GERALD HANDO APEWA ZAWADI NA MREMBO SALMA ALLY MSHIRIKI MISS KINONDONI!!

Mtangazaji wa kipindi cha powerbreakfast kinachorushwa na radia ya Cluods kila siku asubuhi akionyesha zawadi yake aliyopewa na Mrembo Salma Ally kwenye shindano la kipaji la Redds Miss Kinondoni lililofanyika jana kwenye hoteli ya Giraffe Ocean View Mbezi jijini Dar es salaam bango hilo lina ujumbe unaomhamasisha mwanamke kupambana na ugonjwa wa ukimwi na lina alama iliyochorwa kwa viganja vya mrembo huyo, viganja hivyo vinaandika alama "W" ambayo mrembo huyo ameelezea kuwa hiyo ndiyo nembo inayomuwakilisha mwanamke katika mapambano ya ukimwi hivyo katika jamii, hivyo Bw. Gerald Hando nadhani atautumia vyema ujumbe huo na kuueneza sehemu mbalimbali nchini hasa ukizingatia kwamba ni mtangazaji wa kituo cha redio kinachokubalika na rika zote katika jamii yetu hapa nchini.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment