MAKUMBUSHO VILLAGE NA MZALENDO PUB KULIWAKA MOTO USIKU WA KUAMKIA LEO!!

Elystone Angai ambaye ni kiongozi wa bendi ya Mashujaa Music Band akiimba jukwaani wakati bendi hiyo ilipofanya onyesho lake la kwanza kwenye vijiji vya makumbusho kwa mafanikio makubwa huku ikifanikiwa kuteka hisia za mashabiki waliohudhuria kwenye onyesho hili, kutokana na wanamuziki wa bendi hiyo kufanya mambo makubwa katika kila idara hivyo kulimudu vyema jukwaa la vijiji vya Makumbusho ambalo awali bendi ya FM academia ilikuwa ikifanya onyesho lao hapo kila jumamosi lakini sasa ni wakati mwingine na ni zamu ya wana Mashujaa Music Band, hebu mdau watembelee kila jumamosi uone shughuli yao pevu.


Hapa ni shoo kwa kwenda mbele kama unavyoona wanenguaji hawa wakinyonga viuno vyao kisawasawa.

Elystone Angai kiongozi wa Bendi hiyo kulia akiongoza mashambulizi jukwaani huku akiwa analikung'uta gitaa la solo.
Mashabiki mbalimbali wa bendi hiyo wakijimwaga ukumbini hapo wakati bendi hiyo ilipokuwa ikitumbuiza kwenye vijiji vya Makumbusho usiku kwa kuamkia leo jijini Dar es salaam.
Yohana "ndugu yake na hela" wapili kulia ambaye ni mdau mkubwa wa Mashujaa Music Band naye alikuwepo kushuhudia burudani hiyo kali kutoka kwa vijana hao ambao wanakuja kwa kasi ya ajabu akiwapa stori marafiki zake.

Huyu ndiye Flora Bamboocha mmoja wa wanenguaji wa Mashujaa Band hapa akifanya vitu vyake jukwaani.
Hawa ndiyo vimwana wa bendi ya Mashujaa Music Bandi iliyokuwa ikiporomosha burudani kali pale vjiji vya Makumbusho usiku wa kuamkia leo.

Dj Makay akiwa kwenye mashine na kufanya mambo makubwa yaliyowafanya wapenzi wa muziki kushindwa kukaa kwenye viti vyao na kucheza muziki kwa muda wote pale Mzalendo Pub Makumbusho, kushoto ni Dj Juice, kulia ni eorge Nzunda na Jofrey Mwakibete kutoka Mo Blog.
Dj Bony Luv katikati na Dj Makay kushoto na rafiki yao wakishoo love.
Wapenzi wa muziki wakitibwilika kwenye ukumbi wa Mzaleno Pub ambapo kila jumamosi kunapigwa disko la kukata na shoka kutoka kwa Dj Bony Luv, Dj Maky na wengine hii ilikuwa usiku wakuamkia leo.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment