TANZANIA TUMRUDIE MUNGU!! (MTUME APOSTLE MATAMBO).

Mtume Apostle Matambo akiongea na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo akisema ametumwa na mungu kuja kuwaambia Watanzania watubu dhambi zao na kumrudia mungu ili wasamehewe, akinukuu baadhi ya vifungu katika Biblia takatifu amesema Mungu anatuagiza watu wote tutubu (mdo. 17:30)bila kuangalia dini wala dhehebu la watu (Yona.3:4-10) mfalme ilibidi atangaze toba kwa nchi nzima(lk.13:3 tusipotubu tutaangamia (mdo.3:19)mungu anasema nirudieni mimi (Yoel.2:12-13) mwisho mungu atatusamehe dhambi zetu zote (Isaya.55:7). akamalizia mtume huyo, kulia ni afisa habari wa Iadara ya habari maelezo Bw.Tiganya
Waandishi hawa wakionekana wanyenyekevu wakati wa maombi waliyoombewa na mtume Apostle Matambo ili waweze kufanya kazi zao kwa haki na waongezewe vipato vyao na waajiri wao.

Baadhi ya waandishi wa habari wakiombewa katika ukumbi wa Idara ya Habari maelezo wakati mtume Apostle Abraham Matambo wa kanisa la Holy City Tample Ministry alipoongea na wasandishi wa habari na kusema kwamba ameletewa ujumbe na mwenyezi mungu juu ya watanzania kutakiwa kumrudia mungu na kuomba Toba ili wasamehewe dhambi zao.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment