Inter yaichapa Barcelona, yatinga fainali..!!

Inter Milan's Alberto Milito Diego (right) and Walter Andrian Samuel celebrate after their UEFA Champions League semi-final second leg match vs Barcelona on April 28, at the Camp Nou stadium in Barcelona. Milan reached the final by beating Barcelona 3-2 on aggregate despite losing the second leg 1-0.
Inter Milan chini ya Jose Mourinho, ilicheza mechi ya kujihami kuizuia Barcelona isifunge zaidi ya goli moja na kufuzu kucheza fainali ya kombe la ligi ya vilabu bingwa barani Ulaya kwenye mechi iliyochezwa Nou Camp, himaya ya Barcelona.

Wakicheza ugenini na faida ya ushindi wa 3-1 walioupata nyumbani, Inter walilazimika kucheza kwa zaidi ya saa moja wakiwa na wachezaji 10 baada ya Thiago Motta kuonyeshwa kadi nyekundu kwa kumfanyia madhambi Sergio Busquets.

Lakini Barca walishindwa kufungua milango ya Inter mpaka mkwaju wa Gerard Pique ulipohitimisha mpambano huo mkali.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment