Mama Anna Abdallah amesema malengo makuu ya ulingo(TWCP) ni uwanja wa kuwaunganisha wanawake wanasiasa katika kujadili mustakabali wa nafasi na ushiriki wa wanawake katika uongozi kisiasa hapa Tanzania
TWCP ni rasilimali muhimu katika kuendeleza masuala ya kijinsia kwenye vyama vya siasa na kuweza kutumia fursa iliyopo kuandaa na kuunganisha nguvu katika kujengeana uwezo wa uongozi na kutafuta suluhisho kwa matatizo na vizingiti vya ushiriki na haki za akina mama katika medani ya siasa
Kushirikisha wanawake wengine bila kikwazo cha itikadi za kichama, kujijengea haki ya kukubalika kisheria na uhalali wa kutambuliwa kitaifa na kamataifa,
Ushiriki ulio sawa katika nyanja zote za maendeleo katika nchi pamoja na vyama vya siasa Tanzania
akimalizia amesema mwelekeo ni kuwezesha sauti za wanawake kwa umoja wao zisikike na kuhakikisha wanawake wanapata usawa kwa kuweka mikakati ya pamoja na kushiriki katika sdiasa ndani ya vyama vyao kwa usawa





0 comments:
Post a Comment