ZAIN YAANGUSHA PATY YA NGUVU KUUAGA MWAKA 2008 NA KUMKABIDHI CHETI MFANYAKAZI BORA!!


Meneja Uhusiano wa Zain Tanzania, Beatrice Mallya (kulia) akipokea cheti kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Zain Tanzania Khalid Muhtadi baada ya kuibuka mfanyakazi bora wa kitengo cha uhusiano wakati wa hafla ya wafanyakazi wa Zain kuuaga mwaka 2008, kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam wiki hii.


Wafanyakazi wa kitengo cha huduma kwa wateja wa Zain Tanzania, wakishangilia huku wakiinua juu kombe baada ya kuibuka washindi wa kudansi wakati wa hafla ya wafanyakazi wa Zain kuaga mwaka 2008, Dar es Salaam wiki hii.

Mameneja Masoko wa Zain Tanzania, Kelvin Twissa (kushoto) na Costantine Magavilla wakitumbuiza kwa kuimba wakati wa hafla ya wafanyakazi wa Zain kuaga mwaka 2008, Dar es Salaam wiki hii



Meneja Uhusiano wa Zain Tanzania, Beatrice Mallya (kulia) na Dangio Kaniki wakiwaongoza wenzao wa idara ya utawala na uhusiano wa umma kucheza wakati wa hafla ya wafanyakazi wa Zain kuaga mwaka 2008, Dar es Salaam wiki hii.


Meneja Kumbukumbu wa Zain Tanzania, Hilda Nakajumo (mbele) akiwaongoza wenzake kucheza dansi wakati wa hafla ya wafanyakazi wa Zain kuaga mwaka 2008, Dar es Salaam wiki hii.


You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment