MATONYA NDANI YA BUJUMBURA


Msanii wa Muziki wa Bongofleva maarufau kwa jina la Matonya anatarajia kuwa na Ziara ndefu ya kimuziki katika Afrika mashariki Ulaya na Marekani ambapo anatarajia kuanzia nchini Burundi.
Matonya ametutonya kwamba katika sikukuu ya Idd atakuwa mjini Bujumbura kwa maonyesho kadhaa ya kimuziki kabla hajarejea nyumbani na kujiandaa kwa maonyesho mengine hapa nyumbani kabla ya kuanza ziara nyingine kama hiyo katika bara la Ulaya na Marekani mwishoni mwa mwaka huu.
Hakutaka kutaja kampuni ambayo ameingia nayo mkataba wa maonyesho hayo kwa madai kuwa wakati ukifika ataitaja lakini amesema kila kitu kiko sawa na akitoka burundi anarudi kujiandaa na tamasha kubwa la Fiesta litakalofanyika huko Tanga tarehe nne mwezi ujao na mikoa mingine kisha yataanza maandalizi ya safari ya Ughaibuni akianzia na Uholanzi, Ujerumani na baadae Marekani.
Sawa Matonya sisi Tunakutakia Maandalizi Mema na Safari Njema!

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment