MKURUGENZI MTENDAJI WA ICF AKIZUNGUMZA NA WANAHABARI JANA!!

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la ICF barani Afrika Bw. Omary Issa akizungumza na waandishi wa habari wa vyomba mbalimbali kuelezea mambo mbalimbali yanayofanywa na shirika hilo katika nchi za Afrika katika kushirikiana na nchi hizo kurekebisha changamoto mabalimbali zinazokabili Tasisi za Ushuru na Forodha, akitolea mfano wa nchi ya Senegal ambayo amesema kazi ya kushughulikia malipo ya kodi na ushuru wa mizigo mbalimbali inayotoka nje ya nchi hiyo na kuingia inachukua siku moja tu, lakini akasema kwa Tanzania kwa mfano unapozungumzia utoaji wa mizigo Bandarini unahusisha idara zipatazo saba hivyo idara zote hizo zinatakiwa kwenda kwa kasi moja katika utendaji wa kazi zao ili kuweza kuondoa changamoto hizo, lakini pia amezungumzia mkutano wa mkubwa wa wawekezaji utakaojulikana kama ICF Investiment Climate Summit utakaofanyika jijini Dar es salaam kuanzia Mei 3-4 2010 na kukutanisha wadau mbalimbali, mkutano huo ulifanyika jana kwenye hoteli ya Kilimanjaro Kempinski.
Waandishi wahabari mbalimbali wakisikiliza mambo mablimbali yalioyoongelewa katika mkutano huo jana

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment