KATIBU MKUU VIWANDA NA BIASHARA AFUNGUA KONGAMANO LA WAJASIRIAMALI KARIMJEE!!

Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara Bi. Joyce Mapunjo akikata utepe kuashiria ufunguzi wa maonyesho ya wajasiriamali kwenye kongamano la Wajasiriamali linalozungumzia mambo mbalimbali ya wajasiriamali katika kuchangia maendeleo ya nchi, lakini pia wajasiriamali hao. kubadilishana mawazo na uzoefu katika biashara zao ili kuifikisha mbali zaidi sekta ya kiuchumi, kupitia wajasiriamali na kuwaletea maendeleo.

Kongamano hilo linakwenda pamoja na maadhimisha ya siku ya wajasiriamali na maonyesho ya taasisi mbalimbai za kibiashara na yafanyika kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam, katika picha katikati ni Bw. Paul Mashauri Mratibu wa maonyesho hayo na kulia ni Juliet Mwinuka Meneja Mradi.


Mgeni rasmi akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa kongamano hilo mara baada ya kuzindua maonyesho hayo kweny viwanja vya Karimjee.
Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara B. Joyce Mapunjo akifungua kongamano hilo kwa hotuba, kulia katika picha ni Rais wa shirikisho la wafanyabiashara wenye Viwanda TCCIA Elvis Musiba.

Washiriki mbalimbali wa kon gamano hilo wakimsikiliza Katibu mkuu Viwanda na Biashara alipokuwa akitoa hotuba yake

Akina mama pia wamekuwa mstari wa mbele katika kongamano hilo kama unavyowaona wakiwa na makabrasha yao na kufuatilia kwa makini kila kilichoendelea.

Mjasiriamali na mbunifu wa mavazi Mustafa Hassanali kushoto alikuwepo katika kongamano kama unavyomuona akifuatilia kwa makini hotuba ya Katibu Mkuu wa Viwanda na Biashara Bi Blandina Nyoni hayupo pichani

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment