MAMA MALKOMITO!
Paulin Zongo AKA Mama Malkomito


Mwanamuziki Paulin Zongo ambaye aliwahi kutamba akiwa na Bendi ya TOT Yuko mbioni kukamilisha Albam yake itakayokuwa na nyimbo Nane.


Akizungumza na FULLSHANGWE jijini Zonga amaesema tayari amekwisharekodi nyimbo Sita na sasa hivi yuko mbioni kumalizia nyimbo mbili zilizobaki, amezitaja nyimbo hizo kuwa ni Umechezea Bahati, Kifo cha mama,Mimi na wewe Daima,Dunia ni ndogo Remix, Safari Remix, Hatuendi hivyo na Usibahatishe Pia Heshima ambazo ndiyo anamalizia kuzirekdi studio,


Zongo ameongeza kuwa albamu hiyo itawaonyesha mashabiki wa wake kuwa bado yupo kwenye Gemu na uwezo wa kufanya kazi nzuri upo na ninajua wayapata burudani murua kupitia albam yangu hiyo.


Ameongeza kuwa amerekodi katika studio tofauti ili kuleta radha tofauti ya muziki kwani kila producer ana uwezo wake na kipaji chake kama tulivyo sisi wanamuziki


amezitaja studio hizo kuwa ni (Big Tone, Metro, Dream Studio na Soundcrafters! albam hiyo inatarajiwa kuingizwa sokoni mwishioni mwa mwaka huu lakini kwanza nitaingiza single mbili moja kwenye vituo vya Televisheni na nyingine kwenye vituo vya Redio ili kuwaonjesha mashabiki wangu sambamba na kuanza kwa bendi yangu itakayojiulikana kama Zongo Band (The Dream)

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment