Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 122 wa IPU wampongeza Balozi Sisco kwa mapokezi mazuri Thailand!!

Spika wa Bunge Mhe. Samuel Sitta na Balozi Sisco Mtiro wakibadilishana vitabu vilivyo tiwa sahihi za wajumbe waliohudhuria Mkutano wa 122 wa IPU toka Tanzania na wageni waalikwa kama ishara ya kumbukumbu ya mkutano huo.
(Picha na Afisa Habari wa Bunge Owen Mwandumbya)

Mhe. Dr. Christene Ishengoma naye akitoa Salam za Pongezi kwa mapokezi mazuri kwa balozi Cisco (mwisho kulia) kwa kipindi chote ambacho wamekua nae hapa Bangkok thailand kuhudhuria mkutano wa 122 wa IPU. Katikati ni Mhe. Prof. Idris Mtulia (Mb)

Spika wa Bunge. Mhe. Samuel sitta akitoa shukrani zake kwa Balozi Cisco Mtiro kwa mapokezi mazuri (kulia) kwa niaba ya ujumbe wa Tanzania unaohudhuria mkutano wa 122 wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU)
wakati wa chakula cha usiku jana, katika Hotel ya Conrad mjini Bangkok. Balozi Cisco licha ya kuwa Ubalozi wake upo Kuala Lumpar Malaysia, pia anashughulikia nchi ya Thailand ambapo kwa kipindi hiki cha mkutano wa 122 wa IPU naye yupo Bangkok kuratibu ugeni wa Tanzania katika nchi hii.

Mhe. Balozi Sisco Mtiro akitoka nje ya Hotel ya Conrad, Mjini Bangkok Thailand, mara baada ya chakula cha usiku na ujumbe wa Tanzania unaoshiriki
mkutano wa 122 wa IPU katika hotel ya Conrad, kulia kwake ni Afisa Habari wa Bunge Owen Mwandumba akimsindikiza.

Spika wa Bunge akifurahia zawadi ya Track suite zenye nembo na rangi ya CCM ambazo zimetengenezwa na Mtanzania anayefanya shughuli zake hapa Bangkok Thailand, Bwana Nicholaus Kipalanga (kulia) alipomtembelea jana katika Hotel ya Conrad jana Usiku. Bwana kapalanga anakampuni yake inayojishughilisha na uuzaji madini iitwayo Asili Germs International Co. Ltd ambapo pamoja na madini anafanya biashara za kutengeneza nguo za sare kwa order Maalumu kama vile sare za makampuni, Tshirt na truck suite kwa ajili vyama na kampeni mbalimbali.





You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment