HII NDIYO TANO BORA YA SHINDANO LA KIPAJI LA REDDS MISS KINONDONI!!

Hii ndiyo tano bora ya shindano la kipaji la Redds Miss Kinondoni lililofanyika usiku wa kuamkia leo kwenye Hoteli ya Giraffe Ocean View iliyoko Mbezi jijini Dar es salaam warembo wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya jaji mkuu Gerald Hando kutangaza matokeo, kutoka kulia ni Irene Hezron, Salma Ally, Alice Lushiku, Caroline Mbembo na Tamara Ally.

Hapa majaji wakiwa makini ili kuhakikisha kazi yao inakwenda vizuri katika shindano hilo.
Huyu yeye alichora bango lenye ujumbe wa kupambana na ugonjwa wa ukimwi kama bango lake linavysomeka.

Huyu alitangaza lakini anelekea yuko sawasawa na kama kuna redio inahitaji mtangazaji hebu jaribuni kuongea na huyu anaweza kuwafaa.
Huyu akalimwaga sebene la kukata na shoka.
Huyu naye akacheza nyimbo ya Kiarabu.
Shindano la kipaji lilianza kwa mrembo huyu kucheza.
Mh! wadau hawa utamu wa Redds uliwadatisha kidogo hebu wacheki mdau.
Mwanaharakati na Muelimishaji Mama Sadako Kulia akiwa na mwanaye anayempenda Aziza nao walijimwaga ukumbini ili kujua kilichojiri katika shindano hilo.
Wanamuziki wa bendi ya Kalunde kutoka kulia ni waimbaji Mwabi Mwapwani, Sarafin Mshindo, Debora Nyangi pamoja naye mpiga gitaa la sollo mpya wa bendi hiyo Eddo wakipozi kwa picha.
Kutoka kulia ni katibu mkuu kamati ya Miss Tanzania Bosco Majaliwa Mwenyekiti wa kamati ya Miss Tanzania Prashant Patel na Mwenyekiti wa kamati ya Miss Kinondoni Boy George na Mkurugenzi wa kamati ya Miss Kinondoni Rahma George.
Wadau hawa kutoka kanda ya Pwani na Kitongoji cha Sinza walikuwepo kwenye shindano la kipaji la Redds Miss Kinondoni.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

1 comments:

  1. Sina mbavu!...

    HAPANA, NAHITAJI KUISHI!

    So what you doing in a prostitution propagating event such as this one? Grow up, this is the territory, hapa hamna vipaji wala nini, ni biashara...

Post a Comment