Pamoja na Bendi hiyo Kukubalika na mashabiki kutokana na uwezo wao katika kupiga muziki lakini pia Josse Mara amechangia kwa kiwango kikubwa bendi hiyo kukubalika na watanzania wengi kwani yeye ndiye anayebeba utanzania halisi katika bendi hiyo hivyo anastahili kupongezwa kutokana na uwezo wake lakini pia kufanya kazi na wenzake kwa ufanisi mkubwa katika bendi hiyo, usiku wa kuamkia leo Camera ya FULLSHANGWE baada ya kutoka kwenye uzinduzi wa Swahili Fashion week ilijimuvuzisha mpaka kule Equator Grill Mtoni na kuwafuma jamaa wakikamua vilivyo huku vimwana wa bendi hiyo wakitakatisha jukwaa kitu kilichomfanya kamanda mshika Camera wa FULLSHANGWE aahirishe zoezi la kuwapotezea wakali hao wa muziki wa Bongo na kuanza kufyatua picha mbalimbali za matukio katika onyesho hilo.
MKALI JOSSE MARA ANAVYOFANYA MAMBO FM ACADEMIA!!
Posted by
ADMIN
You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)





0 comments:
Post a Comment