Profesa David mwakyusa azindua bodi mpya ya taaisisi ya utafiti wa madawa ya binaadamu- NIMR

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Profesa David Mwakyusa akiwasili makao makuu ya Taasisi ya Utafiti wa Madawa wa Binaadamu jijini Dar akiongozana na Katibu Mkuu wake Mh. Blandina Nyoni mchana huu kuzindua bodi ya taasisi hiyo. Nyuma toka shoto ni Dk. Mwele Malecela, Mganga Mkuu Kiongozi, Dk. Deo Mtasiwa na mwenyekiti mpya wa bodi hiyo Profesa Samuel Maselle

Profesa David Mwakyusa akiwa na Katibu Mkuu Blandina Nyoni na Mganga Mkuu Kiongozi katika picha ya pamoja na wajumbe wa bdoi mpya ya NMR aliyoizindua leo. Wajumbe wa bodi hiyo mpya ni pamoja na Mbunge wa Mbozi Magharibi Dk. Luka Siyame, Dr Hassan Mshinda, Dr. Edith Ngirwamungu, Jonathan Tangwa, Dr Alaick Abdallah Juma, Profesa Eligius Lyamuya, Dk. Catherine Kuwite, Bi. Elli Pallangyo, Elisa Mjema, Dk Salim Mohamed Abdullah na Dk. Mwele Malecela ndiye katibu wa bodi hiyo

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment