TATIANA DURAO BALOZI WA MATENDE AFRIKA MASHARIKI NA KATI!!

Balozi wa ugojwa wa Matende (ELEPHANTIASIS DISEASE) kwa nchi za Mashariki na Afirica ya kati (Ambassador for Elephantiasis disease in East and Central Africa) ambaye pia ni Mshindi wa pili wa BBA2 Tatiana Durao kutoka Angola , leo jijini Dar es Salaam amezungumza na wandishi wa habari kuhusu kusherehekea siku yake ya kuzaliwa Machi 31, 2010 pamoja na hilo atafanya ziara fupi katika kisiwa cha Unguja pamoja na kuwasaidia watoto wa KIWOHEDE wa jijini Dar es Salaam.
Tatiana Durao z ameongeza kuwa sasa amechaguliwa kuwa balozi wa Matende Afrika ya mashariki na kati na pia ni mlezi wa kituo cha watoto yatima cha Kiwohede kilichopo jijini Dar es salaam.
Mbali ya kazi zake hizo Tatiana Durao amesema kazi atakayofanya akiwa nchini ni kurekodi kipindi chake kinachoitwa "Oh Tatiana" TV Series kitakachorushwa katika televisheni mbalimbali barani Afrika, amesema katika shughuli zake hizo atasherehekea siku yake ya kuzaliwa na watoto yatima wa Kituo cha Kiwohede na kuenda Zanzibar ambako pia anatarajia kurekodi kipindi chake hicho.

Tatiana Durao akiwa katikati akiwa pamoja na meneja wake Alice Mutumba wa kampuni ya True Media ya Uingereza na msaidizi wa Tatiana Ebmenalda Antonio.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment