Obama ataka majibu kuhusu usalama

Rais Barack Obama wa Marekani.
Rais Barack Obama ametaka vyombo vya usalama vya marekani kueleza mara moja ni kwa nini habari kuhusu raia wa Nigeria aliyejaribu kulipua ndege ya marekani hazikutumiwa ipasavyo.
Bwana Obama amezipa idara za usalama hadi alhamisi tarehe 31, kueleza jinsi Umar Farouk Abdulmutallab alivyoruhusiwa kupanda ndege ya marekani wakati ambapo tahadhari ilikuwa imetolewa kumhusu.
Wazazi wa Umar walikuwa wametahadharisha ubalozi wa marekani nchini Nigeria kuhusu mwenendo wa mwana wao.
Obama ameshutumu idara hizo kwa uzembe ambao nusura ungesababisha maafa. Amesema kuwa iwapo habari kumhusu Umar zingetumiwa vilivyo na idara za usalama, raia huyo wa Nigeria hangeruhusiwa kusafiri.
Umar mwenye umri wa miaka 23 alikuwa amejaribu kulipua ndege ya Marekani iliyokuwa na abiria 300 mnamo tarehe 25 mwezi desemba.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment