JERRY MURRO ADAIWA KUNASWA NA POLISI KWA RUSHWA!!

Mwandishi wa habari Bora wa jumla mwaka 2009 kutoka Televisheni ta TBC Jerry Murro inadaiwa amekamatwa na polisi na yuko kituo cha polisi kati (Central) jijini Dar es salaam kwa mujibu wa blogu ya Issamichuzi.blogspot.com Jerry Murro alikamatwa leo jijini akitaka kupokea kitita cha shilingi milioni 10 kutoka kwa mwananchi mmoja katika mtego uliokuwa umetegwa dhidi yake
Kamanda wa polidi wa kanda maalum ya Dar es salaam Suleiman Kova anatarajiwa kutoa taarifa wakati wowote kuhusiana na sakata hilo na tutawaletea taarifa zaidi mara baada ya kupata taarifa zaidi.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment