Bonanza Nyama Chabezi Tegeta Jumapili,Vimwana wa Mashujaa kupamba jukwaa!!


Bendi ya Mashujaa Musica (Watoto wa Cash Lady) siku ya jumapili itashuka katika viwanja vya Nyama Chabezi Tegeta kutumbuiza wakati wa Bonanza litakaloshirikisha vikundi mbalimbali vya Viduku, na Michezo ya watoto ikiwa ni pamoja na Pool, kuvuta kamba michezo yote itaanza saa nane mchana ikiwa ni pamoja na michezo ya watoto ya kukimbiza Kuku na watoto kushindana kucheza makirikiti.

Burudani hiyo itaanza saa nane mchana ambapo Mashujaa Musica watatumbuiza chini ya wanamuziki wake wote akiwemo Rapa Mahili Ibrahim Milinda Nyeusi(Vuvuzela), Kiongozi wa Bendi Jado Fidifosi, Mtalaam wa Masauti Pasia Budance na Raja Rada. Kwa mujibu wa msemaji wa Mashujaa musica, Shaaban Mpalule, Maandalizi yote kwa ajili ya onyesho hilo yamekamilika “sisi tumeshajipanga kwa ajili ya burudani hiyo, hivyo kazi imebaki kwa wakazi wa eneo hilo kujitokeza kwa wingi ili washuhudie kazi mpya ya bendi yangu ikiwa ni pamoja na kupata radha mpya ya nyimbo mpya”alisema Mpalule Hiyo itakuwa ni mara ya kwanza kwa bendi ya Mashujaa kutumbuiza katika eneo la ukunda wa Mbezi ambapo wamesema wataonyesha miondoko mbalimbali ikiwemo kuchinja bata, Wamefulia, kwa kiingilio cha shilingi elfu tatu wakubwa na watoto shilingi mia tano.

Wakazi wa Tegeta na maeneo yanayokaribiana mmetakiwa kufika siku hiyo ili kushuhudia burudani hizo, ambapo zawadi mbalimbali zimeandaliwa kwa mashabiki 50 wa kwanza watakaowahi kuingia kukaa katika sehemu zao. Mashujaa Musica kwa sasa imekamilisha kurekodi nyimbo sita ambapo wanatazamia kufanya uzinduzi wa Album yao ya kwanza yenye nyimbo Mwanike, Moshi wa Sigara, Safari ya Vikwazo, Deodata, Mama Mi Nashangaa, sambamba na Intro ambazo zinaendelea kutesa katika sehemu mbalimbali za vyombo vya habari, Radio, Magazeti, na Tv.

Ratiba ya wiki Mashujaa Musica Jumatano –Mashujaa Pub Vingunguti Kiingilio KinywajiIjumaa - woodland kiwalani kwa jimmy kiingilio 3000 Jumamosi –Mashujaa Pub Vingunguti Kiingilio shilingi elfu 2000Jumapili - Nyama Chabez Tegeta Kiingilio Shilingi 3000 wakubwa na watoto 500.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment