Pius Aloysius ateuliwa Mkurugenzi wa Bodi ya NBAA!!

Waziri wa Uchumi na Fedha Mustafa Mkulo
Benjamin Sawe Maelezo Dar es Salaam
Waziri wa Fedha na Uchumi Mh..Mustafa Mkulo amemteua Bwana Pius Aloysius Maneno kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu kuanzia tarehe 22 mwezi wa nane mwaka 2009 Taarifa iliyotolewa na msemaji wa Wizara ya Fedha na Uchumi Ingiaedi Mduma imesema kuwa uteuzi huo ni kwa mujibu wa kifungu cha 6 cha sheria namba 33 ya mwaka 1972 na kurekebishwa na sheria namba 2 ya mwaka 1995 iliyoanzisha NBAA. Hapo awali Bwana Pius alikuwa Meneja wa Corporate Service na alikuwa anakaimu nafasi ya Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment