Pages

WAZIRI WA KAZI PROF.KAPUYA AZINDUA MWAKA WA VIJANA!!

Mgeni Rasmi Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana Prof. Athman Jma Kapuya akiongea na vijana wakati wa kongamano la vijana lililoandaliwa na Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa YUNA na kufanyika ukumbi wa APEADU kwenye ofisi za Umoja huo mtaa wa Mafinga Kinondoni Jijini Dar es salaam katika kuadhimisha siku ya vijana Duniani.
Katika kongamano hilo vijana wamejadili mambo mbalimbali yanayowahusu kama vile Elimu, Afya, Ajira, Michezo, Haki zao na mambo mengine mengi wanayokumbana nayo katika maisha ya kawaida kama vijana huku wakiazimia kuomba Serikali iwaruhusu kuunda Baraza la Vijana la Taifa litakalosimamia mambo yao yote ili kuwatetea na kuwasimamia katika mipango mbalimbali ya Kisera inayowahusu vijana.
Katika Hotuba yake Waziri Kapuya amewaasa vijana kuunda Baraza litakalokuwa ni la kitaifa zaidi kuliko kuwa Baraza la kiubabaishaji linaloweza kuleta athari kubwa kwa taifa Waziri pia alizindua mwaka wa Vijana unaoanza leo tarehe 12 Agosti 2010 mpaka Agosti 11 , 2011 na utakuwa ukiadhimisha kila mwaka Duniani kote.
Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana Prof. Athman Juma Kapuya akiingia kwenye ukumbi wa mkutano wa kati wa kongamano la vijana lilioandaliwa na Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa YUNA na kufanyika ukumbi wa APEADU kwenye ofisi za umoja huo Mtaa wa Mafinga Kinondoni jijini Dar es salaam nyuma ya Waziri ni Mwakilishi wa UNIDO Nchini Emmanuel Kalenzi.
Vijana kutoka shule na Asasi mbalimbali za vijana waliohudhurika katika kongamano la vijana lililofanyika leo kwenye ofisi za Umoja wa Mataifa katika kuadhimisha siku ya vijana Duniani.

Mikoko ya Vodacom kukuza uchumi kwa washindi!!


Baadhi ya washindi wa magari ya Hyundai i10 yanayotolewa na Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania kupitia promosheni yake ya ‘Shinda Mkoko’ wamesema zawadi hiyo itawasaidia kukuza uchumi wao kwani itarahisisha usafiri katika shughuli zao.


Akizungumza kwa njia ya mahojiano kutokea Dodoma baada ya kuibuka mmoja wa washindi wa promosheni hiyo, Tolino Pechaga ambaye ni fundi umeme wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) alisema anatumaini gari hilo litakamilisha ndoto yake ya kimaisha katika kujiletea maendeleo.


Akifafanua alisema, ingawa alikuwa akitumia magari ya wafanyakazi kutoka Maili mbili anakoishi hadi Udom, ujio wa Hyundai i10 utamaliza muda wa kukimbizana na basi hilo na kumpa nafasi ya kufanya kazi zake binafsi baada ya muda wa kazi kwa mwajiri wake.


“Unajua mimi ni mwajiriwa wa chuo, lakini nafanya pia kazi zangu binafsi. Usafiri ulikuwa kikwazo namba moja kufikia malengo yangu, lakini sasa kila kitu kitaenda sawa kwani tayari nitakuwa na usafiri wangu binafsi utakaorahisisha maendeleo yangu,” alisema Pechaga.


Kwa upande wake Benard Asenga wa Keko Magurumbasi jijini ambaye ni mfanyabiashara wa duka la bidhaa ndogondogo na vyakula alisema alikuwa akitumia muda mwingi na baiskeli kufuata bidhaa sokoni Kariakoo, lakini gari hilo litamuwezesha kuboresha utoaji huduma kwa wateja wake.



Aidha Asenga alifafanua kwamba mara baada ya kukabidhiwa Hundai i10 aliyojishindia atabadilisha mtindo wa biashara anaoufanya na anafikiria kuwa mjasiriamali wa kati (SME’s) na kumiliki duka la bidhaa za jumla na rejareja.


“Sasa sitatumia tena baiskeli kufuata bidhaa mjini, nafikiria kukuza biashara yangu kutoka hatua moja kwenda nyingine jambo litakaloniwezesha kukuza hali yangu kiuchumi,” alisema mfanyabiashara huyo.


Naye Simon Kihuru ambaye ni dereva wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songea alisema zawadi hiyo iliyotolewa na Vodacom Tanzania itampunguzia gharama za usafiri kwa ajili kuwapeleka na kuwarudisha watoto wake shule kwani wataweza kutumia gari hiyo kwa matumizi ya binafsi.



“Kama nilivyosoma kwenye magazeti mbalimbali kwamba gari hiyo haitumii gharama kubwa kuihudumia, kwa kuwa mimi ni dereva itaniwezesha kutunza fedha zangu baada ya kukwepa huduma za daladala ambazo sio salama sana hususani kwa watoto,” alisema Kihuru.



Akizungumza hivi karibuni kwenye hafla ya uzinduzi wa promosheni ya ‘Shinda Mkoko’ iliyopanga kuwazawadia wateja wake gari moja aina ya Hyundai i10 kila siku Mkurugenzi wa Masoko wa Vodacom Tanzania Ephraim Mafuru alisema shindano hilo litawahusisha wateja wote wa kampuni hiyo nchini na kwamba ndani ya siku 100 kila siku mtu atakuwa anajipatia gari moja.

EUROPEAN THRILLER – BAYERN VS REAL - LIVE ON SUPERSPORT!!


Two of the traditional giants of European football clash in a mouth-watering pre-season friendly as Bayern Munich host Real Madrid at the Allianz Arena on Friday, live on your World of Champions.



Bayern were double winners in Germany last season and got their new campaign off to the perfect start with a comfortable 2-0 success over Schalke in the DFB Supercup at the weekend. They are the team to beat in Germany this year, but coach Louis van Gaal will have some personal reasons to want a win in this one too.




He has previously had two spells in charge of Real’s archrivals Barcelona, and nothing would please him more than to sow the seeds of doubt in the Madrid team’s pre-season plans. Real coach Jose Mourinho has been working hard at putting his personal stamp on the Spanish side he joined in June from European champions Inter Milan.




Mourinho plotted the downfall of Bayern in the UEFA Champions League title-decider in May, and now has a quick return fixture against the side. Pre-season friendlies count for little in the greater scheme of things, but nobody wants to lose a high-profile fixture such as this one.




Pride is everything in European football and there will be no shortage of it out there at the Allianz Arena when these giants go toe-to-toe in Munich. DStv viewers can tune in for live coverage of the match on Friday August 13 (2155) on SS3, SS3A, SS3N and Maximo.

MTANZANIA APATA NAFASI KUSOMEA SHAHADA YA UZAMILI CHINA!!

Balozi Mdogo katika Ubalozi wa China nchini Tanzania FU JIJUN (kulia) jana akimkabidhi fomu ya nafasi ya masomo nchi za nje( skolaship ) Mfanyakazi kutoka Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo Sozy Ngate ( kushoto) katika Ubalozi wa China jijini Dar es Salaam. (katikati ) ni Mkurugenzi wa Utamaduni kutoka Wizara ya Habari ,Utamaduni na Michezo Prof. Hermas Mwansoko. Ngate atakuwa nchini China kwa muda wa mwaka mmoja kusoma Shahada ya Uzamili katika Utawala.
(Picha zote na Mwanakombo Jumaa-MAELEZO) .
Balozi Mdogo wa China nchini Tanzania (charge d Affaires in the Chines Embassy in Tanzania) FU JIJUN (kulia) akiongea na Mkurugenzi wa Utamaduni kutoka Wizara ya Habari ,Utamaduni na Michezo Prof. Hermas Mwansoko jana katika Ubalozi wa China jijini Dar es Salaam wakati wa hafla fupi ya kumkabidhi fomu ya nafasi ya masomo ya Shahada ya Uzamili katika UTAWALA , Mfanyakazi wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo Makao Makuu Sozy Ngate(hayupo pichani).

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii yakabidhi vifaa Tiba Dodoma!!

Katibu Mkuu wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii bi. Blandina nyoni amekabidhi vifaa mbalimbali vya tiba katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, makabidhiano hayo yamefanyika juzi mkoani humo na hii ni moja ya mashine ya usingizi iliyokabidhiwa kwa hospitali hiyo
Katibu mkuu Bi Blandina Nyoni akikabidhi moja ya vifaa tiba vinavyotumika kwa ajili ya operesheni ya akina mama wajawazito kwa katibu Tawala wa mkoa wa Dodoma bi. Madenge

Moja ya kitanda kinachotumika kulazia mgonjwa anayehitaji uangalizi wa hali ya juu katika chumba cha watu mahututi(ICU)

BLOOD DIAMONDS - A TRAGEDY OF HISTORIC PROPORTION!!


African and international headlines have been dominated with the trial of former Liberian President, Charles Taylor and his alleged gift of blood diamonds to supermodel Naomi Campbell.



In the 1990s, the African countries of Sierra Leone, Liberia, Angola and the Democratic Republic of Congo disintegrated into civil war. Civilians were raped, murdered and attacked during the decade-long war. Collectively over 4 million civilians died.



What connected each conflict was the currency used to fund them – diamonds. HISTORY™ will provide a detailed look into the harsh reality behind the production of the world’s most valuable gems. Blood Diamonds depicts the brutality of a regime – supposedly backed by Charles Taylor – where millions of people lost their lives due to the conflicts over blood diamonds.




As citizens in four African warzones suffered, diamonds from those countries flowed freely into the world’s diamond market. Diamonds are the world’s most precious gems, but in West and Central Africa, their cost has been greater than anyone could have ever imagined.



Tune in to watch BLOOD DIAMONDS on the History Channel (DStv channel 254) on Saturday August 14 at 21.30.

MWENYEKITI WA (YUNA) HAPA NCHINI AWAPA CHANGAMOTO VIJANA!!

Mwenyekiti wa Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa hapa (YUNA) chini Benny Kikove akizungumza na wajumbe waliohudhurika kwenye kongamano la vijana linaloendelea kwenye ofisi za UN katika ukumbi wa APEADU Mtaa wa Mafinga Kinondoni jijini Dar es salaam, kongamano hilo linajadili mambo mbalimbali yanayowahusu vijana pamoja na changamoto wanazokumbana nazo katika ujana wao katikamkuadhimisha siku ya vijana duniani.
Wanafunzi wa shule mbalimbali wakiwa katika kongamano hilo wamesema wana matarajio mengi mara baada ya kongamano hilo kwani litawafanya kupeana uzoefu mbalimbali katika kukabili chanagamoto wanazokutana nazo katika maisha ya sasa.

Mmoja wa Wajumbe wa mkutano huo na Afisa wa UN hapa nchini Bi Hoyce Temu kushoto akiandika mambo mbalimbali yanaojadiliwa na vijana katika kongamano hilo.


Wajumbe mbalimbali wakimsikiliza mwenyekiti wa Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa hapa nchini YUNA Bw. Benny Kikove wakati alipokuwa akiongea na wajumbe wa konamano hilo asubuhi hii.

HRW: Zaidi ya watoto 700 watekwa na LRA


Karibu watu 700 wakiwemo watoto wametekwa kwa nguvu kutoka nyumbani kwao kwenye maeneo ya vijijini katika Jamhuri ya Afrika ya kati na kaskazini mwa Jamhuri ya demokrasi ya Congo.


Asili ya kundi la Lord's Resistance Army,linaloongozwa na Joseph kony,ni Kaskazini mwa Uganda.Leo hii wapiganaji wake wako hadi Congo kaskazini,Sudan Kusini na mashariki mwa Jamhuri ya Afrika ya Kati.


Shirika la kutetea haki za binaadamu la Human Rights Watch linasema kuna ushahidi kwamba kundi hilo limekuwa likiteka watu nyara kufwatia amri ya Joseph Kony.


Habari kwa hisani ya www.bbcswahili.com

TAIFA STARS NA HARAMBEE STARS NGUVU SAWA!!

Kiungo mshambuliaji wa Timu ya Harambee Stars ya Kenya, Macdonald Mariga (kushoto) akidhibitiwa na wachezaji wa Taifa Stars, Jerry Tegete (katikati) na Nurdin Bakari, wakati wa mchezo wa Kimataifa wa kirafiki uliochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam leo jioni. Timu hizo zimetoka sare ya bao 1-1.
Picha kwa hisani ya www.sufianimafoto.blog

Precision Air yaleta ndege mpya!!


Na Mwandishi Wetu


SHIRIKA la Ndege la Precision linalotoa huduma bora Tanzania, limetangaza kuleta ndege yake mpya ya sita aina ya ATR42-500 itakayowasili Agosti 26 mwaka huu kutoka Toulouse, Ufaransa, ikiwa ni sehemu ya kutekeleza programu ya kutoa huduma za kisasa zaidi. Mkurugenzi Mkuu na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Precision Air, Alfonse Kioko, aliwaambia waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuwa, ndege hiyo mpya itakayopachikwa jina la Bukoba, itafuatiwa na nyingine ya saba itakayoingia Septemba 15 mwaka huu.



Mwaka 2006, Precision na ATR ya Ufaransa walisaini mkataba wa dola za Marekani milioni 129 ili kutoa ndege saba mpya. Ndege ya kwanza kati ya hizo iliwasili Machi 2008. Tangu wakati huo, Precision imepokea ndege tano aina ya ATR 72-500 na kufanya iwe na ndege tano mpya mpaka sasa. Pia ina ndege nyingine tatu za zamani. Kioko alisema baada ya ndege hiyo yenye namba 5H-PWF kuwasili, wataizindua Dar es Salaam Agosti 27.




Alisema ina vifaa vya kisasa vya burudani kwa ajili ya wasafiri kuangalia sinema na kusikiliza muziki wakiwa safarini. Ndege hiyo ina uwezo wa kubeba abiria 70. Mkurugenzi huyo pia alitangaza kwamba tangu kuanza mwaka mpya wa fedha, idadi ya abiria wapya imeongezeka kwa asilimia 12 kulinganisha na mwaka jana. Pia mizigo ya biashara imeongezeka licha ya kudorora kwa uchumi duniani.




Akizungumza katika mkutano huo, Meneja Masoko wa Precision, Emillian Rwejuna alisema kampuni hiyo inatarajia kupata ndege ya Boeing 737, kati ya Oktoba na Novemba mwaka huu. Rwejuna alisema kupatikana kwa ndege hiyo kutapanua wigo wa huduma za safari.




Ndege hiyo ya tatu aina ya Boeing 737 itaboresha safari za Johannesburg, Afrika Kusini, na pia katika miji ya Kinshasa na Lubumbashi, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Precision Air hivi sasa inafanya safari katika miji ya Dar es Salaam, Mwanza, Tabora, Musoma, Shinyanga, Kigoma, Kilimanjaro, Zanzibar, Mtwara na Arusha. Pia ina safari za Nairobi na Mombasa, Kenya na Entebbe, Uganda.

WAGOMBEA UBUNGE WA CUF (W) ILALA WAJITAMBULISHA!!

Mgombea Ubunge kupitia Chama Cha Wannanchi CUF Hussein Siyoverwa akizungumza mbele ya wanahabari leo kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo wakati wagombvea hao kutoka Majimbo ya Ilala, Segerea na Ukonga walipojitambulisha mbele ya wanahabari, wanaofuatia katika picha ni Kimangala Ayubu Mussa na Gulam Nasoro Mkurugenzi wa Uenezi, Mahusiano ya Umma CUF Wilaya ya Ilala.
Wagombea wa ubunge katika majimbo ya Ilala, Segerea na Ukonga kupitia Chama Cha Wananchi CUF wakionyesha fomu zao mbele ya waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo leo mara baada ya kukabidhiwa na Mkurugenzi wa Wialaya ya Ilala leo, kutoka kulia ni Heko Pori Ukonga,Husein Siyoverwa Ilala na Kimangala Ayubu Musa Segerea.

MAOFISA HABARI WAKUTANA LEO JIJINI DAR.

Mkurugenzi wa Idara ya Habari(MAELEZO) Clement Mshana akiongea na Maofisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Wizara,Idara zinazojitegemea na wakala wa serikali leo jijini Dar es salaam.Pamoja na mambo mengine amewatoa wito kwa Maofisa hao kushiriki kikamilifu kutoa habari zinazohusu utendaji wa serikali kwa wananchi.
Maafisa habari wakiwa katika mkutano huo.
Baadhi ya Maofisa habari ,Elimu na Mawasiliano wa Wizara,Idara zinazojitegemea na wakala wa serikali wakifuatilia masuala mbalimbali leo jijini Dar es salaam wakati Mkurugenzi wa Idar ya Habari (MELEZO)Bw. Clement Mshana alipokutana nao. Picha na Aron Msigwa.

CLOUDS TV WAUNGANA NA MTV BASE

Usiku wa kuamkia leo, ndani ya ukumbi wa Much More uliopo katika jengo la Club Billicanas, umefanyika uzinduzi rasmi wa ushirikiano kati ya Clouds TV na televisheni ya Kimarekani MTV Base. katika ushirikiano huo, Clouds TV itakuwa ikirusha baadhi ya vipindi vya MTV Base kwa saa kadhaa kila siku jioni kuanzia saa 12. Pichani ni Mkurugenzi wa Clouds Entertainment Jose Kusaga (kulia) akitoa shukrani zake kwa MTV Base kupitia mwakilishi wao Mr. Paul

TWIGA STARS RECEIVED BY WASHINGTON GOVERNOR CHRISTINE GREGOIRE!

The Twiga Stars pose with Washington's governor, Christine Gregoire.
Photos and Story By Nisha Ligon http://www.twigastars.com/.
Today the Twiga Stars, Tanzania's national women's football team, visited the Washington State Capitol, where they were received by Governor Christine Gregoire. The Twiga Stars, who were brought to Washington State for a training tour by Rahma Al-Kharoosi, president of RBP Oil and Industrial Technologies, got the chance to learn about state legislative procedure, sing a Tanzanian song for their hosts, and to speak to the Governor herself. She wished them the best of luck and told the Tanzania ladies that she has a special interest in women's football as both of her daughters are footballers. Ms. Al-Kharoosi thanked the Governor for taking the time to speak to them, and added that it was inspiring for the girls to meet such an accomplished woman who has shown "yes we can."
A special tradition at the Washington Legislative Building is to make a wish while rubbing the nose of a George Washington bust. The Twiga players each took a rub and wished to make it to the Women's World Cup (to be held in Germany in summer 2011).
The Twiga Stars have been training in Washington since August 2, and are preparing for the African Women's Championship to be held in South Africa this October. The top two teams from the African Championship will proceed to the Women's World Cup in Germany. The Twiga Stars have shown they're ready for the competition by posting a number of impressive performances here in Washington, including a 4-0 victory over Dos FC last night. Asha "Mwalala" Rashid scored 2 goals, while Mwanahamis Omary and Fatuma "Kitunini" Mustapha each scored one. Ms. Al-Kharoosi said she's very happy with the teams performance and is confident that they are gaining the experience they need to succeed in the continental championship this

The players pose with George Washington Statue!
Twiga Stars matron Rahma Al-Kharoosi rubs George Washington's Statue and wishes for her girls to make it to the World Cup.

Ms. Al-Kharoosi, who has arranged and paid all expenses for this trip.
Photo op outside of the State Capitol

Ukweli Kuhusu Haruna Moshi ‘ Boban’ : Alikosa Namba Gavle IF


Na Maggid Mjengwa,Gavle, Sweden



HII ni sehemu tu ya makala inayohusu sakata la Haruna Moshi kukatisha mkataba na klabu ya Gavle IF. Kuna mengi yamesemwa na kuandikwa kuhusu Haruna Moshi kukatisha ghafla mkataba wake na klabu ya Gavle IF ya hapa Sweden. Hata hivyo, wapenzi wa soka wa Tanzania hawakuweza kupata ukweli hasa juu ya sakata la Haruna Moshi ‘ Boban’.



Nikiwa katika mji wa Gavle, mahali ambapo Haruna Moshi aliishi na kucheza kandanda ya kulipwa nimeweza kukusanya taarifa zenye kuonyesha nini kilitokea.




Kwa mujibu wa taarifa hizo, Haruna Moshi alikuwa na uwezo wa kuichezea klabu hiyo. Kilichojitokeza ni kwa Haruna Moshi kuwa majeruhi kwa muda mrefu huku nafasi ya kiungo wa kati anayoichezea ikigombaniwa na wachezaji zaidi ya watatu.Katika muda wote aliokuwa na Gefvle IF, Haruna Moshi amecheza mechi tano tu za Ligi Kuu ya Sweden.




Katika mechi hizo, ni mbili tu amecheza tangu mwanzo na nyingine tatu aliingia akitokea kwenye benchi la wachezaji wa akiba.Kwa mujibu wa maelezo ya Mkuu wa Idara ya Michezo ya klabu ya Gefle IF, Per Olson yeye anaamini, kuwa Haruna ana bahati mbaya.




Kuwa hata walipokwenda kwenye kambi ya mazoezi nje ya nchi, Haruna hakuwepo kutokana na familia yake kutarajia kupata mtoto. Hivyo, alikosa mechi tatu muhimu za kujipima nguvu na ambazo zingemweka Haruna Moshi kwenye nafasi nzuri ya kushindania namba.




Na mchezaji aliyesababisha Haruna Moshi abaki kwenye benchi ni Yussif Chibsah kutoka Ghana. Chibsah anachezea nafasi ya kiungo wa kati kama alivyo Haruna Moshi. Kurejea kwake katika klabu hiyo akitokea Ghana ndiko kulikofuta kabisa matumaini ya Haruna Moshi.




Ni nani huyu Yussif Chibsah? Na je, ilikuwa ni sahihi kwa Haruna Moshi kukatisha mkataba wake? Angeweza kubaki Sweden na kucheza katika klabu nyingine? Itaendelea… Habari hii ni kwa hisani ya


http://www.kwanzajamii.com/?p=2705 kwa habari zaidi bofya hapo.

M-Net's Big Brother ALL STARS: Images from day 21 (Sunday August 8, 2010)

It’s day 21 on M-Net’s Big Brother All Stars --- and Lerato is evicted from the Big Brother All Stars into the Barn, to join Hannington and Sammi. Last night’s show also featured Malawian rising star Young Kay. Stay tuned to M-Net’s BIG BROTHER ALL STARS with 24/7 coverage on DStv channel 198 plus daily edited shows on M-Net and AfricaMagic. For more information on the series, log on to www.mnetafrica.com/bigbrother.