KISUMA BAR NDIYO WACHOMAJI BORA WA (NYAMACHOMA) 2009 TZ!!

Mwakilishi wa Kisuma bar akipokea zawadi ya shilingi milioni 1 kutoka kwa mkuu wa mkoa wa Dar es alaam Abbas Kandoro baada ya baa hiyo kuibuka kidedea katika uchomaji wa nyama. kulia ni Maneno mbegu meneja uhusiano wa kampuni ya bia TBL na kati ni Fimbo Butala meneja wa kilaji cha Safari Lager kilichodhamini shindano hilo.
Msndo bandi wakitoa burudani katika fainali hizo zilizoshirikisha baa tano ambazo ni Madrid Pub, Kisuma Bar, Africentre, Nguruko Bar na Titanic Bar Kisuma baa walishinda katika shindano hilo na kijinyakulia shilingi milioni 1 taslimu.

Majaji mwa shindano hilo wakionja nyama kutoka kwa mabanda matano yaliyoingia katika fainali kutoka kulia ni Doglas Sakibu, Clement Talawa na Lawrent Salvi.

Mkuu wa mkoa wa Dar es alaam Abbas Kandoro katikati aliyekuwa mgeni rasmi katika fainali za nyama choma 2009 katika viwanja vya Leaders jana akipata maelezo ya shindano hilo kutoka kwa meneja uhusiano wa TBL Maneno Mbegu kushoto ni Meneja wa kilaji cha Safari Lager Fimbo Butala.




You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment