RAIS KIKWETE ALIPOTEMBELEA NANENANE MKOANI DODOMA HIVI KARIBUNI!!

Mkurugenzi wa Maendeleo ya Mazao (KIUMO) Bwana Geoffrey Kirenga akimwelezea Rais Jakaya Kikwete namna ya utekelezaji wa Mpango wa Ruzuku ya Pembejeo za Kilimo kwa kutumia utaratibu wa vocha nchini wakati wa Maonyesho ya Nanenane Mkoani Dodoma hivi karibuni.
(Picha zote na Anna Itenda wa Maelezo)
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Bi Nyabaganga Taraba (kushoto) akimwelezea Rais Jakaya Mrisho Kikwete jinsi ya utaratibu wa kuendeleza miradi ya Umwagiliaji alipotembelea kwenye Maonyesho ya Nanenane Mkoani Dodoma .

Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano Bi Nyabaganga Taraba (kushoto) akimwelezea Rais Jakaya Mrisho Kikwete jinsi ya utaratibu wa kuendeleza miradi ya Umwagiliaji alipotembelea kwenye Maonyesho ya Nanenane Mkoani Dodoma .

Rais Jakaya Kikwete mpenzi wa watoto akiwa kwenye picha ya pamoja na mtoto Betha Chiwanga na mama yake Neema Chiwanga walipokutana na Rais njiani wakati wa maonyesho ya nanenane Mkoani Dodoma hivi karibuni.



Mkurugenzi Mkuu wa Jukwaa la Wakulima na Wafugaji (Farmers Centre Ltd )akimwonyesha madawa mbalimbali yanayotumika kwa ajili ya Wakulima na wafugaji kwenye maonyesho ya Nanenane yaliyofanyika Mkoani Dodoma hivi karibuni .

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment