JAFARAI AWAMWAGIA MASHABIKI WAKE "WALI NAZI"!!

Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya Jafarai amesema tayariamekamilisha Albam yake mpya inayokwenda kwa jina la Wali Nazi ambayo itakuwa na nyimbo 9 Jafarai amezitaja nyimbo zilizomo kwenye albam yake hoyo mpya kuwa ni Wali Nazi yenyewe, Msijisahau, Jafarai, Saa Nyingine, Unapenda, na Ye na Mimi, amesema kuwa nyimbo zote zimerekodiwa katika studio za Fish Crub za hapa jijini huku akiwa amewashirikisha wanamuziki Naazizi kutoka Kenya, Lamaa ambaye pia ni Producer wa albam hiyo na Wateule, albam hiyo itakuwa sokoni wakati wowote kuanzia sasa na itapatikana kote nchini.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment