Al Shabaab wafurusha wafanyikazi wa WFP, Somalia!

Moja ya picha inayoonyesha wafanyakazi wa shirika la mpango wa chakula duniani wakiwa kazini Nchini Somalia
Kundi la wapiganaji wa kislamu nchini somalia, Al-shabaab, wameamrisha shirika la Umoja wa Mataifa wa mpango wa chakula, WFP, kusimamisha shughuli zake na kuondoka nchini humo.
Kundi hilo linalodhibiti maeneo mengi ya kusini mwa nchi hiyo, limesema kuwa litachukua hatua dhidi ya raia yeyote wa Somalia anayeshirikiana na shirika hilo la WFP.
Kundi hilo limesema WFP linaangamiza wakulima nchini humo kwa kusambaza chakula cha bure nchini humo.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment