HUU NDIYO MTITI WA KUNDUCHI BAADA YA WATOTO KUGONGWA NA KUFA!!

WAKAZI wa Kunduchi Mtongani jijini Dar es Salaam, leo walizua kizazaa baada ya kuifunga barabara kuu inayotoka Mbuyuni kuelekea eneo hilo kufuatia gari aina ya Toyota Hiace linalofanya shughuli za daladala kati ya Kunduchi na Mwenge kuwagonga na kuwaua watoto wawili wa familia moja. Vurugu hizo zilisababisha askari wa kutuliza ghasia FFU, kutumia mabomu ya kutoa machozi ingawa baadaye walikatazwa kutumia mabomu hayo na askari wa JWTZ wa kambi iliyopo jirani na eneo hilo kutokana na muingiliano wa mionzi kati ya mabomu hayo na vifaa vyao. Picha kwa hisania ya http://www.globalpublishers.info

Dereva wa pikipiki (mwenye fulana ya pundamilia) akipewa kichapo na akina mama baada ya kutaka kupita kinguvu eneo lililofungwa.

Akina mama wakimueleza kilio chao afisa mmoja wa polisi aliyekuwa akiwataka kuacha vurugu.

Barabara ikiwaka moto baada ya wananchi kuchoma matairi ya gari katikati ya barabara.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment