LIGI YA MUUNGANO KIKAPU KUFANYIKA JULAI 3-9 MWAKA HUU

Katibu mkuu wa shirikisho la mpira wa kikapu nchini (TBF) Alexander Msoffe akizungumza na wanahabari kwenye ukumbi wa idara ya habari maelezo asubuhi hii jijini Dar es salaa wakati alipokuwa akitangaza kuanza kwa ligi Muungano katika mchezo huo inayotarajiwa kufanyika visiwani Zanzibar kuanzia Julai 3-9 mwaka huu. ambapo itashirikisha timu nane kutoka bara na timu nane kutoka visiwani, ambapo mgeni wa heshima atakuwa Jaji Mkuu wa Tanzania Augustino Ramadhan.
Timu zinazotarajiwa kushiriki ligi hiyo kwa wanaume na wanaume ni Savio,JKT, Oilers, Mzinga Corporation wanaume, wanawake ni Jeshi Stars Police Dar es salaam Lioness na CMTU.
Kwa upande wa Zanzibar timu za wanau ni Stonme Town, Kisima Majogoo, Rangers, Tornardo, na wanawake ni Jeshi , JKU na Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji.
Katika picha kushoto ni Afisa habari mwandamizi wa Idara ya Habari Maelezo Bw. Mwirabi Cisse.
Mike Maluwe katibu mkuu wa TBF akifafanua jambo katika mkutano huo uliofanyika leo kwenye ukumbi wa idara ya habari maelezo jijini Dar es salaam kushoto ni katibu mkuu wa TBF Alexander Msofe.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment