Na Anna Nkinda – Maelezo
Elimu ya dini na elimu ya mazingira vikichanganywa kwa pamoja nchi itapata wataalamu wa hali ya juu ambao watasaidia kuleta maendeleo ya nchi..
Hayo yamesemwa leo na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati akiongea na washiriki wa mashindano ya kuhifadhi Qur’an tukufu yaliyofanyika katika Hoteli ya Movenpick iliyopo jijini Dar es Salaam.
Mama Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) aliwataka waandaaji wa mashindano hayo ambao ni ubalozi wa Misri kupitia kituo chake cha utamaduni kiitwacho Egyption Islamic Center kilichopo Chang’ombe na Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) mkoa wa Dar es Salaam kuona umuhimu wa kujenga kituo kama hicho katika mikoa mingine.





0 comments:
Post a Comment