ESTERIANO MAHINGILA WA (BRELLA) APEWA TUZO NA ARIPO!!

Aliyewahi kuwa mwenyekiti wa (ARIPO) African Regional Intellectual Property Organization na Mkurugenzi mtendaji wa Msajili wa makampuni (BRELLA)Bw. Esteriano Mahingila akizungumza mbele ya waandishi wa habari wakati taasisi hiyo ya ARIPO ilipoongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam juu kusaidia nchi wanachama wa shiriki hilo Afrika katika kulinda na kuelimisha juu ya miliki haki ubunifu, ambapo pia taasisi hiyo inaendesha semina jijini Dar es salaam katika hoteli ya New Africa , inayohusu haki miliki ubunifu katika sekta ya kilimo, wanaofuatia katika picha ni Emanuel Sackey Mkuu wa utafiti RIPO, Grolia Binamungu Ofisa mkuu wa Leseni BRELLA na mwisho ni Flora Mpanju afisa kutoka ARIPO African.
Mkuu wa Utafiti wa shirika la ARIPO Emmanuel Sackey kulia akimkabidhi ngao Mkurugenzi Mtendaji wa Msajili wa Makapuni BRELLA Esteriano Mahingila kama heshima na kutambua mchango wa kazi zake wakati alipokuwa mwenyekiti wa tasisi hiyo ya ARIPO barani Afrika ambapo aliiongoza miaka miwili kwa mafanikio ARIPO ina wanachama 17 katika bara la Africa.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment