TRAVELTINE YARINDIMA KWA MIDUNDO YA MIAMBA YA TAARAB NCHINI!!

Malkia wa taarab Bi. Kidude Baraka akitumbuiza usiku wa kuamkia leo katika hoteli ya Travertine, Magomeni Mapipa, jijini Dar katika onyesho kabambe akishirikiana na Jahazi Modern Taarab, Mwanahawa Ally na Babu Ayubu. Bi. Kidude ambaye yupo Dar kwa ziara fupi alikonga nyoyo za mamia ya mashabiki waliofurika ukumbini hapo kwa kibao chake kisichochuja cha MUHOGO WA JANG'OMBE.

Kiongozi wa Jahazi Modern Taarab, Mzee Yusuf, akimtambulisha malkia

Babu Ayubu alichangamsha na kibao chake kipya cha 'Jipu la kwapa' na 'Chaja ya Kobe' nyimbo ambazo anaigiza sauti ya Bi. Kidude na kuleta raha ya aina yake

Huu ni umati mkubwa wa mashabiki uliohudhuria katika onyesho hilo la kukata na shoka kweli lilikuwa ni onyesho kabambe
Bi. Kidude akiwa na Promota wa onyesho hilo John Tall (kushoto) na mwenyeji wake, Yasmin Razak

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment