Naye Meneja matukio wa klabu hiyo Mahamed Bawazir akielezea zaidi amesema lengo la kuleta bendi tofauti katika klabu hiyo ni kuwapa wateja wake burudani tofauti kwa wakati tofauti ili kiula mmoja aweze kuridhika na kiwango cha burudani kinachotolewa na klabu hiyo ya kisasa nchini awali bendi za Akudo Impact na Fm Academia ziliwahi kutoa burudani katika vipindi tofauti kwenye klabu hiyo
Wakati huohuo katika kuadhimisha kumbukumbu ya kifo cha Baba wa Taifa Mwalimu J.K.Nyerere Mkurugenzi huyo wa ASET amesema wanamuziki wa bendi yake wamekusudia kumuenzi baba wa taifa kwa kufanya usafi maeneo yote ya nyumbani kwa Mwalimu huko Msasani, ameongeza kwamba kinachofanyika sasa ni kufuatilia taratibu zote zinazohusika ili kupata kibali cha kuwaruhusu wanamuziki hao kwa kushirikiana na baadhi ya mashabiki wenye mapenzi mema ili kumkumbuka mwalimu kwa kufanya usafi nyumbani kwake na maeneo yanayozunguka nyumbani kwa mwalimu.





0 comments:
Post a Comment