MWENYEKITI WA (YUNA) HAPA NCHINI AWAPA CHANGAMOTO VIJANA!!

Mwenyekiti wa Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa hapa (YUNA) chini Benny Kikove akizungumza na wajumbe waliohudhurika kwenye kongamano la vijana linaloendelea kwenye ofisi za UN katika ukumbi wa APEADU Mtaa wa Mafinga Kinondoni jijini Dar es salaam, kongamano hilo linajadili mambo mbalimbali yanayowahusu vijana pamoja na changamoto wanazokumbana nazo katika ujana wao katikamkuadhimisha siku ya vijana duniani.
Wanafunzi wa shule mbalimbali wakiwa katika kongamano hilo wamesema wana matarajio mengi mara baada ya kongamano hilo kwani litawafanya kupeana uzoefu mbalimbali katika kukabili chanagamoto wanazokutana nazo katika maisha ya sasa.

Mmoja wa Wajumbe wa mkutano huo na Afisa wa UN hapa nchini Bi Hoyce Temu kushoto akiandika mambo mbalimbali yanaojadiliwa na vijana katika kongamano hilo.


Wajumbe mbalimbali wakimsikiliza mwenyekiti wa Asasi ya Vijana ya Umoja wa Mataifa hapa nchini YUNA Bw. Benny Kikove wakati alipokuwa akiongea na wajumbe wa konamano hilo asubuhi hii.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment