TAMASHA LA VODACOM SABASABA CONCERT LILIVYOFANA MWEMBEYANGA!!

Msanii wa muziki wa kizazi kipya Ambwene Yesaya (AY) akifanya vitu vyake jukwaani wakati wa tamasha hilo” Sabasaba Concert “ lililoandaliwa na kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom na kufanyika kwa siku mbili mfululizo Julai 6-7 kwenye viwanja vya Mwembeyanga wilayani Temeke, tamasha hilo lilishirikisha wasanii wa mbalimbali pamoja na bendi za muziki wa dansi.

Wanamuziki wa bendi ya Akudo Impact wakicheza jukwaani wakati wa tamasha la “Sabasaba Concert “ ambalo liliandaliwa na kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania na kufanyika kwenye viwanja vya Mwembeyanga wilayani Temeke jijini Dar es salaam lililoshirikisha wasanii mbalimbali wa muziki wa kizazi kipya na bendi za muziki wa dansi.

Akudo Impact wakifanya mambo makubwa katika tamasha la Sabasaba Concert katika viwanja vya Mwembeyanga Wilayani Temeke.
Ilikuwa ni shangwe kwa kwenda mbele kwani wasanii mbalimbali walifanya mambo makubwa katika tamasha hilo jana.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment