Na Mdau Asha Kigundula,Cairo Misri
WACHEZAJI wa Simba wametakiwa kuiondolea Tanzania aibu kwa kuwafunga wapinzani wao katika mchezo wao wa kesho dhidi ya Haras El Hadood utakafanyika mjini Alexandria nchini hapa.
Akizungumza na wachezaji hao mjini hapa juzi Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Misri Jestas Nyamanga, alisema kuwa kuwafunga Haras El Hadood kutaijengea nchini heshima.
Nyamanga alisema kuwa ni muhimu mkubwa sana kuweka utaifa mbele kwa kuwa sasa ndiyo timu pekee iliyobaki katika mashindano ya kimataifa kwa Tanzania.
Alisema kuwa Simba ina kila sababu ya kuwatoa wapinzani wao hao kutokana na maandalizi mazuri iliyopata ikiwa ni pamoja na kuweka kambi mjini hapa kwa muda wa siku tano.
Nyamanga alisema kuwa licha ya kuwa wapinzani wao wana mbinu nyingi lakini ana uhakika wachezaji hao wakiamua wana uwezo mkubwa wa kuwang’oa wapin zani wao.
Naye Afisa wa Ubalozi Ibrisa Juma alisema kuwa kutokana na kauli za wamisri kwa timu za Tanzania itakuwa jambo kubwa na nzuri kwa timu ya Simba kuwaondoa wapinzani wao hao.
Juma alisema kila mara wamekuwa wakizomewa kwa kuwaambiwa timu za Tanzania haziwezi kufanya lolote katika mashindano yoyote nchini hapa.
“Tuna kila sababu ya kujivunia kwa kuwaondoa wapinzani wetu katika manshindano haya wanatudharau sana…endapo tutawaondoa nasiu watatuheshimu”alisema Juma.
WACHEZAJI wa Simba wametakiwa kuiondolea Tanzania aibu kwa kuwafunga wapinzani wao katika mchezo wao wa kesho dhidi ya Haras El Hadood utakafanyika mjini Alexandria nchini hapa.
Akizungumza na wachezaji hao mjini hapa juzi Kaimu Balozi wa Tanzania nchini Misri Jestas Nyamanga, alisema kuwa kuwafunga Haras El Hadood kutaijengea nchini heshima.
Nyamanga alisema kuwa ni muhimu mkubwa sana kuweka utaifa mbele kwa kuwa sasa ndiyo timu pekee iliyobaki katika mashindano ya kimataifa kwa Tanzania.
Alisema kuwa Simba ina kila sababu ya kuwatoa wapinzani wao hao kutokana na maandalizi mazuri iliyopata ikiwa ni pamoja na kuweka kambi mjini hapa kwa muda wa siku tano.
Nyamanga alisema kuwa licha ya kuwa wapinzani wao wana mbinu nyingi lakini ana uhakika wachezaji hao wakiamua wana uwezo mkubwa wa kuwang’oa wapin zani wao.
Naye Afisa wa Ubalozi Ibrisa Juma alisema kuwa kutokana na kauli za wamisri kwa timu za Tanzania itakuwa jambo kubwa na nzuri kwa timu ya Simba kuwaondoa wapinzani wao hao.
Juma alisema kila mara wamekuwa wakizomewa kwa kuwaambiwa timu za Tanzania haziwezi kufanya lolote katika mashindano yoyote nchini hapa.
“Tuna kila sababu ya kujivunia kwa kuwaondoa wapinzani wetu katika manshindano haya wanatudharau sana…endapo tutawaondoa nasiu watatuheshimu”alisema Juma.





0 comments:
Post a Comment