De Plaizir amsifu Banana zoro!
Mwanamuziki kutoka nchini Congo,Blanchard De Plaizir anayefanyia shughulizake na muziki nchini Uingereza,aliyewasili nchini wiki iliyopita,amsifiamwanamuziki Banana wa nchini baada ya kusikiliza kazi zake palealipohudhuria moja ya shoo za B Band,Hunters.

Mwanamuziki huyo alisema ya kwmaba Tanzania imejaliwakuwa na wanamuziki wenye vipaji hivyo wanatakiwa kufanyia kazi vipaji hivyo ili waweze kusikika kimataifa.Aliweza kumtolea mfano mwanamuziki Banana kwa kusema ya kwamba Banana nimwanamuziki mzuri lakini anahitaji kusikika zaidi nje ya Tanzania ili aweze kukubalika.

“Nimeweza kushuhudia wanamuziki mbalimbali kwa muda niliokaa nao,nimependa jinsi Banana anavyofanya kazi zake,kwani ni mwanamuziki aliyebarikiwa kuwa na kipaji.Mbali na hayo, De Plaizir atarekodi nyimbo moja na mwanamuziki huyo pamoja na baadhi ya wanamuziki kutoka bendi ya Akudo kwakuwa anahitaji kupata kumbukumbu ya wanamuziki kutoka nchini.

“Narekodi ngoma na Banana pamoja na baadhi ya wanamuziki wa Akudo ili tu niweze kuweka kumbukumbu yangu hapa nchini,wimbo utakuwa bora na wakimataifa zaidi,kaeni tayari”Alisema.Mwanamuziki huyo ambaye anatarajia kuondoka nchini wiki hii baada ya kukamilisha kazi ya kurekodi na wanamuziki hao.

You liked this post? Subscribe via RSS feed and get daily updates.

0 comments:

Post a Comment