DEMOKRASIA MAKINI WATOA RATIBA ZOEZI LA UCHAGUZI MKUU UJAO!!

Chama cha Demokrasia Makini makao makuu kinatoa taarifa kwa wanachama na wapenzi na umma kwa ujumla kuwa ratiba ya kuchukua fomu kwa ajili ya wagombeakatika nafasi za udiwani, ubunge na urais zitaanza kutolewa tarehe 1/7/2010 na kurudiswa tarehe 25/7/2010 tarehe 26/7/2010 hadi tarehe 10/8/2010 kura za maoni zitafanyika Bara na Visiwani .
Tarehe 12/8/2010hadi 16/8/2010 zitakuwa ni siku za kusikiliza rufaa tarehe 17/8/2010 ni siku ya uteuzi wa wagombea tarehe 19/8/2010 itakuwa ni uteuzi wa wagombea kwa tume taifa ya uchaguzi.
Na tarehe 20/8/2010 hadi tarehe 30/10/2010 zitakuwa ni siku za kampeni kwa wagombea wote tarehe 31/10/2010 ni siku ya upigaji kura, wote wenye mapenzi mema na chama hicho wanakaribiswa kuchukua fomu na kugombea katika nafasi hizo.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment