwa kuwahamasisha wanawake kuanzisha vyama vya Akiba na Kukopa (SACCOS) na vikundi vya uzalishaji mali ili kupunguza umaskini. Pia wanawahamasisha wanawake ili waweze kujiamini na kugombea nafasi za uongozi ili wapate kuingia katika nafasi za maamuzi ndani ya chama na serikali.
"Umoja wetu unakabiliwa na tatizo kubwa la usafiri kwani tunatumia usafiri wa baiskeli kwenye wilaya zetu lakini jiografia ya mkoa wetu ni ngumu, baiskeli haikidhi mahitaji ya watendaji ukizingatia ni kina mama. Hivyo tunashindwa kuwafikia walengwa kwa muda muafaka", alisema Mwinula.
Mama Kikwete amemaliza jana ziara ya kikazi ya siku tatu katika mkoa wa Kagera yenye lengo la kuchangia juhudi za kupunguza vifo vya kinamama vinavyotokana na uzazi kwa kutoa vifaa vya huduma ya afya ya uzazi, hususan katika wodi za wazazi. Kuhamasisha juhudi za maendeleo kwa wanawake kupitia vikundi vya SACCOS na benki za vijijini- VICOBA.
Kuhamasisha juhudi za kupunguza matukio ya mimba na utoro mashuleni, kuhamasisha vikundi vya SACCOS na benki za vijijini- VICOBA na kuhamasisha juhudi za kupunguza matukio ya mimba na utoro mashuleni.

VACANCY NOTICE NO. 5/2009


The United Nations Development Programme (UNDP) office in Tanzania invites applications from suitably qualified Tanzania nationals to fill the vacant post of Communications Analyst.
Post No: 00045554
Post Title: Communications Analyst
Type of Contract: Fixed Term Appointment
Level: ICS.9
SUMMARY OF KEY FUNCTIONS:
Ensures development and implementation of a UNDP CO communication strategy
Public information management and strengthening of external relations
Maximize publicity of UNDP/Delivering as One
Supervision of the UNDP website, intranet, CO web-based knowledge management system
Facilitation of knowledge building and knowledge sharing within UNDP and with partners
Effective management of the Communications Office and supervision of Communications staff
RECRUITMENT QUALIFICATIONS:
At least Master’s level in Communication, Journalism, Public Relations; or equivalent professional work experience in the communication area, combined with an advanced university degree in a related discipline;
At least two years of directly relevant experience at the national or international level in public relations, communications or advocacy;
Previous experience with a multilateral or international organization is helpful but not mandatory;
Extensive experience in the usage of computers and office software packages, good knowledge and experience in handling of web-based management systems;
Fluency in English and Kiswahili.
Mode of application:
The details Terms of Reference are attached herewith. The letter of application, a completed standard UNDP Personal History Form (Form P.11) available from http://www.tz.undp.org/, together with copies of academic certificates and transcripts and currently written CV should be sent to: The Human Resources Unit, UNDP Office, P.O. Box 9182 Dar es Salaam not later than 7 August 2009. The post title must be indicated on the envelope.
Applications should be sent either by post or dropped at UNDP Office.
Only Short-listed applicants will be contacted.

VIJANA WA TANZANIA WATEMBELEA KITUO CHA WAZEE CHINA!!

Mkuu wa msafara wa ujumbe wa vijana ulioko mjini Qingdao,China ambaye pia ni Mkurugenzi wa Shule za Sekondari kutoka Wizara ya Elimu ya Mfunzo na Ufundi,Leornard Musaroche akizungumza na Bi. Li Aiguo Mkurugenzi mkuu wa kituo cha huduma za jamii cha Zhanshan.
Picha no Aron Msigwa – MAELEZO.

Vijana kutoka Tanzania walio ziarani China wakiwaangalia wazee wakicheza karata katika kituo cha huduma za jamii cha Zhanshan mjini Qingdao , China . Kituo hicho hutoa huduma mbalmbali kwa wazee wastaafu na wale wasiojiweza zikiwemo huduma nyingine za jamii .


Raia wa China wakiwa na vijana kutoka Tanzania (hawapo pichani) wakimuangalia mnyama maarufu nchini China anayejulikana kama tembo wa baharini (sea elephant) wakati akitoa burudani huku akipuliza zumari yenye milio tofauti na kushangiliwa na umati wa watu katika hifadhi ya Polar sea mjini Qingdao.



MELI YA MIZIGO YALIPUKA NA KUWAKA MOTO BANDARINI!!

Meli ambayo ahikufahamika mara moja kama ni ya mizigo ama ni ya uvuvi imelipuka na kuanza kuwaka moto wakati ikiwa imetia nanga katika bandari ya Dar es alaam leo asubuhi huku juhudi za kuzima moto huo zilizokuwa zikifanywa na boti ndogo za kuzima moto kutoka kikosi cha zimamoto cha Bandari zikiwa ngumu kutokana na uwezo mdogo wa Boti hizo kusukuma maji ya kuzima moto kuelekea eneo la tukio, kadiri boti hizo zilivyokuwa zikijaribu kuzima moto katika meli hiyo na moto ulikuwa ukizidi kuwaka kitu kilichoonyesha uwezo mdogo wa kikosi hicha kuhimili matukio ya moto kwa vyombo vya baharini.
Mmoja wa wafanyakazi wa Bandari ambaye alikuwepo katika eneo la tukio na ambaye hakutaka kutajwa jina lake amesema kuwa inasemekana meli hiyo ilinunuliwa na mfanyabiashara Bakhressa na ilikuwa ikifanyiwa matengenezo madogomadogo, ndipo ikatokea hitilafu katika mfumo wa umeme kitu kilichosababisha ilipuke moto, hata hivyo bado jeshi la polisi na Mamlaka ya Bandari hawajatoa taarifa yoyote mpaka sasa taarifa zaidi tutawaletea baadae.
Wakazi wa maeneo mbalimbali wakiangalia jinsi meli hiyo ilivyokuwa ikiungua kwenye bandari ya Dar es alaam asubuhi hii.

Moto uliendelea taratibu huku moshi akitanda eneo zima la posta ya zamani.

Hapa ikiendelea kuungua baada ya kulipuka moto

Twanga Pepeta 'Kusugua Kisigino' Kiwalani, wamo Mrisho Mpoto na Wabogojo!!

Wanamuziki wa Bendi ya African Stars wakiwa wammejipumzisha katika moja ya kazi zao za kurekodi video zao.
BENDI ya muziki wa dansi ya African Stars 'Twanga Pepeta International' inatarajia kuwapa mashabiki wake wa Kiwalani, Dar es Salaam, burudani ya staili yake mpya iliyoshika kasi ya 'Sugua Kisigino' kwenye ukumbi wa Gaza Strip. Mkurugenzi wa Kampuni ya First Entertainment iliyoandaa onyesho hilo,
Victorian Nachenga 'Victor Buguruni', alisema Dar es Salaam jana kuwa bendi hiyo itafanya onyesho hilo Alhamisi (Julai 30, mwaka huu) kuanzia saa 3 usiku kwa kiingilio cha sh. 5,000. Victorian alisema Twanga Pepeta itasugua kisigino kwa wakazi wa Kiwalani na vitongoji vyake, onyesho ambalo pia ni sehemu ya kuendelea kutambulisha albamu ya 10 ya bendi hiyo, Mwana Dar es Salaam iliyozinduliwa mwezi uliopita kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee.
Alisema onyesho hilo pia litapambwa na burudani kutoka kwa wasanii wengine wakiwamo Mrisho Mpoto 'Mjomba', Athuman Ford 'Wabogojo', Steve Nyerere na Sunche na Kapeto. Mkurugenzi huyo alisema katika onyesho hilo maalumu, bendi hiyo itatambulisha nyimbo zake saba mpya zikiwamo Sumu ya Mapenzi uliotungwa na Khalid Chuma 'Chokoraa', Mwisho wa ubaya ni aibu (Saulo John 'Ferguson'), Sintopenda tena (Saleh Kupaza), Nazi haivunji jiwe. Nyingine ni Shida Darasa na Mwana Dar es Salaam uliobeba jina la albamu, zilizotungwa na Charles Gabriel 'Chalz Baba' na mwingine uliotungwa na Rogart Hega 'Katapila'.
Albamu nyingine ambazo bendi hiyo imewahi kutoa na kutamba katika anga za muziki nchini ni Kisa cha Mpemba mwaka 1999, Jirani (2000), Fainali uzeeni (2001), Chuki binafsi (2002), Ukubwa jiwe (2003), Mtu pesa (2004), Safari 2005 (2005) na Password (2006).

MUSIC MAYDAY KUTOA MAFUNZO MBALIMBALI KATIKA SANAA BURE!!


Kupitia kituo chake cha
TALENT FACTORY
Inakuletea
MAFUNZO YA SANAA YA UIGIZAJI

Yatakayotolewa BURE kwa muda wa mwaka 1
(vigezo kuzingatiwa)

Walengwa ni vijana wenye kipaji cha uigizaji umri kati ya miaka16 – 27
USAILI UTAFANYIKA
TAREHE: 4 AGOSTI 2009
MUDA: 2:30 ASUBUHI HADI 10:00 JIONI

FOMU ZINAPATIKANA:
MUSIC MAYDAY TANZANIA iliyopo Sinza Afrikasana karibu na jengo la marie stoppes na

Kituoni TALENT FACTORY - Moroco nyuma ya Best Bite karibu na Dawasco mtaa wa kuingia shule ya Msingi kumbukumbu.
MWISHO WA KURUDISHA FOMU: Jumamosi tarehe 1 Augusti 2009.

TALENT FACTORY - MMTZ Centre for Talent Development through Arts education (Music, Dance, and Theatre & Fine Arts) and Artists’ meeting point.
MUSIC MAYDAY TANZANIA (MMTZ)
We support youth in Africa to explore, develops and utilizes their creative and Artistic talents for a better world.
MUSIC MAYDAY PROGRAMS
BCONNECTED FESTIVAL
CHEZA TANZANIA
MULTIMEDIA COMPUTER COURSES
MUSIC RECORDING
TALENT FACTORY
· DANCE TRAINING
· MUSIC TRAINING (THEORY AND INSTRUMENTS)
· THEATER TRAINING
· PAINTING TRAINING
WORKSHOPS
§ MUSIC
§ RECORDING
§ SOUND ENGINEERING
§ VIDEO PRODUCTION
SCHOLARSHIP & INTERSHIP SUPPORT
COMMUNITY SERVICE PROGRAMS
Music Mayday provides opportunities for creative and artistic development of youth in
Africa working towards a future in which all youth are able to contribute to a better world. Addis Ababa │ Amsterdam │
Dar es Salaam │ Budapest │
Johannesburg │ Kampala Music Mayday Tanzania│ Kijitonyama │ P.O. Box 34747 │ Dar es salaam │ Tanzania
T +255 (0)22 2771156 │ F +255 (0)22 2771157 │ http://www.tanzania.musicmayday.org/

WAGONJWA TARAFA YA KATERERO WALALA NA MAITI WODINI!!

Na Anna Nkinda - Maelezo 27-07-2009
Katoro Wagonjwa wa kijiji cha Katoro kata ya Katoro Tarafa ya Katerero wilaya ya Bukoba vijijini wanaolazwa katika kituo cha afya Katoro wanakabiliwa na tatizo la kulala na maiti wodini kutokana na kituo hicho kutokuwa na chumba cha kuhifadhia maiti.
Hayo yamesemwa jana na daktari Mfawidhi wa kituo hicho Augustine Mnyamukama wakati akisoma risara ya watumishi kwa mke wa Rais Mama Salma Kikwete aliyefika kituoni hapo kwa ajili ya kutoa vitanda vya kujifungulia viwili, vitanda vya kawaida vitano na mashuka kumi. "Kama mgonjwa akifariki katika kituo chetu hakuna mahali pa kuhifadhia maiti jambo ambalo linawafanya wagonjwa wa wodi husika kulala na maiti hadi ndugu wa marehemu watakapokuja kuichukua maiti na kwenda kuizika", alisema.
Dk. Mnyamukama aliyataja matatizo mengine yanayoikabili kituo hicho kuwa ni upungufu wa watumishi, upungufu wa madawa muhimu pamoja na vifaa, vitanda vya kuzalishia na vya kawaida, hakuna wodi maalum ya akina mama wajawazito na wanaume, kutokuwepo kwa huduma ya upasuaji wa dharula , nyumba za watumishi, umeme na maji. Aliendelea kusema kuwa pamoja na matatizo hayo jitihada za pamoja zinafanyika kati ya wananchi na Serikali ili kuweza kutatua matatizo hayo. "Hivi sasa tumefanikiwa kupata gari la kusafirisha wagonjwa wa dharula hali iliyosababisha kupungua kwa vifo wa watoto na kina mama wajawazito, tunatoa huduma ya Ugonjwa wa UKIMWI pia Halmashauri ya wilaya ya Bukoba kwa kushirikiana na wafadhili (JRF) wamewezesha kukarabatiwa kwa wodi ya watoto", alisema. Aliyataja magonjwa yanayowasumbua wananchi wa eneo hilo kuwa ni maralia, magonjwa ya nayoshambulia mfumo wa hewa, kuharisha, minyoo, upungufu wa damu, vichomi na magonjwa yanayosababishwa na virusi vinavyosababisha Upungufu wa Kinga Mwilini.
Akikabidhi vifaa hivyo Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) aliwataka wananchi wa eneo hilo kuvitunza vifaa hivyo ili viweze kutumika kwa muda mrefu kwa vizazi vijavyo. "Katika maeneo mengine wananchi wamekuwa wakiharibu na hata kuiba vifaa mbalimbali vinavyotolewa na wafadhili jambo ambalo limekuwa likikatisha tamaa na kurudisha nyuma maendeleo ya nchi", alisema.
Kituo hicho kipo umbali wa kilomita 58 kutoka Hospitali ya mkoa kilijengwa mwaka 1947 kikiwa zahanati na ilipofika mwaka 1974 kilipandishwa hadhi na kuwa kituo cha Afya kinahudumia zaidi ya wakazi 13,574 pamoja na kuhudumia zahanati za Kishogo, Butainamwa, Kaibanja, Ruhunga, Kihumulo na Kyamulaile.
Kwa upande wa tiba kituo hicho kinatoa huduma ya wagonjwa wanaotibiwa nyumbani na kurudi (OPD), kutibu wagonjwa kwa wastaini 90 kwa siku na kulaza wagonjwa wa wastani kumi na tisa kwa siku. Pia kituo kinatoa huduma za kinga kwa mama na mtoto, uzazi wa mpango, elimu ya afya kwa jamii, huduma ya mkoba, kuzuia maambukizi ya Virusi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto na upimaji wa virusi kwa hiari.
Mama Kikwete yuko katika ziara ya kikazi ya siku tatu katika mkoa wa Kagera yenye lengo la kuchangia juhudi za kupunguza vifo vya kinamama vinavyotokana na uzazi kwa kutoa vifaa vya huduma ya afya ya uzazi, hususan katika wodi za wazazi. Kuhamasisha juhudi za maendeleo kwa wanawake kupitia vikundi vya SACCOS na benki za vijijini- VICOBA. Kuhamasisha juhudi za kupunguza matukio ya mimba na utoro mashuleni, kuhamasisha vikundi vya SACCOS na benki za vijijini- VICOBA na kuhamasisha juhudi za kupunguza matukio ya mimba na utoro mashuleni.

Ancelotti: Terry going nowhere

Chelsea manager Carlo Ancelotti.

John Terry

Chelsea manager Carlo Ancelotti has urged people to trust him when he says John Terry will remain at Stamford Bridge.
The England captain has been linked with a British record move to big-spending Manchester City, with the Londoners having already rejected formal interest from Mark Hughes' men.

I don't think it is a necessity now for us to go out and spend a ridiculous amount of money trying to find the perfect signing.
Frank Lampard
Ancelotti was adamant when he first arrived at the club that Terry was a "symbol" of Chelsea and must be kept, and when asked again about the player's future on their pre-season tour of the United States, he said: "We have to wait and for some people, it's a problem to wait. But for sure, Terry will stay at Chelsea - we never had a problem. You have to have trust in me."
Chelsea striker Didier Drogba - who looks set to stay with the club after his own future was in doubt earlier this summer - added: "He's our captain and we need him. We know he's going to stay with us."
We have to wait and for some people, it's a problem to wait. But for sure, Terry will stay at Chelsea. You have to have trust in me.
Coach Carlo Ancelotti
Meanwhile, midfielder Frank Lampard does not think his club need to match City's spending to overhaul Manchester United as English Premier League champions. "I don't think it is a necessity now for us to go out and spend a ridiculous amount of money trying to find the perfect signing," he told the Sunday Mirror. "Of course, there's a couple of players out there who would add a lot to this team.
"But there are millions of players who would not add much to this squad because we are strong across the board."

Jumla ya wanafunzi 623 wa kike katika Mkoa wa Kagera wapata Mimba!!

Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiongea na wanafunzi katika moja ya ziara zake ambazo amekuwa akizifanya katika mikoa mbalimbali, hivi sasa yuko Mkoani Kagera kwa ziara ya siku tatu aliyoianza jana.

Na Anna Nkinda - Maelezo
26/07/2009 Kagera. Jumla ya wanafunzi 623 wa kike katika shule za Msingi na Sekondari mkoani Kagera wameacha shule kwa kipindi cha miaka miwili baada ya kupata ujauzito.
Hayo yamesemwa jana na Afisa elimu wa mkoa huo Florian Kimolo wakati akisoma tarifa ya maendeleo ya elimu kwa Mke wa Rais Mama Salma Kikwete ambaye ameanza ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani humo.
Akifafanua taarifa hiyo Afisa elimu huyo alisema kuwa wanafunzi waliopata ujauzito wa shule ya Msingi ni 395 na wa Sekondari ni 228.
"Tatizo la mimba mashuleni limekuwa ni sugu katika mkoa huu kwani wanafunzi wengi wenye umri mdogo wamekuwa wakikatiza masomo yao kwa kupata ujauzito na hivyo kuharibu mwelekeo wa maisha yao", alisema Kimolo.
Aliendelea kusema kuwa wilaya ya Chato ndiyo inayoongoza kwa wanafunzi wengi kupata ujauzito kwani wanafunzi wa shule za msingi 130 na wa Sekondari 74 walipata ujauzito.
Ili kutatua tatizo hilo Serikali imewachulia hatua mbalimbali wahusika wa matukio hayo ambapo hadi sasa kuna kesi zinazoendelea kwa watendaji, mahakamani na Polisi pia watuhumiwa watano wamefungwa.
Naye Mama Kikwete ambaye ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) alisema kuwa muitikio wa elimu katika mkoa huo ni mkubwa wanachotakiwa kufanya ni kuzungumza na watoto pamoja na wazazi na kuonyesha ushirikiano wa hali ya juu lazima tatizo hilo litatatuliwa.
"Katika mkoa wa Kilimanjaro tatizo la upatikanaji wa mimba mashuleni lipo chini ukilinganisha na mikoa mingine hapa nchini ni vyema mkawauliza mbinu gani wamezitumia katika hilo na kuweza kufanikiwa ili nanti muende kujifunza", alisema.
Mama Kikwete ameanza jana ziara ya kikazi ya siku tatu katika mkoa wa Kagera yenye lengo la kuchangia juhudi za kupunguza vifo vya kinamama vinavyotokana na uzazi kwa kutoa vifaa vya huduma ya afya ya uzazi, hususan katika wodi za wazazi. Kuhamasisha juhudi za maendeleo kwa wanawake kupitia vikundi vya SACCOS na benki za vijijini- VICOBA.
Kuhamasisha juhudi za kupunguza matukio ya mimba na utoro mashuleni, kuhamasisha vikundi vya SACCOS na benki za vijijini- VICOBA na kuhamasisha juhudi za kupunguza matukio ya mimba na utoro mashuleni.

MDAU SAMANTHA EDWIN TEMBA AFIKISHA SIKU YA 40!!

Edwin Temba aka (Mac Temba) anasema "Wadau jana mtoto wangu kafikisha siku ya 40 tangu azaliwe, akiwa na afya njema namshukuru sana mungu"! Na sisi pia kama wana FULLSHANGWE tunamtakia kila heri baby Samantha Edwin Temba pia tunawatakia bwana Edwin na my wife wake wampe malezi mema mtoto Samantha kwa sababu ya ugumu wa malezi kutokana na Utandawazi.

IAEA Director-General!!

IAEA Director-General ..
The International Atomic Energy Agency(IAEA) Director-General Mohamed ElBaradei is in Tanzania for a two days official visit.El Baradei discussed with President Jakaya Kikwete about peaceful use of Uranium,which has been recently discovered in Tanzania.Tanzania plans to use its uranium deposits to generate alternative energy with technical backing from the IAEA.Tanzania wants to work with IAEA to enhance local capacities through science and technology transfer mechanisms.ElBaradei visited neighbouring Kenya on Thursday and also will travel to South Africa and Botswana.

TWANGA PEPETA, MARLOW KUFANYA MAMBO MAKUBWA MISS TEMEKE 2009!!

Twanga Pepeta wakifanya vitu vyao mambo yatakuwa hivi Redds Miss Temeke 2009 TCC Sigara Chang'ombe ijumaa Agosti 1.

Msanii Marlow akiimba katika moja ya maonyesho yake.

Bendi ya African Stars "wana Dar es alaam" ama ukipenda Twanga Pepeta na Mwanamuziki Malon wanatarajiwa kutoa burudani katika shindano la Redds Miss Temeke 2009 linalotarajiwa kufanyika Agosti mosi kwenye ukumbi wa TCC sigara Chang'ombe, ambapo warembo takriban 12 wanatarajiwa kuchuana vikali katika kinyang'anyiro hicho.
Akiongea na Tovuti ya FULLSHANGWE mwandaaji wa shindano hilo kutoka kampuni ni BMP ambayo ndiyo imepewa dhamana ya kuandaa shindano hilo kwa kanda ya Temeke bw, Benny Kisaka, amesema mipango yote imekamilika hivyo kinachosubiriwa ni mashabiki watakaohudhuria katika shindano hilo kushangweka na burudani kutoka kwa wana Twanga Pepeta na Msanii maarufu na mkali katika muziki wa Bongofleva kwa sasa anayekwenda kwa jina la Malony ambaye amesumbua sana Ulaya na Marekani na kufanikiwa kujizolea mashabiki huko Ughaibuni
Ameongeza kuwa kwa sasa mazoezi yanaendelea kwenye ukumbi huohuo wa TCC Chang'ombe ambapo wapo chini ya jopo la walimu wanne ikiwa ni mwalimu wa kufundisha jinsi ya kutembea jukwaani na walimu wengine watatu kwa ajili ya kucheza shoo ya utambulisho, walimu hao ni Lona Swai Miss Temeke namba mbili mwaka jana, Bob Rich, Nyamwela kutoka Twanga pepeta na Mako Chale.
Shindano linadhaminiwa na Redds premium Cold , Vodacom, Aurora Security, Gazeti la Jambo Leo, 88.4 Clouds Fm, Mariedo Boutique, Valley Sping, Sophia Records, Raque Studio, Renzo Saloon, Mbunifu Ally Remtullah, Screen Masters tiketiza VIP zinauzwa 50.000 shilingi wasiliana na wahusika kwa namaba 0713406507.