Viongozi wa vyama vya upinzani wampongeza Rais Kikwete Dodoma!!

Mwenyekiti CUF Profesa Ibrahim Lipumba akimpongeza Mwenyekiti wa CCM taifa,Rais Jakaya Mrisho Kikwete wakati wa ufunguzi wa Mkutano mkuu wa CCM uliofanyika katika ukumbi wa Kizota mjini Dodoma jana.

Msanii Dokii akiwatumbuiza wajumbe wa MkutanoMkuu wa CCM katika ukumbi wa Kizota mjini Dodoma jana.

Mwanasiasa mkongwe Kingunge Ngombale Mwiru akijadiliana jambo na Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Jakaya mrisho Kikwete pamoja na katibu mkuu wa CCM Yusuf Makamba wakati wa mkutano mkuu wa CCM unaofanyika mjini Dodoma(picha na Freddy Maro)

Baadhi ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM wakimpongeza mwenyekiti wa TLP Augustine Mrema wakati alipokuwa akitoa salamu za Chama chake na kumpongeza Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa kutekeleza kwa ufanisi program mbalimbali za maendeleo nchini.

Mwenyekiti wa CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mkewe Mama Salma Kikwete wakiongea na Katibu Mkuu wa CCM Yusuf Makamba muda mfupi baada ya kumalizika kwa awamu ya kwanza ya mkutano Mkuu wa CCM mjini Dodoma jana jioni Mkutano huo unaendelea leo asubuhi.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment