Rwanda imesema haihusiki na kumpiga risasi aliyekuwa mkuu wa majeshi anayeishi uhamishoni nchini Afrika Kusini.
Luteni Jenerali Faustin Kayumba Nyamwasa, mkosoaji wa Rais wa Rwanda, yuko katika hali mbaya baada ya kupigwa risasi nje ya nyumba yake mjini Johannesburg.
Luteni Jenerali Faustin Kayumba Nyamwasa, mkosoaji wa Rais wa Rwanda, yuko katika hali mbaya baada ya kupigwa risasi nje ya nyumba yake mjini Johannesburg.
Rosette Nyamwasa amesema ilikuwa ni jaribio la mauaji kwani mtu huyo mwenye silaha hakudai fedha au chochote kabla ya kumpiga risasi mume wake.
Serikali ya Rwanda imekana kuhusika na madai hayo.
Serikali ya Rwanda imekana kuhusika na madai hayo.
Luteni Jenerali Nyamwasa alipigwa risasi tumboni na amekuwa akifanyiwa upasuaji katika hospitali moja mjini Johannesburg.
Mchambuzi wa BBC wa masuala ya Afrika Martin Plaut amesema tangu alipoondoka Kigali mwezi Februari, Luteni Jenerali Nyamwasa amekuwa kama mwiba kwa Rais Paul Kagame, ambaye anamshutumu kwa ufisadi.
Mchambuzi wa BBC wa masuala ya Afrika Martin Plaut amesema tangu alipoondoka Kigali mwezi Februari, Luteni Jenerali Nyamwasa amekuwa kama mwiba kwa Rais Paul Kagame, ambaye anamshutumu kwa ufisadi.
Kukana rasmi
Familia ya Nyamwasa ilikuwa inarejea kutoka kununua bidhaa kwenye majira ya mchana siku ya Jumamosi wakati mtu huyo mwenye silaha alipokaribia gari lake.
Bi Nyamwasa ameiambia BBC, " Mtu mwenye silaha alizungumza na dereva wangu, lakini alitaka nafasi apate kumpiga risasi mume wangu."
" Mume wangu alipoinama, akafyatua risasi. Na bahati nzuri, imempata kwenye tumbo na si kichwani... Mume wangu alitoka haraka...na akainyakua bunduki. Katika fujo kama hiyo, mtu huyo hakuweza kufyatua risasi."
Familia ya Nyamwasa ilikuwa inarejea kutoka kununua bidhaa kwenye majira ya mchana siku ya Jumamosi wakati mtu huyo mwenye silaha alipokaribia gari lake.
Bi Nyamwasa ameiambia BBC, " Mtu mwenye silaha alizungumza na dereva wangu, lakini alitaka nafasi apate kumpiga risasi mume wangu."
" Mume wangu alipoinama, akafyatua risasi. Na bahati nzuri, imempata kwenye tumbo na si kichwani... Mume wangu alitoka haraka...na akainyakua bunduki. Katika fujo kama hiyo, mtu huyo hakuweza kufyatua risasi."
Amesema Bw Kagame alitaka mume wake afe.
Amesema, " Bw Kagame amesema bungeni kwamba anataka kumwuua mume wangu, na atamfuata popote alipo na kumwuua."
Lakini serikali ya Rwanda imeiambia BBC kwamba "inauamini uwezo wa serikali ya Afrika Kusini wa kufanya uchunguzi wa kina wa tukio hilo".
Amesema, " Bw Kagame amesema bungeni kwamba anataka kumwuua mume wangu, na atamfuata popote alipo na kumwuua."
Lakini serikali ya Rwanda imeiambia BBC kwamba "inauamini uwezo wa serikali ya Afrika Kusini wa kufanya uchunguzi wa kina wa tukio hilo".
Waziri wa mambo ya nje Louise Mushikiwabo amesema katika taarifa yake, " Tumesikia taarifa hizi kupitia vyombo vya habari, hatuna uthibitisho wa tukio hili."
" Tunaitakia familia ustahamilivu na nguvu." Kwa Habari zaidi nenda
" Tunaitakia familia ustahamilivu na nguvu." Kwa Habari zaidi nenda






0 comments:
Post a Comment