Mkutano wa Kamati Kuu ya CCM Dodoma leo!!

Katibu mkuu wa CCM Yusuf Makamba akimkaribisha Mwenyekiti wa CCM Taifa,Rais Jakaya Mrisho Kikwete katika ukumbi wa White House tayari kuongoza kikao cha kamati Kuu ya CCM mjini Dodoma leo asubuhi.

Mwenyekiti wa CCM Taifa ,Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza kikao cha Kamati kuu ya CCM mjini Dodoma leo asubuhi.Wengine waliokaa meza kuu kutoka kushoto ni Rais Mstaafu awamu ya Tatu Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu awamu ya Pili ali Hassan Mwinyi, Rais wa Zanzibar Amani Abeid Karume,Katibu Mkuu wa CCM Yusuf Makamba, makamau mwenyekiti wa CCM Bara Pius Msekwa na Rais Mstaafu wa Zanzibar Salmin Amour.

Wagombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM Makamu wa Rais Dr.Ali Mohamed Shein na Waziri kiongozi wa SMZ Shamsi Vuai Nahodha wakisalimiana katika viwanja vya makao Makuu ya CCM mjini Dodoma leo asubuhi (picha na Freddy Maro)

Mgombea Urais wa Zanzibar ambaye pia ni Waziri kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Shamsi Vuai Nahodha akisalimia baadhi ya wanachama wa CCM mjini Dodoma muda mfupi kabla ya kuanza kikao cha Kamati kuu ya CCM.

Mgombea urais wa Zanzibar Balozi Ali Karume akisalimia baadhi ya wanachama wa CCM jinni Dodoma leo asubuhi.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment