REDDS MISS KINONDONI WATEMBELEA FREE MEDIA!!

Mhariri mtendaji wa gazeti la Tanzania Daima linalochapishwa na kampuni ya Free Media Absalom Kibanda akiongea na warembo wanaoshiriki katika shindano la Redds Miss Kinondoni wakati warembo hao walipotembelea chumba cha habari cha gazeti hilo mchana huu katika ofisi zao zilizopo mtaa wa Mkwepu jijini Dar es salaam.
Ziara hii ya warembo ni ya kimafunzo kabla hawajapanda jukwaani julai 2 kwa lengo la kujifunza mambo mbalimbali yanayofanywa katika utayarishaji wa gazeti hilo.
Warembo hao wanatarajiwa kuchuana katika kinyang'anyiro kitakachofanyika ijumaa wakiwania taji hilo kwenye ukumbi wa Mlimani City uliopo Chuo Kikuu cha Mlimani jijini Dar es salaam, katika shindano hilo burudani itatolewa na vijana machachari kutoka kundi la THT la jijini Dar es salaam pamoja na Sebene la kukata na shoka kutoka kwa vijana wa African Stars wana wa (Kutwanga na kupepeta).
Mhariri mtendaji wa Gazeti la Tanzania Daima Absalom Kibanda katikati akimtambulisha Kaimu Mhariri Mtendaji wa gazeti hilo Ansbert Gurumo kushoto kwa warembo wa Redds Miss Kinondoni waliotembelea ofisi za gazeti hilo leo mchana.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment