Waziri Marck Mwandosya amesema wakazi wa jiji la Dar es salaam wasiwe na wasiwasi wowote bali waendelee kutumia maji hayo kwa ni uchunguzi wa kina umefanyika na kugundua kwamba hakuna sumu yoyote ambayo imepatikana katika chanzo cha mtambo wa Ruvu juu ambako ndiyo husukuma maji kuja katika jiji la Dar es salaam kwa matumizi ya wakazi wa jiji.
Amesema eneo ambalo tukio hilo lilitokea ni sehemu iitwayo Kwala katika Wilaya ya Morogoro Kusini lilitiwa sumu kwa lengo la kuvua samaki na wavuvi haramu ni kilomita sabini mpaka kufikia kwenye chanzo cha mtambo wa Ruvu Juu, hivyo hakuna wasiwasi wowote wa kuwepo kwa sumu hiyo na mpaka sasa Sampuli ya maji iko kwa mkemia mkuu ili kubaini kama kuna tatizo lolote pamoja na kwamba uchunguzi wa awali umeonyesha hakuna aina yoyote ya sumu katika maji hayo, wanaofuatia kwenye picha ni Kaimu katibu mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji Damas Shirima na mwisho ni Mkurugezi wa Idara ya Habari Maelezo Clement Mshana.





0 comments:
Post a Comment