Mapigano yavunja mkataba wa Darfur!

Imearifiwa kuzuka upya mapigano katika jimbo la Darfur licha ya Rais wa Sudan Omar al-Bashir kutangaza kusitishwa kwa vita eneo hilo la magharibi.
Kundi la kutoa misaada ya utabibu la Ufaransa liitwalo Medecins du Monde limesema limesimamisha harakati zake katika eneo la kati la Darfur la Jebel Marra.
Kundi la waasi wa Sudan Liberation Army (SLA) limedai kumetokea mapigano makali usiku wa Jumatano.
SLA hawakuafikiana na mkataba wa kusitisha mapigano ambao wiki hii serikali ya Sudan ilikubaliana na kundi jingine kubwa la waasi la Jem.
Msemaji wa kundi linalounga mkono SLA Abdel Wahid Mohamed el-Nur amesema majeshi ya serikali yalishambulia maeneo kadha ya milimani, ukiwemo mji wa Deribat.
Hata hivyo upande wa jeshi la Sudan umekanusha kutokea mapigano yoyote. http://www.bbcswahili.com/

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment