MALOU STOUNCH AREJEA FM ACADEMIA

Mwanamuziki wa siku nyingi na maarufu hapa nchini anayejulikana kwa jina la Malou Stounch na aliyeahi kutamba na kundi la Fm Acadimia (wajelajela) amerejea katika kundi la muziki la Fm Academia (Original) habari zilizoifikia FULLSHANGWE zinasema mwanamuziki huyo atatambulishwa rasmi katika onyesho la sikukuu ya Eid El Fitr litakalofanyika kwenye kijiji Cha makumbusho kijitonyama.
Akizungumzia zaidi Meneja wa Bendi hiyo Mujibu Khamis amesema katika onyesho hilo pia Bendi hiyo itatambulisha mtindo wake mpya unaoitwa (Zombolo na Matembele) Yaani kwa Kiswahili (Samaki na Matembele)
Mujibu ameongeza kuwa mtindo huo utakuwa tishio kama wanavyojulikana Fm Academia kwa kutoa burudani kali hilo mashabiki watashuhudia wenyewe hapo makumbusho katika sikukuu ya Idd
Wakati huohuo Mujibu amesema mwanamuziki Nguli wa Jamhuri ya kidemokrasia ya kongo General Def Defao anatarajia kutoa buruda ni ya kukata na shoka katika mikoa ya kandaya Ziwa katika mikoa ya Mwanza Kagera na ambapo katika sikukuu ya idd Mosi atakuwa Mwanza na Idd pili atakuwa Bukoba na Idd tatu atakuwa Geita wakazi wa huko kaeni mkao wa kula burudani hiyoooo! inakuja

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment