AJALI YA NDEGE KATIKA PICHA ILIYOTOKEA HUKO MANGA MKOANI TANGA!!

Sehemu ya ndege iliyopata ajali baada ya kutua barabarani kwa dharura na kugonga basi la watalii ambalo linaonekana juu kushoto likiwa limeanguka
Ndege ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania kikosi cha NGERENGERE ikiwa imeanguka na kuligonga basi la watalii waliokuwa barabarani katika eneo la MANGA mkoani TANGA na kusababisha rubani WAWILI wa ndege hiyo kupoteza maisha. Kwa mujibu wa taarifa rasmi, ndege hiyo yenye namba 9119 ilikuwa katika mazoezi.

Taarifa hiyo imesema askari wa JWTZ na polisi walifika eneo la tukio kwa ajili ya kuondoa ndege hiyo ambayo ilikuwa imelala katikati ya barabara na kuzuia magari ya kutoka ama kwenda Dar, Tanga na Arusha kwa masaa kadhaa. Picha na mdau Peter Mwakabwale. (Picha kwa hisani ya Michuziblog)

Askari wakagua na kusimamia ulinzi katika eneo la ajali


You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment