Waziri wa Fedha apokea msaada wa waathirika wa Kilosa Ikulu jioni hii!!

Waziri wa Fedha na Uchumi Mh. Mustafa Mkulo akipokea shehena ya marobota ya viatu alivyokabidhiwa leo jioni Ikulu kwa ajili waathirika wa mafuriko ya Kilosa. Msaada huo umetolewa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kupokea kutoka Serikali ya China hivi karibuni. Msaada huo ulikabidhiwa na Naibu Katibu wa Rais Ndugu Shabani Gurumo kwa niaba ya Rais.

Waziri wa Fedha na Uchumi Mh. Mustafa Mkulo akiendesha moja ya baiskeli za misaada kwa ajili ya waathirika wa mafuriko ya Kilosa baada ya kukabidhiwa na Rais kikwete leo Ikulu jijini Dar es salaam.
Waziri wa Fedha na Uchumi Mh. Mustafa Mkulo akionyesha mmoja ya pikipiki alizokabidhiwa leo Ikulu na Rais Kikwete kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa mafuriko ya Kilosa.

Waziri wa Fedha na Uchumi Mh. Mustafa Mkulo akitoa maelezo leo Ikulu jijini Dar es salaam kwa Naibu Katibu wa Rais Ndugu Shabani Gurumo(kushoto) na Msemaji wa Wizara ya Fedha na Uchumi Bi. Ingiahedi Mduma(katikati) ,jinsi atakavyoigawa misaada ya wathirika wa mafuriko ya Kilosa aliyopatiwa leo Ikulu na Rais Kikwete




You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment