Rais Kikwete azindua Ujenzi wa Miundombinu ya Mfumo wa Mabasi yaendayo Haraka Dar es Salaam!!

Rais Jakaya Mrisho Kikwete ,Mwakilishi mkazi wa Benki ya Dunia John Mc Intyre(watatu kulia),Waziri wa Miundombinu Dr.Shukuru Kawambwa(kushoto) na Waziri wa TAMISEMI Mhe.Selina Kombani(kulia) wakifunua kitambaa kuashiria kuzindua rasmi ujenzi wa Miundombinu ya mfumo wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam wakati wa sherehe za uzinduzi zilkizofanyika Ferry kivukoni jijini Dar es Salaam leo mchana.
(Picha na Freddy Maro)
Mtendaji Mkuu wa Mradi wa Mabasi yaendayo Haraka jjijini Dar es Salaam(Dar Rapid Transit Agency ) Bwana Cosmas Takule akieleza jinsi mradi huo utakavyofanya kazi pindi utakapo kamilika hivi karibuni jijini Dar es Salaam huku Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaamm williuma Lukuvi wakisikiliza kwa makini.

Mtendaji Mkuu wa Mradi wa mabasi yaendayo Haraka jijini Dar es Salaam Bwana Cosmas Takule akionyesha mchoro wa ramani ya utekelezaji wa mradi huo jiji Dar es salaam huku Rais Jakaya Mrisho Kikwete,Waziri wa Miundombinu Dr.Shukuru Kawambwa, Waziri wa TAMISEMI Bi.Selina Kombani na Mwakilishi Mkazi wa Benki ya dunia Bwana John Mc Intyre wakisikilza kwa makini wakati wa sherehe za uzinduzi wa ujenzi wa miundombinu ya mradi huo zilizofanyika Ferry Kivukoni, jijini Dar es Salaam leo mchana.



You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment